The Quonquerer
JF-Expert Member
- May 14, 2009
- 777
- 111
Kwa wale wataalam, mimi nimekuwa sceptical na hii kitu ya zero rating kwa bidhaa kutoka Kenya na zile za kwetu kwenda kwao. Hivi, kwa kufikia uamuzi huu, si kwamba tume-weaken our potential of domestic industrial growth? Je ulikuwa uamuzi sahihi?Je kuna simulation study iliyofanyika kuonyesha kuwa faida ya kutotoza ushuru itakayopatikana ni kubwa kuliko ule ushuru tuliokuwa tukikusanya (trade off between ‘future' economic growth and revenue loss, i bet in billions). Je hata hizo chache tunazopelekwa kwao, wanapoziwekea NTBs (vikwazo visivyo vya ki-ushuru), maana soko lile lina matatizo, si kwamba tunazidi kuuvaa mkenge? Je uko mkakati upi ulio imara wa kutambua ROOs (Rules of Origin) ili kuwa na uhakika kwamba bidhaa zote zinazo-qualify kweli zinatoka Kenya, TRA na Wizara ya Viwanda na Biashara wana umakini na uwezo kiasi gani kuweza kubaini hili? Na kwenye Soko la Pamoja, je usimamiaji wa utambuzi wa professional qualifications uko makini kiasi gani kuhakiki kuwa hatutaleta vihiyo kwetu hapa kwa kisingizio cha soko la pamoja, hasa iwapo utambuzi wa ndani wenyewe ni tatizo? Na Mutiso , balozi wao anaposema kuwa nchi kubwa zimeendelea kiviwanda hivyo zinataka kutu-weaken as a region kuleta bidhaa zao kwetu na hivyo tufanye biashara kati yetu,maana the Rest of the World tumewawekea CET (Common External Tariff), wao wenyewe kama Kenya, si kwamba nao wanafanya hivyo hivyo kwa nchi wanajumuia wakati wao hawataki kufanyiwa na nchi nyingine. Nina maswali mengi zaidi ya hayo kuliko majibu kuhusu huu ushirikiano, nimeuliza tena kwa sababu kuna member wa JF mmoja na jina nalikumbuka alikuja hapa akaniita ‘myopic nationalist' na mwingine ‘that i live in fear ‘which is OK to me kama sielewi. Sasa, kabla na wengine hawajaniita hivyo, naomba kuelemishwa kwanza kuhusu hayo, maana mimi sielewi mpaka leo! Nadhani JF ni sehemu ya kuelemishana zaidi kuliko kugombana. Naomba kusaidiwa! A thing is that, i don't practice these things, so am not in a picture!