Fahamu historia ya Mama Sophia Mathew Simba

Fahamu historia ya Mama Sophia Mathew Simba

Thanks for the thread. Mimi kama mwanamke mtanzania naomba kujua UWT inamwakilisha nani? Ilianza kama chama cha wanawake wa Tanzania, na ikawa imeimarika sana wakati wa chama kimoja. Lakini baada ya kuja multiparties, UWT imekuwa umoja wa wanawake wa CCM. Hilo limeiondolea credibility machoni mwa wanawake. As long as haikubali kuwa independent of party politics na kusimamia maslahi ya wanawake wote wa Tanzania bila kujali kama ni wana CCM au la, sioni kama kuna mtu yeyote atakayeweza kurudisha hadhi ya UWT ya zamani. Mimi binafsi siko tayari kuwa mwanachama wa UWT kabla sijajua hicho chama kinasimamia vipi maslahi yangu kama mwanamke wa kitanzania.
 
Mama Sophia Simba: Kwanza nikiri kwamba si jambo zuri kwamba katibu mkuu wangu imebidi Baraza Kuu limwondoe. Mimi binafsi siyo kitu ambacho nilitarajia, kwa sababu mimi ndiye niliyemtafuta yeye na jina lake kulipeleka kwenye vikao vya chama ili lipitishwe. Kwa hiyo, hiyo imeonyesha kwamba ni udhaifu kwa upande wangu. Nikiri kwamba sikulifanyia kazi vizuri lile jina. Pengine nilikuwa sikujiandaa vizuri.
Binadamu kufanya makosa ni kawaida, na pale nilikosea. Hata hivyo, nilijitahidi sana kufanya naye kazi vizuri. Nimekaa naye kipindi cha mwaka mmoja. Unapopewa madaraka inabidi kwanza ujifunze, kwa hiyo nilijitahidi sana kuhakikisha kwamba katibu mkuu huyu, ambaye mimi mwenyewe nilimtafuta, aweze ku-cope na ile ofisi. Lakini kukawa kuna matatizo ya… Kwanza huwezi kumfananisha huyo na akina Thecla Mchauru, Kate Kamba, Dk Msimu ambao kiwango cha elimu yao kidogo ilikuwa zaidi. Hata Halima Mamuya elimu yake iko juu zaidi ya huyu. Huyu alibebeshwa mzigo ambao hakustahili, tulifanya makosa. Tulimbebesha mzito mkubwa wa kiutendaji. Pengine kisiasa kazi nyingine angeweza kuzifanya, lakini kiutendaji… Kuna kazi za utendaji zina miiko yake ambayo kiwango cha elimu yake ilikuwa kidogo kina matatizo.

Raia Mwema: Sawa kulikuwa na makosa, lakini wewe ulimpataje pataje hadi akaukwaa ukatibu mkuu wa UWT? Mama Sophia Simba: Huyu alikuwa mjumbe wa Baraza Kuu la UWT, ndicho kitu kimoja ambacho kilinifanya nimteue. Nimekuwa naye kwenye baraza tokea mwaka 2003. Mimi nimemjua Husna wakati nikigombea ujumbe wa Baraza Kuu. Kwa hiyo, nilipokwenda Arusha yeye ndiye aliyenisaidia kutafuta kura, siyo campaigner, lakini ndiyo nilianza kumfahamu.

Lakini nikamfahamu pia ndani ya vikao. Kwa hiyo nilimjua kwa hivyo. Na kwa bahati mbaya sana, sikujaribu kuomba ushauri kwa mtu yeyote kutaka kujua habari zake zaidi. Ndiyo maana nasema nakiri makosa. Hakuna mtu aliyenishawishi kuhusu yeye.


Hii habari imenishangaza sana...yaani Ms Simba anakiri kuwa Husna Mwilima alikuwa na udhaifu kwa kiasi hicho...yet Rais Kikwete amemteua kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba?

What does that say about President Judgement?

Kana kwamba hiyo haitoshi, Waziri wetu Ms Simba anasema Wanawake ambao hawapo kwenye chama au UWT ni kwamba "WAPO WAPO TU"..!!!

Halafu kuwa wana JF humu wanasema hii interview ni nzuri..ama kweli Tanzania tuna great Thinkers.
 
Hii habari imenishangaza sana...yaani Ms Simba anakiri kuwa Husna Mwilima alikuwa na udhaifu kwa kiasi hicho...yet Rais Kikwete amemteua kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba? What does that say about President Judgement?

Ndugu yangu hapo jibu kichwani.....
 
mkataba miaka 33???duh kisha kiasi wanacholipwa wao kiduuchu kwa mwaka haya na huyu mama anasema aah tumejifunza kutokana na makosa,sasa makosa yenu yatamfanya huyo muhindi atawale hilo jengo miaka 33 na kuendelea kuwalipa hivyohivyo visenti mnavyolipwa na nyinyi mnapiga miayo tu,yaani nashindwa hata kuendelea kuandika kwa hasira,huyo manji anajua kweli kucheza na akili mbofumbofu za viongozi wetu,yaani utaona jinsi jamaa anavyotengeneza pesa kilaini sana daah.
 
Hivi mnaomtetea huyu mama mipasho anayeona sifa kuwa na affair ina maaana hamjui ziongozi wangapi duniani wame resign kwa sababu ya affairs???? Kama mnataka mabadiliko lazima kuwa na morals, na boundaries. How can we join the rest of the developed countries if we still think like this...anyway viongozi wetu ndio reflection yetu.

Mimi naona JK ndio mwenye matatizo..Hii hapa listi ya viongozi nk. walio resign kwa sababu ya extramarital
http://en.allexperts.com/e/s/se/sex_scandal.htm
Na vingine nyingi tu!

http://www.msnbc.msn.com/id/31522908/ns/politics-more_politics/
http://www.watoday.com.au/opinion/politics/moving-day-approaches-but-should-buswell-go-20100425-tl04.html?autostart=1
http://abcnews.go.com/Politics/story?id=7930748&page=1
http://www.thaindian.com/newsportal/uncategorized/orissa-minister-resigns-over-sex-scandal_100129448.html
 
Thanks for the thread. Mimi kama mwanamke mtanzania naomba kujua UWT inamwakilisha nani? Ilianza kama chama cha wanawake wa Tanzania, na ikawa imeimarika sana wakati wa chama kimoja. Lakini baada ya kuja multiparties, UWT imekuwa umoja wa wanawake wa CCM. Hilo limeiondolea credibility machoni mwa wanawake. As long as haikubali kuwa independent of party politics na kusimamia maslahi ya wanawake wote wa Tanzania bila kujali kama ni wana CCM au la, sioni kama kuna mtu yeyote atakayeweza kurudisha hadhi ya UWT ya zamani. Mimi binafsi siko tayari kuwa mwanachama wa UWT kabla sijajua hicho chama kinasimamia vipi maslahi yangu kama mwanamke wa kitanzania.

Basi badala ya kuitwa UWT, wabadili jina iitwe UWCCM!!
 
swali kwa Sophia Mathew Simba: Unakiri kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Kitwana Kondo kama boyfriend.Unakiri kuwa Kitwana Kondo hakukuoa.Unakiri kuwa wakati wa mahusiano yenu,Kitwana Kondo alikua na mke wake na wewe ulilifahamu hilo.Uone kuwa ulikiuka maadili kuwa na mahusiano na mume wa mtu?huoni kuwa unapaswa kumwomba radhi mke wake kwa kuingilia ndoa yake?
{ The Son Of Africa}


mkuu,heshima mbele
Mwandishi aliyefanyia interview sophia simba sijui alikuwa anafikiria nn,yaani baada ya yule mama kujichanganya tu juu ya issue yake na kitwana basi yeye angemuuliza hilo swali,nafikiri na interview ingeishia hapo hapo.
 
Back
Top Bottom