Mau Mau
JF-Expert Member
- Dec 30, 2012
- 673
- 478
Dhana ya uwepo wa kitu cha siri imeghubika nembo za kwenye sarafu na kufanywa kuwa ishara au alama inayoonekana.
Alama ya 'Jicho' - hili ni jicho ndani ya umbo la pembe tatu - ni moja ya alama inayohusishwa na masuala ya ushetani ambayo pia imeonekana kuwa na uhusiano wa karibu na Iluminati, kundi la watu matajiri linalosemekana kwamba hutafuta kumiliki mali za dunia kwa nguvu ya shetani.
Alama hii ya jicho inadhaniwa kuficha kitu fulani kwasababu yenyewe ipo sehemu fiche kiasi kwamba sio rahisi kwa mtu kuitambua kwa macho yake moja kwa moja.
Pia inajitokeza sio tu kwa makanisa kadhaa bali pia kwenye majengo yenye kujihusisha na imani za kishetani kote duniani na pia alama hiyo ya jicho ipo katika noti za dola za Marekani pamoja na chapa ya muhuri mkubwa wa Marekani.
Ukweli ni njia ya zamani isiyo ya kawaida ya kuashiria nchi. Na alama ya jicho inaashiria matamanio ya kuwa na sauti au nguvu.
Ukichanganya na lile umbo la piramidi, ni kama ishara ya kundi fulani la zamani.
Lakini kwanini watu hulinganisha alama hii na masuala ya ushetani?
Awali kabisa, alama hiyo ya jicho ilikuwa na Kikristo na matumizi ya kwanza kabisa ya alama hiyo yanahusishwa na michoro ya dini hasa ya kumwakilisha mungu.
Ilibuniwa kama ishara ya uangalizi wa huruma ya Mungu juu ya wanadamu.
Chanzo kingine cha alama hiyo ni kitabu cha zamani kabisa cha nembo ambacho kwa mara ya kwanza kabisa kilichapishwa mwaka 1593. Alama hiyo ya jicho iliwekwa kuashiria 'utakatifu' yaani 'mungu'.
Kujenga yaliopita
Hakuna anayejua chanzo cha ubunifu wa alama hii lakini wa kwanza kabisa kuhusika na ubunifu wake aliihusisha na imani za kidini.
Umbo la pembe tatu lilikuwa ni alama ya muda mrefu ya Utatu wa Kikiristo; yaani Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu; na kuna wakati Mungu aliashiriwa kuwa ndani ya umbo hilo la pembe tatu.
Miale ya mwanga ambayo mara nyingi hungaa ndani ya alama hiyo pia ni miongoni mwa alama za mwanzo kabisa za Kikiristo.
Lakini chanzo cha lile jicho ni nini? Mungu amekuwa akiashiriwa kwa njia nyingi hapo kabla, mfano mkono mmoja unaojitokeza kutoka mawinguni lakini sio kama jicho.
#Itaendelea
Alama ya 'Jicho' - hili ni jicho ndani ya umbo la pembe tatu - ni moja ya alama inayohusishwa na masuala ya ushetani ambayo pia imeonekana kuwa na uhusiano wa karibu na Iluminati, kundi la watu matajiri linalosemekana kwamba hutafuta kumiliki mali za dunia kwa nguvu ya shetani.
Alama hii ya jicho inadhaniwa kuficha kitu fulani kwasababu yenyewe ipo sehemu fiche kiasi kwamba sio rahisi kwa mtu kuitambua kwa macho yake moja kwa moja.
Pia inajitokeza sio tu kwa makanisa kadhaa bali pia kwenye majengo yenye kujihusisha na imani za kishetani kote duniani na pia alama hiyo ya jicho ipo katika noti za dola za Marekani pamoja na chapa ya muhuri mkubwa wa Marekani.
Ukweli ni njia ya zamani isiyo ya kawaida ya kuashiria nchi. Na alama ya jicho inaashiria matamanio ya kuwa na sauti au nguvu.
Ukichanganya na lile umbo la piramidi, ni kama ishara ya kundi fulani la zamani.
Lakini kwanini watu hulinganisha alama hii na masuala ya ushetani?
Awali kabisa, alama hiyo ya jicho ilikuwa na Kikristo na matumizi ya kwanza kabisa ya alama hiyo yanahusishwa na michoro ya dini hasa ya kumwakilisha mungu.
Ilibuniwa kama ishara ya uangalizi wa huruma ya Mungu juu ya wanadamu.
Chanzo kingine cha alama hiyo ni kitabu cha zamani kabisa cha nembo ambacho kwa mara ya kwanza kabisa kilichapishwa mwaka 1593. Alama hiyo ya jicho iliwekwa kuashiria 'utakatifu' yaani 'mungu'.
Kujenga yaliopita
Hakuna anayejua chanzo cha ubunifu wa alama hii lakini wa kwanza kabisa kuhusika na ubunifu wake aliihusisha na imani za kidini.
Umbo la pembe tatu lilikuwa ni alama ya muda mrefu ya Utatu wa Kikiristo; yaani Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu; na kuna wakati Mungu aliashiriwa kuwa ndani ya umbo hilo la pembe tatu.
Miale ya mwanga ambayo mara nyingi hungaa ndani ya alama hiyo pia ni miongoni mwa alama za mwanzo kabisa za Kikiristo.
Lakini chanzo cha lile jicho ni nini? Mungu amekuwa akiashiriwa kwa njia nyingi hapo kabla, mfano mkono mmoja unaojitokeza kutoka mawinguni lakini sio kama jicho.
#Itaendelea