FAO LA KUJITOA: Tundu Antipas Lissu Kupigania Wafanyakazi

Hivi miez mingapi imepita tangu ateuliwe na imebaki mingapi, nasikia tu atafungua kesi na kesi zenyewe hazifunguliwi

Naona muda wake utapita bila kufanya chochote cha maana
 
Kwakweli nitamshangaa Mtanzania atakayepinga hili, ukienda kwenye hizi Ofisi za Mifuko ya Jamii utawaonea huruma wanaodai mafao yao. Mlalahoi kafanya kazi anadai milioni 1 tu lakini anazungushwa hakuna maneno. PPF wako wazi kusema njoo ukifikisha miaka 55, NSSF wao wanakupiga kalenda kama ya miezi 4 hivi, ukienda unapigwa tena miezi 4.
 
Mkuu, unatakiwa uwe serious kwenye mambo ya maana. Halafu unajiita doctor? Pambafu thana!

ona akili zako, una tukana nini? endeleza utamaduni wa kuhoji, usiamini kila unalo ambiwa, kasema anapigania watu kwa nija zipi, mimi ni dr kama huamini endelea kutukana.
 
Kwakweli nitamshangaa Mtanzania atakayepinga hili, ukienda kwenye hizi Ofisi za Mifuko ya Jamii utawaonea huruma wanaodai mafao yao. Mlalahoi kafanya kazi anadai milioni 1 tu lakini anazungushwa hakuna maneno. PPF wako wazi kusema njoo ukifikisha miaka 55, NSSF wao wanakupiga kalenda kama ya miezi 4 hivi, ukienda unapigwa tena miezi 4.
NSSF ni matapeli haswa.
 
Mungu ambariki mtani wangu,maana nilikuwa nmeshajiwekea malengo baada ya mwaka Mungu akipendezwa nngeachana na hii kazi ya mhindi nihangaike na mambo yangu , lkn hawa pumbafu wanataka tusichukue hela zetu, kazi tufanye sisi matumizi ya pesa zetu watupangie
 
Mungu ambariki mtani wangu,maana nilikuwa nmeshajiwekea malengo baada ya mwaka Mungu akipendezwa nngeachana na hii kazi ya mhindi nihangaike na mambo yangu , lkn hawa pumbafu wanataka tusichukue hela zetu, kazi tufanye sisi matumizi ya pesa zetu watupangie

Nimesoma kwa uchungu sana hii meseji.
 
Tundu Antipas Lissu, Kuwapigania Wafanyakazi--FAO LA KUJITOA.

Kama kuna watetezi wa wafanyakazi katika nchi hii, basi ni pamoja na Tundu Antipas Lissu. Kwa kutumia taaluma yake, kwa moyo wake wote akishirikiana na Chama cha Wanasheria nchini (TLS) ambacho yeye ndiye Rais (ama kiongozi wa juu), Tundu Lissu ameahidi kushughulikia na kupigania wafanyakazi ili waweze kupata haki yao ya fao la kujitoa mahakamani; (na kwa sasa wapo kwenye mchakato).

Itakumbukwa kwamba, tangu mwezi May mwaka 2016, mifuko ya jamii nchini (PPF/NSSF na mingineyo) ilisitisha utoaji wa fao la kujitoa kwa madai ya kutekeleza sheria ya mifuko hiyo kwamba ili mfanyakazi achukue pesa yake, basi lazima awe amefikisha umri wa miaka 55 au 60.

Yaani wewe kijana mwenzangu na umri wako huo wa miaka 25 au 30 inapotokea leo umefukuzwa kazi na mwajiri, basi kuchukua pesa zako zilizoko kule PPF/NSSF ambazo ni jasho lako, eti unatakiwa kuishi miaka 25 au 30.

Kumbuka hapo, pesa haiongezeki thamani, kumbuka, kuchukua pesa yako haupati riba, kumbuka kodi unalipa ila bado unazuiwa kuchukua haki yako. Toa neno moja kwa Tundu Lissu, wakati huo huo, wafanyakazi wote tumuombee kwa Mungu Tundu Antipas Lissu--Jembe. Kwa maana yeye ndiye anaonekana kuwa mtetezi wetu wafanyakazi.

*Zingatia: Kama Mwanasheria, na Rais wa Chama Cha Wanasheria (TLS), anayo MAMLAKA ya kuishitaki serikali kwa jambo lolote pale anapoona mambo hayako sawa. Maana wapo watakaohoji....'yeye kama nani'? Pili...wapo watakaohoji, kwa nini TUCTA wako kimya? Jibu ni kwamba, TUCTA si wenzetu wale, hawako kupigania maslahi ya wafanyakazi, in a nutshell, they (TUCTA) are opportunists.

Solidarity Forever, For The Union Makes us Strong.

Argument ya serikali pamoja na SSRA kuhusu fao la kujitoa ni nzuri, kwamba nia ya mifuko hii ni kuwafanya wafanyakazi wawe pensionable ili waweze kuishi decent life baada ya muda wao wa utumishi kumalizika.

Waingereza wana msemo usemao " NO RULE WITHOUT EXCEPTION" or EXCEPTION CONFIRMS THE RULE" - Kuna makundi maalumu ambao ni wanachama wa mifuko hii ambao kwa nature ya ajira zao ni vigumu sana ku - attain umri huo ambao ni wa kisheria kuwa pensionable: SSRA inaweza ikabadili umri wa kuwa pensionable kwa sekta hizo ambazo zimethibitika zina ugumu wa kukithi matakwa ya sheria hii. Au, wakaruhusu makundi haya maalumu kuendelea na utaratibu uliokuwepo tangu awali wa fao la kujitoa.
 
Jàman mbona watu wanachukuwa mafao yao mifiko yte inatoa mafao tena kwa fasta sana ushahidi upo kabisa

Mkuu kaa kimya kabisa kama wewe ulibahatika kupata labda ulipitia mlango wa nyuma. Watu wanazungushwa mwaka na zaidi na hamna hata dalili.

Unaambiwa ukae miezi sita baada ya mkataba wako kuisha wa kazi. Baada ya kupeleka form unaambiwa usubiri wafanye uchunguzi watakupigia simu hiyo inachukua tena miezi mingine sita na simu haipigwi. Ukienda kuuliza unaambiwa usubiri miaka 55 yaani ni usumbufu juu ya usumbufu. Alafu kila mtu ana majibu yake.
Nipo na Lissu katika hili tena mstari wa mbele
 
Back
Top Bottom