Familia kwenda bungeni yapo yaliyoficha nyuma ya hulka hiyo inayochukiwa na wengi

Familia kwenda bungeni yapo yaliyoficha nyuma ya hulka hiyo inayochukiwa na wengi

Steven Joel Ntamusano

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2023
Posts
8,787
Reaction score
5,536
Abedi Pele enzi zake akaichezea timu ya Taifa ya Ghana aliwika vilivyo. Alicheza 9 na 10 naukumbuka wepesi wake na namna alivyowasumbua mabeki. Jina lake la kuzaliwa ni Abedi Ayew lakini mashabiki wakaona wamfananishe na Mfalme Pele mwenyewe.

Baada ya kustaafu soka watoto wake wawili wakaamua kufuata nyayo za Baba yao. Jordan na Andre wamecheza pale Uingereza kwa misimu kadhaa pia ni sehemu ya kikosi cha Ghana kinachoshiriki afcon mara kwa mara, wameirithi kaka aliyoifanya Baba yao na kila anayewaona anawapigia makofi.

Alikuwepo Profesa mmoja mwenyeji wa Kilimanjaro, aliaga dunia mwaka 2021 inasemekana alisumbuliwa na COVID19, alikuwa ni mtaalam wa magonjwa ya watoto, aliishi Mbezi Beach. Watoto wa profesa yule pia ni wataalam wa afya wameirithi kazi ya Baba yao na wanaziendeleza shughuli alizofanya mzazi wao kwa umahiri.

Sioni dhambi yoyote kwa mtu kuirithi fani ya Baba au Mama yake. Mara nyingi wanakua huku wakiwatazama wazazi wao kwa ukaribu. Wanajikuta wakitamani siku moja kupita njia zile zile za wazazi na ni vigumu wazazi kuwavunja moyo.

Sishangai kuiona Familia ya mstaafu Kikwete ikizama kwenye siasa. Ridhiwani amekua akimuona Baba yake majukwaani akishughulika na siasa za moja kwa moja. Mama Salma pia anao wito wa kisiasa wa moja kwa moja hivyo ni vigumu kwa mtoto wao kutoingiwa na hamu ya kuja kufanana na Baba yake mzazi.

Sioni dhambi yoyote ile kwa mtoto kurithi mapenzi ya kitu fulani kutoka kwa mzazi wake. Inategemea na uwezo wa mzazi kumshawishi mtoto wake kuamua kufanana nae, japo wapo wazazi wengi ambao humuacha mtoto wao awe huru katika kufanya analohisi linamfaa kulifanya maishani mwake.

Zipo familia zinapenda ualimu, Baba mpaka mtoto wa mwisho wanakuwa waalimu, hakuna dhambi yoyote ile maji kufuata mkondo.

Zipo familia zinapenda uanasayansi, Baba mpaka mtoto wa mwisho wote wanavaa majoho meupe wakiwa maabara, hakuna kosa lolote linalofanyika kwa wao kuamua kujikita katika fani hiyo.

Mfano Baba yangu ni mwanasheria mbobezi, kuna ubaya gani na mimi nikawa mwanasheria mbobezi?, ni kosa kufuata nyayo za Mzazi wangu?.

Kibaya ni pale ambapo nafasi ya Baba na Mtoto walio kwenye taaluma moja, inapotumika vibaya kwa maslahi binafsi na kuendekeza zile hulka zilizo kinyume na matarajio ya jamii inayowatazama. Kuiipenda fani ya mzazi mara nyingi ni tabia ambayo mtoto anafanya maamuzi baada ya kuhakikishiwa usalama wa kimaisha na mzazi huyo.

Kosa linakuwa pale Baba, Mama na watoto walio kwenye fani moja wanapokwenda kinyume kabisa na matakwa halisi ya fani hiyo na hivyo kuwakwaza wote wanaowaheshimu. Wanapojirahisisha na kukubali kuchafua majina yao kwa kuendekeza rushwa nyepesi na kuwakwaza wadau wanaotegemea kuona mema yakitoka kwao.

Familia zinakwenda bungeni kwa kasi na hili limekuwa likiwaudhi baadhi ya watu. Lakini hata kingekuwa ni chama kingine zaidi ya CCM kinatawala Tanzania sioni ni kwa namna gani viongozi wangeweza kukwepa ushawishi wa moja kwa moja kutoka kwa watu wenye kuwahusu kwa asilimia mia moja.

Maji hufuata mkondo siku zote.
 
Abedi Pele enzi zake akaichezea timu ya Taifa ya Ghana aliwika vilivyo. Alicheza 9 na 10 naukumbuka wepesi wake na namna alivyowasumbua mabeki. Jina lake la kuzaliwa ni Abedi Ayew lakini mashabiki wakaona wamfananishe na Mfalme Pele mwenyewe.

Baada ya kustaafu soka watoto wake wawili wakaamua kufuata nyayo za Baba yao. Jordan na Andre wamecheza pale Uingereza kwa misimu kadhaa pia ni sehemu ya kikosi cha Ghana kinachoshiriki afcon mara kwa mara, wameirithi kaka aliyoifanya Baba yao na kila anayewaona anawapigia makofi.

Alikuwepo Profesa mmoja mwenyeji wa Kilimanjaro, aliaga dunia mwaka 2021 inasemekana alisumbuliwa na COVID19, alikuwa ni mtaalam wa magonjwa ya watoto, aliishi Mbezi Beach. Watoto wa profesa yule pia ni wataalam wa afya wameirithi kazi ya Baba yao na wanaziendeleza shughuli alizofanya mzazi wao kwa umahiri.

Sioni dhambi yoyote kwa mtu kuirithi fani ya Baba au Mama yake. Mara nyingi wanakua huku wakiwatazama wazazi wao kwa ukaribu. Wanajikuta wakitamani siku moja kupita njia zile zile za wazazi na ni vigumu wazazi kuwavunja moyo.

Sishangai kuiona Familia ya mstaafu Kikwete ikizama kwenye siasa. Ridhiwani amekua akimuona Baba yake majukwaani akishughulika na siasa za moja kwa moja. Mama Salma pia anao wito wa kisiasa wa moja kwa moja hivyo ni vigumu kwa mtoto wao kutoingiwa na hamu ya kuja kufanana na Baba yake mzazi.

Sioni dhambi yoyote ile kwa mtoto kurithi mapenzi ya kitu fulani kutoka kwa mzazi wake. Inategemea na uwezo wa mzazi kumshawishi mtoto wake kuamua kufanana nae, japo wapo wazazi wengi ambao humuacha mtoto wao awe huru katika kufanya analohisi linamfaa kulifanya maishani mwake.

Zipo familia zinapenda ualimu, Baba mpaka mtoto wa mwisho wanakuwa waalimu, hakuna dhambi yoyote ile maji kufuata mkondo.

Zipo familia zinapenda uanasayansi, Baba mpaka mtoto wa mwisho wote wanavaa majoho meupe wakiwa maabara, hakuna kosa lolote linalofanyika kwa wao kuamua kujikita katika fani hiyo.

Mfano Baba yangu ni mwanasheria mbobezi, kuna ubaya gani na mimi nikawa mwanasheria mbobezi?, ni kosa kufuata nyayo za Mzazi wangu?.

Kibaya ni pale ambapo nafasi ya Baba na Mtoto walio kwenye taaluma moja, inapotumika vibaya kwa maslahi binafsi na kuendekeza zile hulka zilizo kinyume na matarajio ya jamii inayowatazama. Kuiipenda fani ya mzazi mara nyingi ni tabia ambayo mtoto anafanya maamuzi baada ya kuhakikishiwa usalama wa kimaisha na mzazi huyo.

Kosa linakuwa pale Baba, Mama na watoto walio kwenye fani moja wanapokwenda kinyume kabisa na matakwa halisi ya fani hiyo na hivyo kuwakwaza wote wanaowaheshimu. Wanapojirahisisha na kukubali kuchafua majina yao kwa kuendekeza rushwa nyepesi na kuwakwaza wadau wanaotegemea kuona mema yakitoka kwao.

Familia zinakwenda bungeni kwa kasi na hili limekuwa likiwaudhi baadhi ya watu. Lakini hata kingekuwa ni chama kingine zaidi ya CCM kinatawala Tanzania sioni ni kwa namna gani viongozi wangeweza kukwepa ushawishi wa moja kwa moja kutoka kwa watu wenye kuwahusu kwa asilimia mia moja.

Maji hufuata mkondo siku zote.
Sentence moja tu ingetosha
 
Mfano Baba yangu ni mwanasheria mbobezi, kuna ubaya gani na mimi nikawa mwanasheria mbobezi?, ni kosa kufuata nyayo za Mzazi wangu?.
Kama umefaulu darasani kwa viwango vinavyotakiwa bila kupigwa factor ya mzazi wako, na ukawa na viwango na vigezo vyote vya kuwa mwanasheria mbobezi...hataka mimi nitajitolea bure kukusaidia ukawe mtetezi wa ' kesi zilizofunguliwa dhidi ya Familia za Gaddafy, Slobodan Milosevic, Samora wa Msumbiji ( kwa ujumla wao R.I.P)' ni mfano huu.
 
Umeandika mawazo mazuri kaka, lakini;

Wewe unadhani hao kina Ayew wanapewa nafasi ya kucheza kwa sababu baba yao alikuwa mchezaji?

Unadhani mtoto wa Messi au Ronaldo watapewa Ballon d'Or kwasababu baba zao walipewa?

Kama watu wengine watanyimwa wasichukue fomu kwasababu mtoto wa fulani amechukua unadhani hiyo inamaanisha nini?

Ukiandika huwa una consider performance na fair competition?

Kama sivyo inabidi ufikirie upya na uweke mawazo yako sawia.
 
Umeandika mawazo mazuri kaka, lakini;

Wewe unadhani hao kina Ayew wanapewa nafasi ya kucheza kwa sababu baba yao alikuwa mchezaji?

Unadhani mtoto wa Messi au Ronaldo watapewa Ballon d'Or kwasababu baba zao walipewa?

Kama watu wengine watanyimwa wasichukue fomu kwasababu mtoto wa fulani amechukua unadhani hiyo inamaanisha nini?

Ukiandika huwa una consider performance na fair competition?

Kama sivyo inabidi ufikirie upya na uweke mawazo yako sawia.
Watoto hukua wakiwa karibu na baba yao wanamtazama anachokifanya na wao wanajikuta wakipita njia zile zile anazopita baba.

Mtoto wa mwanasheria anayekua akimtazama baba mwanasheria kuna asilimia zaidi ya 90 akaipenda fani ya sheria, wazazi wengi wanapomuona mtoto anajenga hamu ya kufanana na wao wanafurahi na kuwatia moyo ili waweze kuingia kwenye fani husika.

JK alikuwa anaongea na mwandishi namna alivyokuwa kwenye michakato ya kuutaka urais na yote aliyafanya pembeni ya Ridhiwani. Hata zile hotuba zake nyingi aliyekuwa akizichapisha ni Ridhiwani yaani mzee anasema cha kuandika na mtoto anakichapisha kwenye laptop.

Huwezi kuona ajabu kwa Ridhiwani kupata hamu ya kuingia kwenye siasa tangu akiwa na umri mdogo ikiwa makuzi yake ndio hayo ya kumuandikia baba hotuba za kisiasa. Wengi tunamnyooshea kidole Ridhiwani na Kikwete kwa sababu ya chuki tu.
 
Wewe Fala mjingamjinga mpumbavu usiyejielewa mfano wako ni very irrelevant kwa wezi kina riziwani na Malaya mama yake salimia.
Hao wameonga kupitishwa na ccm bila kupingwa unasema sijui mamavi gani .
.mkunndu wakoo mchu kumama mako
Matusi yako yanaonyesha ulivyo na hasira nyingi za kitoto.

Mtoto kuipenda fani ya baba sio dhambi hata kidogo.
 
Matusi yako yanaonyesha ulivyo na hasira nyingi za kitoto.

Mtoto kuipenda fani ya baba sio dhambi hata kidogo.
Wajinga wajinga kama nyie mnaoandika maposti yenu ya kichawa kifala Fala lazima niwakemee kama mapepo yanavyokemewa madhabahuni.
Kwa hiyo mtoto na mke wote wamependa fani ya baba na wote wanapitishwa bila kupingwa.
Embu jaribu kutumia vizuri hata kidogo ubongo uliopewa na Mungu kwa hizi akili zako ni wazi unamzihaki Mungu.
Unaonekana huna akili au hutumii vizuri akili zako kwa sababu za kimaslai au njaa zako
 
Wajinga wajinga kama nyie mnaoandika maposti yenu ya kichawa kifala Fala lazima niwakemee kama mapepo yanavyokemewa madhabahuni.
Kwa hiyo mtoto na mke wote wamependa fani ya baba na wote wanapitishwa bila kupingwa.
Embu jaribu kutumia vizuri hata kidogo ubongo uliopewa na Mungu kwa hizi akili zako ni wazi unamzihaki Mungu.
Unaonekana huna akili au hutumii vizuri akili zako kwa sababu za kimaslai au njaa zako
Mjinga mjinga wewe ambaye unadhani kutukana hovyo ndio ujanja. Kuna ubaya gani mtoto na mke kuamua kuifuata fani ya baba nyumbani?.

Nyumba ya Dr wa watoto aliyefariki mwaka 2021 imejaa madaktari, baba mtaalam wa watoto, watoto na mke wake wataalam wa udaktari mwingine, kuna dhambi gani?.

Hawajampinga Ridhiwani jimboni kwake na hawajaona sababu ya kufanya hivyo, unataka kuleta dharau kwamba hawajui wanachokifanya?.

Tumia lugha za kawaida achana na huo utoto wa matusi, hujui unaongea nani.
 
Back
Top Bottom