Familia ya Nyerere mnaaibisha taifa

Status
Not open for further replies.
Mtoa uzi uja sema nikiasi gani ulitozwa!!!sasa nimeamini Kambarage alikuwa mzalendo wa kweri hakujilimbikizia MALI,pumzika kwa amani Kambarage
 
duh!hiv cku dhaifu anasepa wa2 watakubal kulipia kuzuru kaburi lake?
 
mamajack,

Haya uliyoandika hapa sio kweli.

Mjane wa Mwalimu analipwa 40% ya mshahara wa Rais wa sasa kama pensheni kila mwezi hadi atakapofariki. Wanae Mwalimu ni watu wazima na walianza kujitegemea siku nyingi kabla ya Mwalimu kufariki.

Kama wanatoza kiingilio pale ni masuala mengine kabisa. Mama Maria Nyerere anatunzwa vizuri tu sio na serikali hii bali hata Museveni wa Uganda.
MUSEVEN WA UGANDA!!!!KWA LIPI M7 amtunze!
 
Baba wa Taifa amezikwa kwenye shamba lake. Tatizo ni nini? Tusishangae kwa hayo yanayotokea labda angezikwa pale Makumbusho!!!! Uongozi wa CCM haukuwa na ujasiri wa kuzungumzia juu ya watu mashuhuri kisiasa nchini watakapoitwa na Mungu watahifadhiwa wapi. Hili lina ugumu wake lakini pia ni ukweli kila mtu atakufa. Kifo cha ghafla cha Edward Sokoine ilikuwa fundisho tosha kuwa watu kama hawa ambao wana nafasi ya kipekee katika taifa wapumzishwe wapi siku wakiondoka duniani.
 
Hivi karibuni nilitembelea Butiama kuzuru makazi, kaburi na Makumbusho ya Mwl. Nyerere.

Kitu kilichonisikitisha na kunishangaza ni kwamba mtu haruhusiwi kuona kaburi la Baba wa Taifa hadi alipie huduma hiyo! Nilipouliza utaratibu huu upo tangu zamani, muhudumu wa pale getini alinijibu kwamba FAMILIA YA MWL NYERERE IMEAMUA KUANZISHA UTARATIBU HUU ILI KUPATA FEDHA ZA KUTUNZA FAMILIA!

Baadaye nilitembelea Makumbusho nikauliza suala hili nikajibiwa na maofisa wa Makumbusho kwamba hapo awali Makumbusho ilikuwa na dhamana ya kuwatembeza wageni wote kwenye makazi, kaburi isipo kuwa baadhi ya maeneo. Hali hiyo ilibadilika baada ya baadhi ya wanafamiilia kuanzisha utaratibu huo ambao kwa kweli wageni wengi, na watanzania kwa ujumla wanaushangaa na ni aibu kwa taifa.

Maoni yangu ni kwamba serikali inapaswa kuchukua dhamana ya kutunza eneo hilo hii ikiwa ni pamoja na usalama wake.

Kadhalika familia ama kikundi cha watu kamwe kisipewe ruhusa ya kufanya biashara ya aina yoyote katika eneo hilo.

Mkuu,

Hili jambo ulilotumwa kuandika hapa ni zito na nafikiri wewe unatambua. Itakuwa ni jambo la busara kutuwekea ushahidi wa haya yote uliyoyasema kwani utakuwa na stakabadhi ya malipo ya hiyo tour yako kwenye kaburi.

Pia hao watu wa kwenye geti ambao walikuzuia kuingia hadi ulipe itabidi uwatambue endapo utahitajika kufanya hivyo.

Si wewe pekee ambae umefika hapo kiasi cha kutoona ulinzi wa askari kwani makumbusho hayo ni kwa raia wa Tanzania na kigeni pia ambao hupenda kufika mahali hapo.

Vinginevyo naona ulichoandika hapa ni nje kabisa ya mstari na pia uangalie maana naona unatoa kashfa kwa familia ya Mwalimu.
 
Mkuu,

Hili jambo ulilotumwa kuandika hapa ni zito na nafikiri wewe unatambua. Itakuwa ni jambo la busara kutuwekea ushahidi wa haya yote uliyoyasema kwani utakuwa na stakabadhi ya malipo ya hiyo tour yako kwenye kaburi.

Pia hao watu wa kwenye geti ambao walikuzuia kuingia hadi ulipe itabidi uwatambue endapo utahitajika kufanya hivyo.

Si wewe pekee ambae umefika hapo kiasi cha kutoona ulinzi wa askari kwani makumbusho hayo ni kwa raia wa Tanzania na kigeni pia ambao hupenda kufika mahali hapo.

Vinginevyo naona ulichoandika hapa ni nje kabisa ya mstari na pia uangalie maana naona unatoa kashfa kwa familia ya Mwalimu.
Wewe unamtisha mtoa mada iLi pindi aatakapoona uoza mwengine asiongee, hayo si mageni nchi hii unashanga nini, kila mahala nchi hii Imeoza
 
mamajack,

Haya uliyoandika hapa sio kweli.

Mjane wa Mwalimu analipwa 40% ya mshahara wa Rais wa sasa kama pensheni kila mwezi hadi atakapofariki. Wanae Mwalimu ni watu wazima na walianza kujitegemea siku nyingi kabla ya Mwalimu kufariki.

Kama wanatoza kiingilio pale ni masuala mengine kabisa. Mama Maria Nyerere anatunzwa vizuri tu sio na serikali hii bali hata Museveni wa Uganda.

hii inch ina pesa zinazotolewa hovyhovyo, For what?
 
Baba wa Taifa amezikwa kwenye shamba lake. Tatizo ni nini? Tusishangae kwa hayo yanayotokea labda angezikwa pale Makumbusho!!!! Uongozi wa CCM haukuwa na ujasiri wa kuzungumzia juu ya watu mashuhuri kisiasa nchini watakapoitwa na Mungu watahifadhiwa wapi. Hili lina ugumu wake lakini pia ni ukweli kila mtu atakufa. Kifo cha ghafla cha Edward Sokoine ilikuwa fundisho tosha kuwa watu kama hawa ambao wana nafasi ya kipekee katika taifa wapumzishwe wapi siku wakiondoka duniani.

Kumbukumbu zangu zinanikumbusha kuwa bunge letu limewahi kujadili muswada wa sheria za mazishi ya viongozi wa kitaifa. Sina uhakika kama muswada ulikidhi mahitaji yote ili iweze kuridhiwa kuwa sheria. Ebu bonyeza hapa: Parliament of Tanzania
 
Ukweli ni kuwa serikali imewapa vingi sana familia ya Nyerere kiasi cha kuwa familia ya Nyerere yenyewe haina cha kurudisha serikalini! hapo ndipo gogoro la kichinichini kati ya familia ya Nyerere na serikali linapoanzia!
Kuna aliyeshangazwa na Makongoro kukosa hata nauli ya kwenda Dodoma!hivi huyu mtu anataka hata usafiri wa Makongoro mwenyewe uhudumiwe na Serikali?! mwisho atakuja kutaka serikali imlipie mfanyakazi wa kukata nyasi za nyumbani kwake (kama hawajafikia hatua hii)?!...na wale mama zetu wanaouza vitumbua barabarani nao mbona hakuna wa kuyakimu maisha yao au hata kuwasemea? au si Watanzania wale?
Hili kaburi lifukuliwe na akazikwe kwao kule ambako wazazi wake wametokea labda huko familia yake inaweza kupatiwa hizo huduma wanazozitaka, lakini isiwe katika ardhi ya Tanzania.

another fieces
 
mlishaamua kumtangaza ni Mtakatifu wenu mtafanya kila mpendalo, Kuona kaburi tsh 500,000, kuligusa 1mil! teh teh teh dunia ina mambo
 
Nani ana uhakika kwamba hiyi familia haitunzwi tena?

Sidhani kama ni rahisi kiasi hicho kuiacha hiyo familia wanaweza kuwa wameweka hiyo fee kwa tamaa zao wenyewe.

Unahitaji kuwa kiongozi mwendawazimu kuitelekeza familia ya mwalimu

:spy: unapigia jibu mstari? kwani hujui kuwa ndivyo walivyo
 
Kitu ambacho hukielewi au hukueleweshwa ni kuwa eneo la Mwitongo kwa sasa liko chini ya TTB, na hii ni kutokana na gharama za uendeshaji wa makazi hayo kwani familia yenyewe hawawezi kuendesha makazi hayo kwa kuwa ni gharama kubwa sana!

Na aliyeachiwa/ rithishwa makazi hayo ni Madaraka, nadhani wa kulaumiwa ni Serikali ambayo huenda inasuasua kupeleka posho Mwitongo...

Zingatia tu kuwa familia ya Mwallimu wanaishi maisha ya kawaida tofauti na kina naniii!!
 
Mie hii taarifa imeongeza hasira zangu ZA MAKAO MAKUU YA WILAYA YA MUSOMA VIJIJINI eti kupelekwa Butiama.Hivi kweeeeelii kweli kweli mura wane kweli.Inamaana hawakupaona Mugango,Murangi,Bukima au sehemu yoyote ya Majita kuwa makao makuu hadi "Buti-hama" tuuu?? lol eti kusogeza huduma kwa wananchi,fyuuuuu
Majita,
Za masiku? Halafu Nyerere alipokuwa hai alikataa Butiama yasiwe makao makuu maana alisema hakuna ardhi ya kutosha kwa wakulima wa Kizanaki ambao watalazimika kuhama kupisha ujenzi wa makao.
 
Hivi karibuni nilitembelea Butiama kuzuru makazi, kaburi na Makumbusho ya Mwl. Nyerere.

Kitu kilichonisikitisha na kunishangaza ni kwamba mtu haruhusiwi kuona kaburi la Baba wa Taifa hadi alipie huduma hiyo! Nilipouliza utaratibu huu upo tangu zamani, muhudumu wa pale getini alinijibu kwamba FAMILIA YA MWL NYERERE IMEAMUA KUANZISHA UTARATIBU HUU ILI KUPATA FEDHA ZA KUTUNZA FAMILIA!

Baadaye nilitembelea Makumbusho nikauliza suala hili nikajibiwa na maofisa wa Makumbusho kwamba hapo awali Makumbusho ilikuwa na dhamana ya kuwatembeza wageni wote kwenye makazi, kaburi isipo kuwa baadhi ya maeneo. Hali hiyo ilibadilika baada ya baadhi ya wanafamiilia kuanzisha utaratibu huo ambao kwa kweli wageni wengi, na watanzania kwa ujumla wanaushangaa na ni aibu kwa taifa.

Maoni yangu ni kwamba serikali inapaswa kuchukua dhamana ya kutunza eneo hilo hii ikiwa ni pamoja na usalama wake.

Kadhalika familia ama kikundi cha watu kamwe kisipewe ruhusa ya kufanya biashara ya aina yoyote katika eneo hilo.

Kabla ya kuwalaumu ..familia ya mwalimu ambaye hakuwa fisadi ...ulizeni serekali yenu inatoa bei gani kuhudumia kaburi na makumbusho yake kwa ujumla???? na kama Mwalimu Mausoleum ni sehemu ya makumbusho ya butiama .....basi kuna malipo fulani hufanywa kwa kutembelea makumbusho hata hapa dar wanalipa .......mlipewa risiti??? kama hamkupewa kosa ndio hapo...
Pili tushukuru kwa sasa mama maria yuupo hai na baadhi ya gharama za ndogo ndogo anazitoa yeye...kama akiwa hayupo ni lazima Serekali iwe tayari kuwafidia watoto wa mwalimu ili wayaachie makazi yao ya msasani na butiama ili yawe URITHI wa Taifa....kwani lazima mjuwe kuwa wao wana haki ya kuwa pale ni kwa baba yao.......kama mnataka pahifadhiwe basi warithi wa mwalimu walipwe fidia ili majengo yote yawe makumbusho kama ile ya pale magomeni ......na wao wanaweza kujengewa makazi mengine dar na butiama in return..la sivyo msishangae siku moja kitukuu wa mwalimu miaka 50 ijayo akaamua kuwa ni kwa maslahi yao wamuuzie mtu yeyote makazi yao ya familia........ndo mbona nyie mnauza nyumba za urithi ,nani anawauliza?
 
Kwanza mimi naomba kuuliza swali moja kwanza nijibiwe?
Unakwenda kuangalia kaburi la Nyerere ili iweje? hebu jiulize kwanza ni lini mara ya mwisho ulitembelea makaburi ya wapendwa ndugu zako?

Anayeshangaa kulipia kaburi la Nyerere mimi nitamshangaa yeye, wewe kama umefunga safari mpaka Butiama ni kwamba unamuamudu Nyerere, basi ni lazima uingie Gharama kama wanazoingia mahujaji wanaokwenda makka na Israel na Italy.
 
Mkuu hapa hoja umeilewa au imekupita kidogo?

Makumbusho ya Nyerere inalipiwa hivi sasa ila ukitaka kuona kaburi unatakiwa ulipie kwa huduma hiyo ya kuona kaburi

Duniani kote makumbusho mengi ni ya kulipia ila hii ya kulipia kuona kaburi ndio naipta sasa.

Nenda kwa waasisi wa usoshalisti kama kina Ho Chi Min na V.I. Lenin, makaburi yao yapo kwenye public squares kuona bure.

Nenda Uturuki, makaburi ya waasisi wao yamejengewa na kuona ni bure, nenda Iraq na Iran hali ni vile vile. Nenda Uingereza na watu wao maarufu, makaburi ni sehemu ya makumbusho au bure

Heck, nenda Tumbuktu na makaburi ya maulamaa maarufu katika mji huo wa kihistoria ni bure.

Hata hapo Zanzibar kuona kaburi la Karume ni bure.

Mkuu hoja nimeielewa vizuri. Labda nikuulize tu kuna tatizo gani kaburi la Mwal. Nyerere kuwa sehemu ya Makumbusho? Sijui location ya kaburi hilo maana sijawahi kufika lakini ningekuwa mmoja wa Wanafamilia hakika ningebuni Makumbusho makubwa sana ya Mwalimu na kaburi la mwalimu lingekuwa sehemu yake.

Ningeyatangaza kwa nguvu zote ili kuvuta maelfu ya watu kutoka pande zote duniani kuja kuyaona. Nyerere is a philosopher wa karne ya 20, watu wengi wanamsoma maandiko yake. Si mtu mdogo hata kidogo. Kwa kuwa tu tumezoea kutake simple mambo yetu lakini hakika, familia ya mwalimu na hata Serikali imechelewa sana katika hilo, inamfifisha Mwalimu Nyerere (RIP)
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom