Lukolo
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 5,143
- 3,209
Hivi jamani hawa polisi wa Tanzania huwa wanafanya mambo haya kwa faida ya nani? Inashangaza sana kututangazia kwamba FBI wapo Arusha wanasaidiana na polisi wetu kufanya uchunguzi kuhusu mlipuko wa bomu kwenye mkutano wa CHADEMA, ilihali ni uongo mkubwa kabisa.
Kusema ukweli, hata mimi ningeshangaa kama polisi waliorusha bomu na kupiga watu risasi wangeleta FBI kufanya uchunguzi. Maana kisheria na taratibu FBI huwa hawana unafiki, na hawana tabia ya kuandika report za uongo. Kwa hakika wangewaumbua polisi wauaji wa Tanzania na serikali yake ya kigaidi.
Juzi hapa viongozi wa CHADEMA wamelalamika kwamba hawajakutana na FBI hata mmoja kwa ajili ya kuwauliza chochote kuhusiana na mlipuko, na walionyesha kushangaa kwamba hao FBI wanafanya kazi na nani! Lakini taarifa za uhakika kutoka ubalozi wa marekani kama zilivyoripotiwa na gazeti la The citizen zinaonyesha kwamba FBI hawapo Arusha, na kamanda wa polisi wa Arusha alipoulizwa alithibitisha hilo.
Sasa ninajiuliza walipotutangazia kwamba FBI wapo Arusha walitaka nini? Ni dhahiri walitaka kupika report ya uongo na kukizushia kesi chadema na ili wasingizie kwamba FBI ndiyo wamegundua hayo!
Hivi katika haya, tuendelee kuwa na imani na jeshi la polisi? Hivi CCM wameshindwa kabisa kucheza fair game hadi watake kufanya haya jamani?
US security agents not in Arusha, says embassy - National - thecitizen.co.tz
Kusema ukweli, hata mimi ningeshangaa kama polisi waliorusha bomu na kupiga watu risasi wangeleta FBI kufanya uchunguzi. Maana kisheria na taratibu FBI huwa hawana unafiki, na hawana tabia ya kuandika report za uongo. Kwa hakika wangewaumbua polisi wauaji wa Tanzania na serikali yake ya kigaidi.
Juzi hapa viongozi wa CHADEMA wamelalamika kwamba hawajakutana na FBI hata mmoja kwa ajili ya kuwauliza chochote kuhusiana na mlipuko, na walionyesha kushangaa kwamba hao FBI wanafanya kazi na nani! Lakini taarifa za uhakika kutoka ubalozi wa marekani kama zilivyoripotiwa na gazeti la The citizen zinaonyesha kwamba FBI hawapo Arusha, na kamanda wa polisi wa Arusha alipoulizwa alithibitisha hilo.
Sasa ninajiuliza walipotutangazia kwamba FBI wapo Arusha walitaka nini? Ni dhahiri walitaka kupika report ya uongo na kukizushia kesi chadema na ili wasingizie kwamba FBI ndiyo wamegundua hayo!
Hivi katika haya, tuendelee kuwa na imani na jeshi la polisi? Hivi CCM wameshindwa kabisa kucheza fair game hadi watake kufanya haya jamani?
US security agents not in Arusha, says embassy - National - thecitizen.co.tz