Lupweko
JF-Expert Member
- Mar 26, 2009
- 20,690
- 20,445
Nilimsikia kwa makini dereva wa sheikh Fareed wa UAMSHO akielezea jinsi walivyoachana na sheikh Faeed. Nimemsikia Fareed mwenyewe akieleza jinsi alivyoachana na dereva wake. Wote wanasema dereva alitumwa na Fareed akanunue umeme, hapo hawajatofautiana.
Tofauti inakuja pale ambapo dereva amesema alimuacha Fareed anaenda kwenye gari (la waliomteka) wakati Fareed anasema gari (la waliomteka) lilikuja wakati dereva ameenda kununua umeme.
Kwa lugha nyingine, dereva anasema aliliacha gari la watekaji likiwa limeshafika na Fareed alilifuata mwenyewe, lakini Fareed amesema wakati gari (la waliomteka) linafika, dereva hakuwepo!
Wachambuzi wa mambo hebu angalieni hapo, inavyoonekana huyu sheikh hakuipanga vizuri hii movie na dili limeshabumbuluka!
Tofauti inakuja pale ambapo dereva amesema alimuacha Fareed anaenda kwenye gari (la waliomteka) wakati Fareed anasema gari (la waliomteka) lilikuja wakati dereva ameenda kununua umeme.
Kwa lugha nyingine, dereva anasema aliliacha gari la watekaji likiwa limeshafika na Fareed alilifuata mwenyewe, lakini Fareed amesema wakati gari (la waliomteka) linafika, dereva hakuwepo!
Wachambuzi wa mambo hebu angalieni hapo, inavyoonekana huyu sheikh hakuipanga vizuri hii movie na dili limeshabumbuluka!