Familia ya Nyerere mnaaibisha taifa

Status
Not open for further replies.
Pigeni business nchi ishauzwa hii,hakuna cha bure.....magamba wameitelekeza family ss kabur lao ndo mnallitaka?
 
hivi karibuni nilitembelea butiama kuzuru makazi, kaburi na makumbusho ya mwl. Nyerere.

Kitu kilichonisikitisha na kunishangaza ni kwamba mtu haruhusiwi kuona kaburi la baba wa taifa hadi alipie huduma hiyo! Nilipouliza utaratibu huu upo tangu zamani, muhudumu wa pale getini alinijibu kwamba familia ya mwl nyerere imeamua kuanzisha utaratibu huu ili kupata fedha za kutunza familia!

Baadaye nilitembelea makumbusho nikauliza suala hili nikajibiwa na maofisa wa makumbusho kwamba hapo awali makumbusho ilikuwa na dhamana ya kuwatembeza wageni wote kwenye makazi, kaburi isipo kuwa baadhi ya maeneo. Hali hiyo ilibadilika baada ya baadhi ya wanafamiilia kuanzisha utaratibu huo ambao kwa kweli wageni wengi, na watanzania kwa ujumla wanaushangaa na ni aibu kwa taifa.

Maoni yangu ni kwamba serikali inapaswa kuchukua dhamana ya kutunza eneo hilo hii ikiwa ni pamoja na usalama wake.

Kadhalika familia ama kikundi cha watu kamwe kisipewe ruhusa ya kufanya biashara ya aina yoyote katika eneo hilo.


mkuuu laiti nyerere angesikia ananunuliwa akiwaa maiti wakati akiwa hai alisweka ndani watu kwa kuambiwa wanaweza kumnununua yeye na serikali yake nahisi hii dhambi maa maria aitomwacha kwa kweli unaambiwa mzee alikuwa amekaataa kabisa hata pension yake akipewa anaenda kupeleka kwenye misadda
baada ya kifo pengine mama maria alikuwa anaanza kufeel umuhimu wa matumizi ya mumewe kwa kweli kwa kuanza kupokea penssiona ya mzee na mpaaka leo wanawabadilishia thamani na mengineyo mama anaukataa kama presidaa anyway....wengi walifurahia kifo cha huyu mzee bila kumsahau rais wetu alichaguliwa na mzee usiniulize nani
 
Naona badala ya kuweka kiwango cha kuangalia kabuli wangeweka kisanduku watu kuchangia kwa hiari yao kama sehemu ya kutunza makumbusho bila shaka wangepata hela nyingi zaidi.
 
Magamba wamemtelekeza mjane wa mwasisi wao wewe unategemea itakuwaje, watoto wote waliwatema kwenye system mpaka juzi makongoro kaponea mikononi mwa wapinzani akapata africa mashariki,sasa unategemea mama nyerere afanyeje?

Auze vitumbua, banaogopa kukamwatwa na mgambo wa jiji, kila mtu anafaidi na kile anachoweza kutumia.

Kama huamini fatilia familia za wastaaf waliowahi kuwa na mchango wa kizalendo kwenye nchi hii uone walivyotelekezwa,na kwasababu makaburi ya waume zao hayatembelewi,hawana mbadala wa kupata pesa.

Safi sana familia ya Mwl. Aibu ni kwa serikali ya magamba.

mamajack,
Kukaa kimya ni bora kuliko kuropoka, hujui unachosema naona umeamua kujidhalilisha, familia ya Nyerere wanapewa huduma zote na serikali.
 
Last edited by a moderator:
mamajack,
Kukaa kimya ni bora kuliko kuropoka, hujui unachosema naona umeamua kujidhalilisha, familia ya Nyerere wanapewa huduma zote na serikali.
mimi nijizalilishe au wewe unazalilisha kupingana na ukweli?hivi unadhanu watanzania wanaishi kwa nadhali ?hizo huduma feki uamtangazia nani?tunajua kila kitu na ndiyo maanatunasema laana ya mwl itawamaliza mAGAMBA!
 
Na kweli viongozi wendawazimu wapo wengi tu wa kutosha!
Nani ana uhakika kwamba hiyi familia haitunzwi tena?

Sidhani kama ni rahisi kiasi hicho kuiacha hiyo familia wanaweza kuwa wameweka hiyo fee kwa tamaa zao wenyewe.

Unahitaji kuwa kiongozi mwendawazimu kuitelekeza familia ya mwalimu
 
Inawezekana. Hata mtoa hoja hana risiti aliopewa kwa malipo hayo. Mbaya zaidi aliongea na mlinzi getini. Moja kati ya mambo mema aliofanya Mkapa na Sumaye ni kuhakikisha pensheni ipo kwa wastaafu wa ngazi kubwa za kitaifa na wajane wa viongozi wakuu wa kitaifa. Walikosea tu kutowaondoa wanaotuibia wakiwa madarakani kama akina Mkapa, Lowasa na Sumaye.

Ilitakiwa afanye ka research kadogo kabla ya kuanza kurusha shutuma kwa familia ya Nyerere na serikali.
 
Nashangaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa hii mpaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Zitakuwa njaa tu za hao watu wa Butiama waliopewa dhamana ya kutunza.


Mie hii taarifa imeongeza hasira zangu ZA MAKAO MAKUU YA WILAYA YA MUSOMA VIJIJINI eti kupelekwa Butiama.Hivi kweeeeelii kweli kweli mura wane kweli.Inamaana hawakupaona Mugango,Murangi,Bukima au sehemu yoyote ya Majita kuwa makao makuu hadi "Buti-hama" tuuu?? lol eti kusogeza huduma kwa wananchi,fyuuuuu
 
Wajasiriamali wa ukweli! I will pay them a visit soon and PAY ENTRANCE FEE plus tip to the family... What a pitty country!
 
Hivi karibuni nilitembelea Butiama kuzuru makazi, kaburi na Makumbusho ya Mwl. Nyerere.

Kitu kilichonisikitisha na kunishangaza ni kwamba mtu haruhusiwi kuona kaburi la Baba wa Taifa hadi alipie huduma hiyo! Nilipouliza utaratibu huu upo tangu zamani, muhudumu wa pale getini alinijibu kwamba FAMILIA YA MWL NYERERE IMEAMUA KUANZISHA UTARATIBU HUU ILI KUPATA FEDHA ZA KUTUNZA FAMILIA!

Baadaye nilitembelea Makumbusho nikauliza suala hili nikajibiwa na maofisa wa Makumbusho kwamba hapo awali Makumbusho ilikuwa na dhamana ya kuwatembeza wageni wote kwenye makazi, kaburi isipo kuwa baadhi ya maeneo. Hali hiyo ilibadilika baada ya baadhi ya wanafamiilia kuanzisha utaratibu huo ambao kwa kweli wageni wengi, na watanzania kwa ujumla wanaushangaa na ni aibu kwa taifa.

Maoni yangu ni kwamba serikali inapaswa kuchukua dhamana ya kutunza eneo hilo hii ikiwa ni pamoja na usalama wake.

Kadhalika familia ama kikundi cha watu kamwe kisipewe ruhusa ya kufanya biashara ya aina yoyote katika eneo hilo.

Nadhani ungeonana na msemaji mkuu wa familia - nchi hii siku hizi u TP ni mwingi. Hata hivyo "familia" isipotoza kuna mtu mwingine atatoza tu!!!
 
Hivi karibuni nilitembelea Butiama kuzuru makazi, kaburi na Makumbusho ya Mwl. Nyerere.

Kitu kilichonisikitisha na kunishangaza ni kwamba mtu haruhusiwi kuona kaburi la Baba wa Taifa hadi alipie huduma hiyo! Nilipouliza utaratibu huu upo tangu zamani, muhudumu wa pale getini alinijibu kwamba FAMILIA YA MWL NYERERE IMEAMUA KUANZISHA UTARATIBU HUU ILI KUPATA FEDHA ZA KUTUNZA FAMILIA!

Baadaye nilitembelea Makumbusho nikauliza suala hili nikajibiwa na maofisa wa Makumbusho kwamba hapo awali Makumbusho ilikuwa na dhamana ya kuwatembeza wageni wote kwenye makazi, kaburi isipo kuwa baadhi ya maeneo. Hali hiyo ilibadilika baada ya baadhi ya wanafamiilia kuanzisha utaratibu huo ambao kwa kweli wageni wengi, na watanzania kwa ujumla wanaushangaa na ni aibu kwa taifa.

Maoni yangu ni kwamba serikali inapaswa kuchukua dhamana ya kutunza eneo hilo hii ikiwa ni pamoja na usalama wake.

Kadhalika familia ama kikundi cha watu kamwe kisipewe ruhusa ya kufanya biashara ya aina yoyote katika eneo hilo.

wanatoza kiasi gani cha fedha mkuuu?
 
Serikali na mamlaka zake wako usingizini, unategemea familia ifanyeje? Hakuna haki bila wajibu. Tafakari, chukua hatua.
Ukweli ni kuwa serikali imewapa vingi sana familia ya Nyerere kiasi cha kuwa familia ya Nyerere yenyewe haina cha kurudisha serikalini! hapo ndipo gogoro la kichinichini kati ya familia ya Nyerere na serikali linapoanzia!
Kuna aliyeshangazwa na Makongoro kukosa hata nauli ya kwenda Dodoma!hivi huyu mtu anataka hata usafiri wa Makongoro mwenyewe uhudumiwe na Serikali?! mwisho atakuja kutaka serikali imlipie mfanyakazi wa kukata nyasi za nyumbani kwake (kama hawajafikia hatua hii)?!...na wale mama zetu wanaouza vitumbua barabarani nao mbona hakuna wa kuyakimu maisha yao au hata kuwasemea? au si Watanzania wale?
Hili kaburi lifukuliwe na akazikwe kwao kule ambako wazazi wake wametokea labda huko familia yake inaweza kupatiwa hizo huduma wanazozitaka, lakini isiwe katika ardhi ya Tanzania.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom