Fathers'day -kina baba wanaowakataa watoto wao kisa nini?

Tausi Mzalendo

JF-Expert Member
May 23, 2010
1,471
722
Kwanza nawapongeza wababa wote kwa mchango wao mkubwa katika kuleta watoto duniani, kuwapenda wake zao au kuwajali mama wa watoto wao na watoto na pia kubeba majukumu yao.HONGERENI SANA KWA SIKU YA LEO.

Hata hivyo nina maswali machache kwa wale wababa wote waliowahi au wenye mpango wa kuwakataa watoto wao:
1.Je wangekataliwa na baba zao wangejisikiaje?

2. Nini kinamfanya Mwanamme amkatae mtoto wake wakati anajua kabisa aliwahi "kupanda "mbegu '? Dhamira haiwasuti?

3.Mwanamke anapokataliwa mwanaye na baba mhusika anajisikiaje?
4. Mtoto aliyekataliwa na babaye anapokuja kutambua anajisikiaje?




Michango yenu tafadhali
 
Mmh.. haya maswali magumu lakini yanagusa sehemu sehemu; kwenye swali la pili nadhani (naweka msisitizo kwenye kudhani) wapo wanaume ambao wanajua kabisa wapenzi wao hawakuwa waaminifu so kumkataa mtoto ni ishara ya kujihami kuwa nisije kushakiziwa mtoto asiye wangu - hasa wanapoangalia shows kama za Maury au Jerry Springer..!!
 
@ MMKJJ,
Naheshimu mawazo na mchango wako.Ukiacha huko kujihami kwa kudhania wakati kuna namna nyingi za kujua kama mtoto ni wako ama la, je wanaume wanapomwadhibu mama hawaoni adhabu kubwa anaipata mtoto ambaye hakuomba mmsababishe kuja duniani/

. Kwamba mama hakuwa mwaminifu, sidhani kunakuja kama kishtukizo.Mwanaume unapojamiiana na mwanamke bila kinga unategemea nini?
 
Namba moja siwezi kuwajibia ila mengine naweza kwasababu nimeona kwa mtu wangu wa katibu sana!!

2. Kukwepa/kukataa na kuogopa majukumu.Kama ambavyo kuna wadada hua wanatoa mimba na kutupa vichanga kisa eti hawako tayari kulea au hawana uwezo ndivyo ilivyo kwa wanaume.Inakua rahisi kwao kusema sio wangu na hata kama ni wangu simtaki kwasababu kwa wakati huo haitamcost kitu iwapo mwanamke atasema tu “sawa bwana“.

3. Maumivu...unyonge...mtu anahisi kuzalilika maana mara nyingi kukataliwa kwa mtoto hua inaendana na dhana ya kwamba mama hakua mtulivu...sio mjanja...hana akili na mengineyo.Hivyo maumivu yanakuwepo bila kusahau aibu mbele ya jamii.Mwanaume akimkataa mtoto kwa baadhi ya watu mama/mwanamke ndo hua anaonekana wa ajabu na sio anaekataa mwanae.

4.Anajisikia vibaya...anamchukia baba mzazi na kumwona hana maana.Nnaemjua mimi baba yake alianza kujisogeza akiwa na miaka 15 mtoto akawa anaenda kumsalimia bibi yake ila hakujali sana kuhusu baba.Ila alivyofikisha miaka 18 baba yake alikua anauliza kwanini haendi kumsalimia mtoto akamuuliza ili iweje...akamjibu siunakuja tu kumsalimia baba yako?!Mtoto akamwambia baba yangu ni yule anaejua mpaka leo nimekula na kuvaa nini pia ninesoma wapi.Miaka 20 baba akampigia mama kumwuliza mbona humruhusu mtoto kuja kwangu mama akamwambia hayo sio maamuzi yangu bali ni yake mwenyewe...ongea nae huyu hapa.Mtoto akamwambia baba yake sitaki mahusiano na wewe nilishakwambia na ukiendelea kunifuatilia ntakuua.Hawezi kufanya kitu kama hicho ila hayo maneno yanaonyesha ni kwa kiasi gani aliumia na kitendo alichofanya baba yake.Ila anampenda sana mama yake ...hilo linanipa furaha!
 
2. Kukwepa/kukataa na kuogopa majukumu.Kama ambavyo kuna wadada hua wanatoa mimba na kutupa vichanga kisa eti hawako tayari kulea au hawana uwezo ndivyo ilivyo kwa wanaume.Inakua rahisi kwao kusema sio wangu na hata kama ni wangu simtaki kwasababu kwa wakati huo haitamcost kitu iwapo mwanamke atasema tu "sawa bwana".
!

Lizzy,
Hapo nimependa maana lawama za wanawake kutupa watoto zipo sana na ni sawa walaumiwe.Mara nyingi "wanaume wanapotupa watoto" hawalaumiwi.Umefika wakati nao waangaliwe vingine!
 
Tausi Mzalendo;
Naheshimu mawazo na mchango wako.Ukiacha huko kujihami kwa kudhania wakati kuna namna nyingi za kujua kama mtoto ni wako ama la, je wanaume wanapomwadhibu mama hawaoni adhabu kubwa anaipata mtoto ambaye hakuomba mmsababishe kuja duniani/

Kwamba mama hakuwa mwaminifu, sidhani kunakuja kama kishtukizo.Mwanaume unapojamiiana na mwanamke bila kinga unategemea nini?

Maswala ya DNA kwenye ulimwengu wa tata kwani yameanza lini Tausi? Tofauti na DNA kuna njia ipi unayoweza kuthibitisha kama mtoto ni wako? Ni wakina mama wangapi wameolewa lakini wamebambika waume zao watoto wa wanaume wengine na wahusika hawajui?. Si wote wanaweza kumdu gharama za kwenda kupima DNA hasa huku bongo hivyo wahusika (wanaume wanakataa watoto) wakijuwa kuwa hawakuwa peke yao kimapenzi na mdada ndiyo maana wanakuwa wagumu kukubali mimba---mtoto kama watakuwa hawana uwakika wa kutosha. Hata kwenye hizo shows alizozitaja Mzee Mwanakijiji, sababu kubwa ya wababa kukataa watoto wao kama hawajapima DNA ni wadada kuwa na mahusiano na mtu zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja. Wakipima DNA na majibu yakasema watoto ni wakwao wote huwa wanakubali majukumu ya kulea watoto wao.


Kwa hiyo, issue siyo kutotumia kinga bali mtoto ni wa nani? Ndo tatizo kubwa kwa mwanaume. Kwa wale wanaojitowa akili na watoto ni wao na DNA imethibitisha kwakweli hapo sijui sababu zaidi ya kusema ''si wanaume wote are good fathers''.
 
Tausi Mzalendo;
Naheshimu mawazo na mchango wako.Ukiacha huko kujihami kwa kudhania wakati kuna namna nyingi za kujua kama mtoto ni wako ama la, je wanaume wanapomwadhibu mama hawaoni adhabu kubwa anaipata mtoto ambaye hakuomba mmsababishe kuja duniani/

Kwamba mama hakuwa mwaminifu, sidhani kunakuja kama kishtukizo.Mwanaume unapojamiiana na mwanamke bila kinga unategemea nini?

Maswala ya DNA kwenye ulimwengu wa tata kwani yameanza lini Tausi? Tofauti na DNA kuna njia ipi unayoweza kuthibitisha kama mtoto ni wako? Ni wakina mama wangapi wameolewa lakini wamebambika waume zao watoto wa wanaume wengine na wahusika hawajui?. Si wote wanaweza kumdu gharama za kwenda kupima DNA hasa huku bongo hivyo wahusika (wanaume wanakataa watoto) wakijuwa kuwa hawakuwa peke yao kimapenzi na mdada ndiyo maana wanakuwa wagumu kukubali mimba---mtoto kama watakuwa hawana uwakika wa kutosha. Hata kwenye hizo shows alizozitaja Mzee Mwanakijiji, sababu kubwa ya wababa kukataa watoto wao kama hawajapima DNA ni wadada kuwa na mahusiano na mtu zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja. Wakipima DNA na majibu yakasema watoto ni wakwao wote huwa wanakubali majukumu ya kulea watoto wao.


Kwa hiyo, issue siyo kutotumia kinga bali mtoto ni wa nani? Ndo tatizo kubwa kwa mwanaume. Kwa wale wanaojitowa akili na watoto ni wao na DNA imethibitisha kwakweli hapo sijui sababu zaidi ya kusema ''si wanaume wote are good fathers''.

Kweli kabisa
 
Lakini wengine labda wanamchukia mama mtoto na siyo mtoto..!!! so inakuwa ni sababu ya kuhalalisha tu chuki iliyoko kwa mama mtu.
 
Back
Top Bottom