Fainali mashindano ya CAF iwe mechi 3 na siyo 1 au 2

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,151
7,920
Mimi huwa napenda kuja na hoja fikirishi kwa hiyo wale wasiopenda kufikiri wananionaga hamnazo. Muda huwa unadhihirisha kile ninachosemaga.

Kumekuwa na malalamiko ya kutaka CAF ibadili fainali za mechi za Klabu Bingwa na Kombe la Shirikisho kutoka mechi mbili na kubakiwa na moja. Binafsi napendeleza fainali hizo ziwe zinachezwa kwa mtindo wa mechi 3 na siyo 1 kama inavyopendekezwa na baadhi ya watu au 2 kama ilivyo sasa. Huu utaratibu wa mechi 3 unaweza kuanza kutumika hatua ya robo fainali.

Ukiacha changamoto ya Afrika ya mashabiki kusafiri umbali mrefu kwenda nchi ya 3 kwa ajili ya fainali, nitaongelea zaidi hatari ya kutopata bingwa anayestahili endapo fainali itakuwa mechi moja. Tukumbuke tunataka bingwa wa viwango na siyo wa kubahatisha.

Mechi moja ina hatari ya kutoa mshindi asiyestahili kwa sababu inawezekana yule mwenye uwezo labda asiamke vizuri siku hiyo. Hii ni sawa na uende kufanya mtihani ukute kuna swali moja. Kuna mjinga anaweza pasi kuliko wale wenye uelewa mpana zaidi kwa sababu tu jana yake kitu pekee alichopitia ni hilo swali. Ndiyo maana mitihani ina maswali mengi ili kutoa nafasi kwa mwenye uwezo zaidi kuonekana na vilaza pia kuonekana.

Ligi ya mpira wa kikapu ya NBA inalijua hili vizuri sana ndiyo maana "playoffs" zake ni mechi 7. Hii ni kuhakikisha yule mwenye uwezo ndiyo anapita kila hatua hadi anapatikana bingwa.

Kuhusu mechi ya 3 kuchezwa wapi, kuna njia tofauti zinaweza kutumika. Wanaweza kuangalia yule aliye juu ya mwenzake katika rank za CAF kupewa faida ya wenyeji kwa mechi 2, inaweza pia kuwa yule atakayeanza mechi ya kwanza apewe ahueni ya mechi mbili za kwanza kabla ya kumalizia mechi ya 3 kwa timu ya pili. nk.

Binafsi naamini future bora ya mpira wa Afrika ni kufanya mashindano ya AFCON kama ligi rasmi ya Afrika na hizi za vilabu kuwa ya chini yake. Niliwahi kulieleza hili katika uzi huu.
 
Ukijua basket ni pts
Na soccer ni goals
Yani game 3 izo 1,2 nani atakuja kuangalia?
 
Bingwa wa uhakika ni kwenye ligi (kila mmoja anacheza na mwingine) CUP Competition kuna happenstances na kukutana na timu nyepesi kuliko mwenzako...

Lakini vitu kama Mashindano haya na hata World Cup sio practical kuzifanya ligi; zitachukua muda mrefu na game nyingi hivyo kupelekea ligi nyingine kuwa disrupted....

Anyway kuna msemo kama wewe ni mzuri sana basi utamfunga kila utakayekutana nae.... Na kwa kusema hivyo achana na game mbili fainali iwe game moja kuhusu itachezwa wapi hio inapangwa hata kabla ya mashindano kuanza....
 
Bingwa wa uhakika ni kwenye ligi (kila mmoja anacheza na mwingine) CUP Competition kuna happenstances na kukutana na timu nyepesi kuliko mwenzako...

Lakini vitu kama Mashindano haya na hata World Cup sio practical kuzifanya ligi; zitachukua muda mrefu na game nyingi hivyo kupelekea ligi nyingine kuwa disrupted....

Anyway kuna msemo kama wewe ni mzuri sana basi utamfunga kila utakayekutana nae.... Na kwa kusema hivyo achana na game mbili fainali iwe game moja kuhusu itachezwa wapi hio inapangwa hata kabla ya mashindano kuanza....
Kupanga fainali ichezwe wapi kabla ya mashindano kuanza ni shida kwa sababu ikitokea klabu mojawapo iliyofika fainali inatokea sehemu hiyo, timu ya pili inaona haitakuwa fair kwao matokeo yake venue inabadilishwa. Hili limeshatokea.

Na bado kuna tatizo la mashabiki kutokuja uwanjani kama timu zote mbili siyo za eneo hilo. Bado logistics za usafiri siyo nafuu au rafiki sana labda kama timu zote mbili zinazocheza ni za nchi jirani na host pia ni jirani, kwa mfano Wydad vs Al Ahly ichezwe Algeria.

Hizo hoja zako nyingine za mwanzo sina uhakika ulikuwa unajibu lipi nililosema ingawa sizipingi.
 
Mshindi wa basketball anaamuliwa kwa points
Mshindi wa soccer anaamuliwa na magoal hivo game 3 za soccer hazitaongeza ushindani Bali zitapunguza
Bado sijaelewa sana point yako ila niseme tu utaratibu wa mechi 3 utaondoa aggregate ya magoli kupata mshindi wa jumla na badala yake itakuwa yule aliyeshinda mechi nyingi zaidi. Kwa maana hiyo, kama timu moja itashinda mechi mbili za mwanzo, mechi ya 3 haitafanyika.

Football imeshawahi kuchukua mawazo kutoka kwenye kikapu, hata wazo la kuhesabu "assists" linatoka kule.
 
Kupanga fainali ichezwe wapi kabla ya mashindano kuanza ni shida kwa sababu ikitokea klabu mojawapo iliyofika fainali inatokea sehemu hiyo, timu ya pili inaona haitakuwa fair kwao matokeo yake venue inabadilishwa. Hili limeshatokea.
Hapo ndio CAF walipochemka.....Kushinda kwenye uwanja wa ugenini pia na against all odds inaonyesha umahili wako; kwahio hata kama mmoja wenu atakuwa na bahati ya kucheza kwake; lakini mwanzo kabla hamjacheza ni kwamba mlikuwa mna chance sawa
Na bado kuna tatizo la mashabiki kutokuja uwanjani kama timu zote mbili siyo za eneo hilo. Bado logistics za usafiri siyo nafuu au rafiki sana labda kama timu zote mbili zinazocheza ni za nchi jirani na host pia ni jirani, kwa mfano Wydad vs Al Ahly ichezwe Algeria.
Unadhani mashabiki kindakindaki wakifika fainali wataacha kwenda kuangalia timu zao; pili hadi kuchagua nchi fulani ku-host fainali lazima due dilligence itakuwa imefanyika kwamba wanaweza ku-hodhi mashindano hayo

na hilo la kuchagua uwanja kabla linahakikisha mpira unapelekwa kwenye nchi nyingi zaidi hata kama hazishiriki au hazina uwezo wa kufika fainali hence kukuza zaidi the beautiful game..., by the way dunia ya sasa walioko nje / wanaoangalia kwenye luninga na Pesa za Sponsorship ni nyingi kuliko hata wanaonunua ticket na kuingia uwanjani; kwahio for the better of the game ni kuhakikisha mpira unazambazwa kila kona..., unadhani kama fainali ikipelekwa huko TIMBUKTU ni mashabiki wangapi huenda wakawa converted kupenda mpira ?
 
Mimi huwa napenda kuja na hoja fikirishi kwa hiyo wale wasiopenda kufikiri wananionaga hamnazo. Muda huwa unadhihirisha kile ninachosemaga.

Kumekuwa na malalamiko ya kutaka CAF ibadili fainali za mechi za Klabu Bingwa na Kombe la Shirikisho kutoka mechi mbili na kubakiwa na moja. Binafsi napendeleza fainali hizo ziwe zinachezwa kwa mtindo wa mechi 3 na siyo 1 kama inavyopendekezwa na baadhi ya watu au 2 kama ilivyo sasa. Huu utaratibu wa mechi 3 unaweza kuanza kutumika hatua ya robo fainali.

Ukiacha changamoto ya Afrika ya mashabiki kusafiri umbali mrefu kwenda nchi ya 3 kwa ajili ya fainali, nitaongelea zaidi hatari ya kutopata bingwa anayestahili endapo fainali itakuwa mechi moja. Tukumbuke tunataka bingwa wa viwango na siyo wa kubahatisha.

Mechi moja ina hatari ya kutoa mshindi asiyestahili kwa sababu inawezekana yule mwenye uwezo labda asiamke vizuri siku hiyo. Hii ni sawa na uende kufanya mtihani ukute kuna swali moja. Kuna mjinga anaweza pasi kuliko wale wenye uelewa mpana zaidi kwa sababu tu jana yake kitu pekee alichopitia ni hilo swali. Ndiyo maana mitihani ina maswali mengi ili kutoa nafasi kwa mwenye uwezo zaidi kuonekana na vilaza pia kuonekana.

Ligi ya mpira wa kikapu ya NBA inalijua hili vizuri sana ndiyo maana "playoffs" zake ni mechi 7. Hii ni kuhakikisha yule mwenye uwezo ndiyo anapita kila hatua hadi anapatikana bingwa.

Kuhusu mechi ya 3 kuchezwa wapi, kuna njia tofauti zinaweza kutumika. Wanaweza kuangalia yule aliye juu ya mwenzake katika rank za CAF kupewa faida ya wenyeji kwa mechi 2, inaweza pia kuwa yule atakayeanza mechi ya kwanza apewe ahueni ya mechi mbili za kwanza kabla ya kumalizia mechi ya 3 kwa timu ya pili. nk.

Binafsi naamini future bora ya mpira wa Afrika ni kufanya mashindano ya AFCON kama ligi rasmi ya Afrika na hizi za vilabu kuwa ya chini yake. Niliwahi kulieleza hili katika uzi huu.
Mkuu waafrika huwa wanasubiri wazungu wafikiri na kuamua. We are very Zombie.
Yani kujiamulia sisi hatuwezi mpaka ulaya iamue.
Ni vizuri kuweka mfumo rafiki kwetu sio lazima tuwe kama wazungu, sisi sio wazungu.
 
Hapo ndio CAF walipochemka.....Kushinda kwenye uwanja wa ugenini pia na against all odds inaonyesha umahili wako; kwahio hata kama mmoja wenu atakuwa na bahati ya kucheza kwake; lakini mwanzo kabla hamjacheza ni kwamba mlikuwa mna chance sawa

Unadhani mashabiki kindakindaki wakifika fainali wataacha kwenda kuangalia timu zao; pili hadi kuchagua nchi fulani ku-host fainali lazima due dilligence itakuwa imefanyika kwamba wanaweza ku-hodhi mashindano hayo

na hilo la kuchagua uwanja kabla linahakikisha mpira unapelekwa kwenye nchi nyingi zaidi hata kama hazishiriki au hazina uwezo wa kufika fainali hence kukuza zaidi the beautiful game..., by the way dunia ya sasa walioko nje / wanaoangalia kwenye luninga na Pesa za Sponsorship ni nyingi kuliko hata wanaonunua ticket na kuingia uwanjani; kwahio for the better of the game ni kuhakikisha mpira unazambazwa kila kona..., unadhani kama fainali ikipelekwa huko TIMBUKTU ni mashabiki wangapi huenda wakawa converted kupenda mpira ?
Hoja zako sizipingi ila hazijazingatia demograph ya Afrika ilivyo na usambazaji usio sawia wa hali za kiuchumi kati ya nchi na nchi. Juzi juzi kulikuwa na mashindano ya U-17 kule Algeria, mechi nyingi viwanja vilikuwa vitupu, pia tumeona mechi za Yanga dhidi ya Marumo, Rivers, Bamako zikichezwa kwenye viwanja vitupu. Kwa hiyo sidhani kama issue ni kukuza upenzi wa soka maana naamini maeneo hayo wanapenda sana soka. Lakini mechi ya fainali ikikosa mashabiki uwanjani ni mbaya kwa brand ya CAF.
 
Hoja zako sizipingi ila hazijazingatia demograph ya Afrika ilivyo na usambazaji usio sawia wa hali za kiuchumi kati ya nchi na nchi. Juzi juzi kulikuwa na mashindano ya U-17 kule Algeria, mechi nyingi viwanja vilikuwa vitupu, pia tumeona mechi za Yanga dhidi ya Marumo, Rivers, Bamako zikichezwa kwenye viwanja vitupu. Kwa hiyo sidhani kama issue ni kukuza upenzi wa soka maana naamini maeneo hayo wanapenda sana soka. Lakini mechi ya fainali ikikosa mashabiki uwanjani ni mbaya kwa brand ya CAF.
Unadhani game la Fainali likichezwa Tanzania hata kama timu ni za kutokea Sayari ya Pluto na Mars uwanja hautatema ?

Inabidi wazingatie bei na wafanye promo za kutosha kama uwanja haujai kwenye fainali basi gundua kwamba CAF wanapwaya kwenye Promo zao na sehemu husika does not deserve to host the final..... Kuweka mechi nyingi za fainali kuta-dilute utamu na kuongeza gharama

Unaongelea Basket umesahau kwamba hizo playoffs zote ni nchi moja na hapa unaongelea continent ambayo to say the least kutoka point A mpaka B sio lelemama
 
Unadhani game la Fainali likichezwa Tanzania hata kama timu ni za kutokea Sayari ya Pluto na Mars uwanja hautatema ?

Inabidi wazingatie bei na wafanye promo za kutosha kama uwanja haujai kwenye fainali basi gundua kwamba CAF wanapwaya kwenye Promo zao na sehemu husika does not deserve to host the final..... Kuweka mechi nyingi za fainali kuta-dilute utamu na kuongeza gharama

Unaongelea Basket umesahau kwamba hizo playoffs zote ni nchi moja na hapa unaongelea continent ambayo to say the least kutoka point A mpaka B sio lelemama
Nafikiri CAF wanafanya kwa jinsi wanavyoweza kukuza msisimko wa mashindano yake. Ndiyo maana sitashangaa msimu ujao Simba kujikuta kundi moja na Wydad.

Sehemu ambazo ungedhani ndiyo zinadeserve kuhost fainali kutokana na mafanikio yao kisoka pamoja na miundombinu ya kisasa ndiyo hizo ambazo kuna uwezekano mkubwa zisijaze viwanja labda kama timu mojawapo inayocheza inatoka jirani. Kwa hiyo labda vipaumbele viwe tofauti na hilo la kudeserve.
 
Unadhani game la Fainali likichezwa Tanzania hata kama timu ni za kutokea Sayari ya Pluto na Mars uwanja hautatema ?

Inabidi wazingatie bei na wafanye promo za kutosha kama uwanja haujai kwenye fainali basi gundua kwamba CAF wanapwaya kwenye Promo zao na sehemu husika does not deserve to host the final..... Kuweka mechi nyingi za fainali kuta-dilute utamu na kuongeza gharama

Unaongelea Basket umesahau kwamba hizo playoffs zote ni nchi moja na hapa unaongelea continent ambayo to say the least kutoka point A mpaka B sio lelemama
Kupunguza mzunguko, mechi mbili za kwanza au mbili za mwisho zinaweza kuchezwa sehemu moja badala ya Point A-B-A.
 
Back
Top Bottom