Hakuna aisee ndiyo yale yale ya fake election zinatumika billions chungu nzima wakati matokeo yanajulikana wazi. Nilifurahia sana uchaguzi wa Ghana upinzani kushinda na kupewa nchi bila kumwaga damu. Sijui kama hili litakuja kutokea hapa kwetu.
Hoja mfu hiyo, kwa sababu uliyoitoa kwamba uchaguzi huru na wa haki ni pale tu upinzani unaposhinda!
Kama upinzani una viongozi wenye uchu wa madaraka tu na walalamishi, kila kukicha, unadhani wapiga kura ni wajinga kutokulijua hilo!
Kuongoza nchi siyo sawa na kuongoza chama chochote, hata cha siasa, ambacho wanachama wake ni wa itikadi moja, wafuasi na wanazi tu.
Viongozi wa vyama vya upinzani, kwa mfano hapa nchini, wameonesha, kwa maneno na vitendo, kwamba ni mabingwa wa kutetea maslahi yao. Kwani wakati wapiga kura wao wanatarajia kutetewa bungeni, wao mara kwa mara wabunge wao wamesusia vikao wakidai kutokuoneshwa 'live' au hupeleka 'hayo malalamiko' yao kwa vyombo vya habari, badala ya kwenye vyombo halali vya haki Kikatiba.
Upinzani Kenya umeshindwa tena, sijui viongozi wa upinzani hapa watakuwa na lipi la kusema, baada ya mmoja wao kumpigia debe Rais aliyekuwa madarakani! Tunasubiri kauli yao kwa hamu.