Sasa kwa nini ukamfuata wakati unamuogopa?. Ni kweli hiyo ndio milio ya bundi. Lakini sio kwamba akilia lazima itokee misiba. Kama kwenye eneo lenu kuna miti mikubwa yenye uwezo wa kimficha bundi,basi hapo yanaweza kuwa maficho yake,na anaweza kuwa analia hapo mara kwa mara. Kwenye mji wetu zamani kulikuwa na miti miti mingi mikubwa,mivule na mikuyu,basi mara nyingi walikuwa wanapenda humo,siku hizi miti mingi imekatwa. Zamani nikiwa mdogo watoto wengi tulikuwa tunaogopa sana mlio wa bundi,ukisikia analia unajifunika sana. Hata wakubwa zetu walituaminisha kwamba ni ndege mbaya,anaashiria mabaya. Lakini siku hizi nikisikia mlio wa bundi naupenda sana,napenda nisikie hivyo ni mlio unaonibembeleza mpaka nalala. Milio yote miwili. (Wa dar haiwahusu)