Fatma Karume: Wananchi wanajua kuna Mahakama, tatizo wakienda hawashughulikiwi. Mfumo wa Haki umefeli

Precious Diamond

JF-Expert Member
Jun 9, 2023
397
993
Mwanaharakati Fatma Karume, amekosoa mfumo anaotumia Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi, Paul Makonda katika kukusanya malalamiko ya watu na kueleza kuwa ni udhalilishaji.

"Sipendi kuona wananchi wanarundikana wako kwenye mistari wanamsubiri Makonda kulalamika, ni udhalilishaji. Lakini tujiulize kwa nini kuna udhalilishaji wa wananchi kiasi hiki, kwa sababu kuna kufeli kwa mfumo,"alieleza Fatma Karume.

"Wananchi wanajua kuna mahakama, kuna ofisi za mkuu wa mkoa, ofisi za wilaya, tatizo lao ni kwamba wakienda hawashughulikiwi, kuna kuanguka kwa mfumo. Tuache kufanya hii michezo, wapeni Watanzania mfumo wa haki unaofanya kazi, wanastahili hilo," alisisitiza zaidi.

Fatma aliongea haya katika mkutano na waandishi wa habari mapema leo Februari 03,2024, kuzungumzia mifumo ya haki,akiangazia suala la usalama wa mawakili.



The Chanzo
 
Mfumo wa Mahakama kulikoni? Moral transformation needed and change of attittude and new legal systems reform. Mahakama haiaminiki tena na wananchi,huo ndio ukweli.watafanya kazi gani sasa?. Taasisi iliyobaki inaaminika ni JWTZ at least.Tuchukue hatua
 
Mwanaharakati Fatma Karume, amekosoa mfumo anaotumia Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi, Paul Makonda katika kukusanya malalamiko ya watu na kueleza kuwa ni udhalilishaji.


The Chanzo
Wananchi wanajua kuna mahakama, kuna ofisi za mkuu wa mkoa, ofisi za wilaya, tatizo lao ni kwamba wakienda hawashughulikiwi, kuna kuanguka kwa mfumo. Tuache kufanya hii michezo, wapeni Watanzania mfumo wa haki unaofanya kazi, wanastahili hilo," alisisitiza zaidi.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom