FBI Hawapo Arusha, polisi ni wazushi!

FBI Hawapo Arusha, polisi ni wazushi!

Nimeipenda hii habari. Thanks to the US Embassy for clarity!

Hii inaonkena RC Arusha na RPC wake walichomekea habari ya FBI ili kuwalaghai Watanzania kwamba Polisi hawahusiki! Tumesikia pia RC Mulongo(call him Muongo) akidai kuwa upelelezi wa awali wakihusisha hao FBI ati ulionyesha mipango ya Bomu la Soweto ilipangwa Arusha!!!!!!Pia tumnesikia kuhusu ujio wa Wachina kutambua hilo Bomu lao ati nani walimuuzia na lini? Zote hizi ni propaganda na longolongo za kutaka kuwazubaisha Watz na mwisho wa siku hakuna lolote wala chochote!!!Nji hii bana.......!!!!!!!!!!!

Huyu RC Arusha ni muongo kama jina lake! Sijiui nini kinamwasha mpaka awe msemaji wa Polisi ilhali hiyo ilikuwa ni kazi ya Chagonja ambaye mpaka sasa hajakamata hata nzi aliyekuwa akinusa damu ya marehemu na majeruhi.
 
Polis wanazidi kujianika kwamba wanahusika na ulipoaji bomu. Uongo wote huu wa nini? walitaka baada ya mda waje na picha ya mtuhumiwa hewa huku wakitutangaizia imechorwa na FBI. Siku zinakuja nazo si nyingi polisi wetu wataumbuka tu
 
Wakuu.

Mtakumbuka kuwa hivi karibu jeshi la Polisi lilisema kuwa FBI wako Arusha kwa ajili ya uchunguzi wa bomu lililo lipuka kwenye mkutano wa CHADEMA. Walidai bomu limetoka CHINA na tayari na wataalamu kutoka China nao wametua Arusha kwa uchunguzi.

Ubalozi wa Marekani umeliumbua jeshi la Polisi kwa kueleza kuwa FBI walio tajwa na kuwa wapo nchini hawapo. Hapa banaibua maswali mazito kuwa Polisi wanaficha nini na tutawaamini vipi wakisema hata wataalamu kutoka China nao wapo?!
 
Policcm ni waongo, wameusika katika mlipuko huo na wanahadaa wananchi. Kama Police wanaongopa, who is going to work with them? Shame on Policcm
 
Hao ndio POLICCM bwana,yalikuwa ni maneno ya uongo kuwahadaa watanzania ili wawe na imani kuwa jambo lile linashughulikiwa kitu ambacho si kweli na ilikuwa vigumu kuwaalika FBI waje wachunguze wakati wao ndio watuhumiwa wakuu.
 
Kwani yule jamaa aliyetumwa kule Arusha na Saidi Mwema bado yupo huko? Kawa mkimya sana, kila siku uongo tu, wakiambiwa polisi wamepoteza legitimacy wanakataa, haya sasa, kiko wapi?
 
red brigade inawatisha si ulisikia kwenye kongamano la demokrasia(la wale makada wa ccm,nccr tlp,udp,cuf)kikwete alimwambia mrema kuwa vurugu zikizidi mrema atakimbilia kenya sasa mimi(kikwete) nitakimbila wapi? hapo tuna raisi au (masanja mkandamizaji?)
 
daaah..hi nchi ishakuwa kiraka..hakuna mkweli tena kwenye hii serekali ya sisiemu..
ALAFU 2015 KIONGOZ WA CCM ANAKUDANGANYA ATAKUTEKELEZEA a, b, c na ww unakubali kirahis..hii serekali ni waongo watuuuupu sasaaa..
 
Duh! Mbna polisi wamejidhalilisha hvyo? Tutawaamin kwa lipi sasa?

Ngoja tuone reaction ya FBI kwa kuhusishwa kutumika "hewa" kwenye hiyo milipuko. Yan polisi wa bongo bure kabisa kwenye strategies.
 
sio tu kwamba jeshi la polisi limekosa weledi,hata aibu tu pia halina.

Mkuu.
Kwa kauli ya ubalozi wa Marekani ni kwamba jeshi la Polisi lenye dhamana ya kulinda usalama wa raia wake limewadanganya wananchi wake walio kuwa na shauku ya kutaka kujua uchunguzi wa FBI utaibuka na majibu gani juu ya usalama wao na ndugu zao waliopoteza maisha kwenye tukio.

Kama jeshi lenye dhamana ya kulinda usalama wa wananchi linatoa taarifa za uwongo kwa wananchi, wananchi watakuwa na sababu gani la kuwa na imani na jeshi lao?! Jeshi hilohilo limeshutumiwa kuwa ndio limehusika na ulipuaji wa Bomu, tutaacha vipi kuamini kuwa waliamua kuwataja FBI kuwa wapo kwenye uchunguzi ili kutupa imani kuwa wanajali usalama wetu kumbe si kweli huku wakiju ukweli wa mambo?!

Kwa namna ya pekee kabisa, na kutoka chini ya uvungu wa sakafu ya moyo wangu, Polisi imedhihirisha tena kuwa haiwezi kubeba matumaini yangu kwao.
 
Kweli jeshi letu lipemoteza mwelekeo na linakimbia kivuli chake. Kiwewe hiki kwa sababu damu za waTZ wasio na hatia zinawalilia.
 
Hii fedheha kubwa kwa Taifa letu na naendelea kujiuliza mara kwa mara kwamba hivi mpaka lini huu Utawala wa Mbayuwayu utaendelea kuliletea Taifa aibu kwasababu ya mambo ya ajabu ajabu?

Najua Mbayuwayu na wenzie Serikalini hii kwake si ishu kubwa sana maana ameshafanya mafyongo huko nyuma hii ina nafuu ukijumla na hulka yake ya kutokuwa na haya basi tutarajie aibu zaidi.Kwa mara nyingine tena Wamarekani wanauona Ujinga,Uongo,Uchonganishi na Utapeli wa Jeshi letu la Polisi kwa kuwasingizia FIB kushiriki katika ujinga wao.

Hili Jeshi letu umefika wakati sasa lifumuliwe lote halafu liundwe na upya,Hakuna kitu kule jamani.
 
Back
Top Bottom