Familia ya Q Chillah walia na mkataba wa maisha

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,305
24,198
Feb 7, 2017

Familia ya Q Chillah walia na mkataba wa maisha

Familia ya msanii Q Chillah imejitokeza na kuhoji mkataba wa Q Chillah na QS Mhonda J. Entertainment ambao unamfunga huyo msanii ''kisheria'' maisha yake yote.

Familia inajiuliza mtoto wao Q Chillah aliposaini mkataba wa maisha wa kazi zake za muziki alikuwa amelewa au vipi kwani hawajawahi kuona mkataba wa kazi za kisaini popote pale ulimwenguni wenye kipengele cha kumfunga msanii ndani ya mkataba maisha yake yote.

Familia ya Q Chillar imetoa ombi kwa QS Mhonda J Entertainment wakae pamoja kupitia mkataba huo upya badala ya kupelekana mbele ya vyombo vya kisheria kupata ufafanuzi wa uhalali wa mkataba wa ''maisha'' baina ya msanii huyo na kampuni ya QS.

Hali hii imewakumba wasanii wengi kutokuwa makini wakati wa kusaini mikataba na hatimaye kutofaidika na jasho la kazi yao. Tusikilize kilio cha wanafamilia ktk video clip hapa chini:

Source: EastAfrica Television
 
Kabla ya kusaini kama huelewi baadhi ya vifungu angeomba ushauri kuliko kusaini kitu usicho kijua...au ndo alikuwa asharamba bwimbwi na kusaini akiwa na arosto?..
 
Feb 7, 2017

Familia ya Q Chillah walia na mkataba wa maisha

Familia ya msanii Q Chillah imejitokeza na kuhoji mkataba wa Q Chillah na QS Mhonda J. Entertainment ambao unamfunga huyo msanii ''kisheria'' maisha yake yote.

Familia inajiuliza mtoto wao Q Chillah aliposaini mkataba wa maisha wa kazi zake za muziki alikuwa amelewa au vipi kwani hawajawahi kuona mkataba wa kazi za kisaini popote pale ulimwenguni wenye kipengele cha kumfunga msanii ndani ya mkataba maisha yake yote.

Familia ya Q Chillar imetoa ombi kwa QS Mhonda J Entertainment wakae pamoja kupitia mkataba huo upya badala ya kupelekana mbele ya vyombo vya kisheria kupata ufafanuzi wa uhalali wa mkataba wa ''maisha'' baina ya msanii huyo na kampuni ya QS.

Hali hii imewakumba wasanii wengi kutokuwa makini wakati wa kusaini mikataba na hatimaye kutofaidika na jasho la kazi yao. Tusikilize kilio cha wanafamilia ktk video clip hapa chini:

Source: EastAfrica Television

Je, huo mkataba ulisainiwa mbele ya mwanasheria? unajua wasanii wetu wana njaa sana Nchi haijui tu. Media inapumbaza umma kuwa jamii ya wasanii inaishi maisha ya kifahari lakini vyumbani mwao wanalia. Yaani miaka yote hiyo G-chillah bado hana gari? bado hajajenga?? Ukweli ni kwamba, mziki barani Afrika una mafanikio kwa alieingia kwenye mziki huku tayari ana hela zake, ni wachache wanaofanikiwa from scratch mfano Diamond.
 
Je, huo mkataba ulisainiwa mbele ya mwanasheria? unajua wasanii wetu wana njaa sana Nchi haijui tu. Media inapumbaza umma kuwa jamii ya wasanii inaishi maisha ya kifahari lakini vyumbani mwao wanalia. Yaani miaka yote hiyo G-chillah bado hana gari? bado hajajenga?? Ukweli ni kwamba, mziki barani Afrika una mafanikio kwa alieingia kwenye mziki huku tayari ana hela zake, ni wachache wanaofanikiwa from scratch mfano Diamond.
Si kweli kuwa muziki kwa Africa unamfaidisha mwanamuziki Mwenye hela ... Nenda kasome historia ya wizkid alivyokulia kwenye maisha magumu kwenye mitaa ya ojualegba, Lagos Nigeria.
 
Ana uwezo wa kuupinga mahakamani kama walimrubun kuusain, au kama hakuuelewa...kaz ni kwake unatenguliwa tu
 
Si kweli kuwa muziki kwa Africa unamfaidisha mwanamuziki Mwenye hela ... Nenda kasome historia ya wizkid alivyokulia kwenye maisha magumu kwenye mitaa ya ojualegba, Lagos Nigeria.
Hujanielewa au umekurupuka...nimesema kuwa ni wachache wanaotokea "from scratch", mojawapo Diamond na huyo Wizkid....asilimia 90 ni walioingia kwenye muziki sio kwasababu ya njaa....MWENYE NACHO HUONGEZEWA.
 
Yani wanamuziki wa Tanzania ni lazima mwisho wa safari wagombane na management.
Uwa wakisaini mikataba utawasikia kwenye media wanasifia management kuwa imewapa kila kitu na mbwembwe nyingi mara kanunuliwa gari sijui nyumba kunbe mbwembwe.
qchillah nakumbuka alipojiunga na QS alifanyiwa interview akawa anasifia kweli yani sana.
Sema Qchillah ana ji-over estimate anahisi kwa uwezo wake ana deserve awe na mapato makubwa coz anajicompare na madogo walioshika soko.
 
Hujanielewa au umekurupuka...nimesema kuwa ni wachache wanaotokea "from scratch", mojawapo Diamond na huyo Wizkid....asilimia 90 ni walioingia kwenye muziki sio kwasababu ya njaa....MWENYE NACHO HUONGEZEWA.
Muongeze Casper Vyovest hapo
 
EEE ndio mkataba wa maisha huo waache kulia lia, je Q angefariki muda mfupi baada ya ku sign ingekuwaje kwa huo upande wa pili? wangeenda kuomba warudishiwe sehemu ya pesa wangekubaliwa na family ya Q? pole yao.
 
Huyo wakat anasain
Huo mkataba alikua ameshapga vyombo
Vyake maana mtu alie
Timamu hawez kusain mkataba wa kisenge hvo
 
Back
Top Bottom