Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 2,208
- 4,704
Kwa mujibu wa sheria ya Tanzania, mtu akifanya yafuatayo huhesabiwa kama amefanya kosa la jinai la uhaini hivyo huadhibiwa kulingana na ukubwa wa kosa hilo.
Kifungu cha 39 (1) cha kanuni za adhabu kinasema kuwa mtu yeyote ambaye yumo ndani ya Jamhuri ya Muungano au popote, kujaribu kumuua Rais, kuanzisha vita dhidi ya Jamhuri ya Muungano, kusababisha, kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri kuhusu kifo, kumwondolea Rais heshima na jina la Mkuu wa nchi, Amiri jeshi mkuu, au kiongozi wa Serikali, kupindua serikiali iliyo madarakani, kutishia Serikali, Bunge au Mahakama kwa makosa haya na yale yaliyotajwa hapo juu mtu wa namna hiyo atakuwa ametenda kosa la jinai ambalo ni kosa la uhaini
Mtu atakayekutwa na hatia ya kosa la uhaini adhabu yake ni kifo na sheria hiyo ya kifo imeelezwa katika kifungu cha sheria namba 39 na 40 cha kanuni za adhabu.
Kifungu cha 39 (1) cha kanuni za adhabu kinasema kuwa mtu yeyote ambaye yumo ndani ya Jamhuri ya Muungano au popote, kujaribu kumuua Rais, kuanzisha vita dhidi ya Jamhuri ya Muungano, kusababisha, kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri kuhusu kifo, kumwondolea Rais heshima na jina la Mkuu wa nchi, Amiri jeshi mkuu, au kiongozi wa Serikali, kupindua serikiali iliyo madarakani, kutishia Serikali, Bunge au Mahakama kwa makosa haya na yale yaliyotajwa hapo juu mtu wa namna hiyo atakuwa ametenda kosa la jinai ambalo ni kosa la uhaini
Mtu atakayekutwa na hatia ya kosa la uhaini adhabu yake ni kifo na sheria hiyo ya kifo imeelezwa katika kifungu cha sheria namba 39 na 40 cha kanuni za adhabu.