Exclusive video ya Simba Robo Fainali ya CAF Cup 1993

Exclusive video ya Simba Robo Fainali ya CAF Cup 1993

DELETED ACCOUNT

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
9,805
Reaction score
15,470
Zinaendelea kuibuka video nyingi zaidi za kumbukumbu ya mafanikio ya Simba katika historia ya mpira Tanzania.

Leo nawaletea video ya robo fainali ya CAF Cup 1993 kati ya USM El Harrachi dhidi ya Simba iliyochezwa kule Algeria. Simba ilivuka kigingi hiki na kwenda hadi fainali na kuwa klabu ya kwanza ya Tanzania kufanya hivyo.


Kumbukumbu zote za timu ya Simba inabidi ziwekwe pembeni ya ile Rolls-Royce ya Nyerere pale Makumbusho ya Taifa maana zina umuhimu wa kipekee.

Ni suala la muda tu kabla hatujapata video za fainali ya CAF Cup 1993. Hilo niachieni mimi bado nalifanyia kazi.

Chanzo: Instagram: @issa_michuzi
 
kwa hii cv ya Simba ni sawa alikwisha chukua kombe la shirikisho..na ndio maana mwamba yupo top 10 za CAF miaka na miaka na mwingine tokea Dunia iumbwe haijawahi kuingia kwenye top 10 za CAF ..mbingu na ardhi
 
Na wewe ni kiboko ulipata wapi video clip hii....nimemuona Godwin Aswile mwenye kiti namba 23.

Nafikiri ni itakuwa clip ya pili kwa ukale baada ya Nigeria vs Taifa stars Afcon 1980

Tuletee clips zaidi...na za Yanga pia
 
Kwa hiyo wala mihogo mibichi na maji ya kandoro (Yanga) bado wanabisha tu kuwa Simba haijafika fainali?
 
Zinaendelea kuibuka video nyingi zaidi za kumbukumbu ya mafanikio ya Simba katika historia ya mpira Tanzania.

Leo nawaletea video ya robo fainali ya CAF Cup 1993 kati ya USM El Harrachi dhidi ya Simba iliyochezwa kule Algeria. Simba ilivuka kigingi hiki na kwenda hadi fainali na kuwa klabu ya kwanza ya Tanzania kufanya hivyo.

View attachment 3328402
Kumbukumbu zote za timu ya Simba inabidi ziwekwe pembeni ya ile Rolls-Royce ya Nyerere pale Makumbusho ya Taifa maana zina umuhimu wa kipekee.

Ni suala la muda tu kabla hatujapata video za fainali ya CAF Cup 1993. Hilo niachieni mimi bado nalifanyia kazi.

Chanzo: Instagram: @issa_michuzi
 
acha kufananisha Simba ya 1993 na hii umbwa koko ya sasa!! acha kabisa...
 
Back
Top Bottom