Fahamu yafuatayo kuhusu mdudu mende

Fahamu yafuatayo kuhusu mdudu mende

hydroxo

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2015
Posts
6,172
Reaction score
14,029
1.Ni mdudu anayeweza kuishi zaidi ya mwezi bila ya kula chakula chochote.

2.Ni mdudu anayeweza kuishi wiki mbili bila ya kunywa maji.

3.Wakati moyo wa mwanadamu ni mmoja wenye chemba nne mende ana moyo mmoja wenye chemba kumi na tatu.

4.Baadhi ya mende wa kike hawaitaji wanaume kuweza kuzalisha mayai hupandana wao kwa wao na kutaga mayai katika kipindi chote cha maisha yao.

5.Mende ana uwezo wa kukaa kwa zaidi ya dakika 40 bila ya kupumua.

6.Mende ana uwezo wa kuishi zaidi ya wiki mbili akiwa amekatwa kichwa.

7.Ana uwezo wa zaidi ya mara 15 ya binadamu wa kuzuia miale mikali ya nuklia isimdhuru na kubaki hai

8.Mende ni mdudu asiye na mapafu.

9.Ana uwezo wa kuruka maili 3 kwa saa.
 
UMESAHAU HII SUPU YAKE INAONGEZA NGUVU ZA KIUME

cockroach-in-soup-yuan-fu-restaurant-chiayi.jpg


cockroah-soap.jpg




0bce0be825233bb73f78b0bc4a4cc887.jpg




cockroach_carolynchee.jpg
 
Naweza amini maana wale jamaa walionaswa shimoni mgodini walikuwa wanakula mende na vyura. Waka survive
 
Kuna mmoja umeisahau. Mende anaruka lakini ukimuweka miguu juu atafika kufa bado hajaweza kugeuka
Ni kweli kabisa mkuu inamuwia vigumu kugeuka ikiwa miguu yake itaangalia juu.
 
K

Kama ni hivyo kwann mende wa kiume wawepo
farajakwangu,si aina zote za mende wa kike wanaweza kutaga mayai bila ya mende wa kiume.

Kuna aina ya mende wanaitwa parthenogenetic cockroach mfano mzuri ni surinam cockroach wanaopatikna katika species ya Pycnoscelus surinam wana uwezo wa kutaga mayai bila ya mende wa kiume.
 
Back
Top Bottom