Exclusive: Picha ya ndege yetu iliyoanguka na Taifa lisilo na shukrani!

Mwanakijiji
nimesoma hii thread mara mbili lakini bado najaribu kujiuliza sababu zilizokusukuma kutumia neno Taifa lisilokuwa na shukrani.
 
Mwanakijiji
nimesoma hii thread mara mbili lakini bado najaribu kujiuliza sababu zilizokusukuma kutumia neno Taifa lisilokuwa na shukrani.

Unakuwa kama humjui mkufunzi part time wa Juche ? . Bila ya extravagant exagerrations story inakuwa hainogi. Hapo hamna distinction kati ya serikali na taifa, sijui wananchi walitakiwa kuandamana nchi nzima kuonyesha masikitiko?
 
Moja ya matatizo makubwa tuliyo nayo nchini kwetu ni hili la watu kutokuwa na integrity.

Watu wanajifanya kwamba wako victims of circumstances, kwamba kuna natural forces zilizo kubwa kuliko wao, kuna mabosi wamewataka wasaini mikataba na hawakuweza kukataa, kuna nidhamu ya kijeshi isiyoruhusu maswali ambayo iliwataka warushe hizi ndege na wasingeweza kukataa.

Guess what? This notion is wrong.

Ni kweli mwanajeshi hatakiwi kukataa amri, lakini si kweli kwamba mwanajeshi mwenye integrity hawezi kujiuzulu kazi yake, even at the risk of being court marshalled, kama anaona analazimishwa kufanya kitu against his will/ sense of integrity.Ndiyo maana hata utetezi wa the Nuremberg trials kwamba "sisi tulikuwa foot soldiers tu, tulipokea maagizo kutoka juu" haiwezi kusimama leo.

Mimi naendelea ku maintain, kwa mtu mwenye ushujaa hasa na integrity ya hali ya juu hawezi kukubali kurusha hizi ndege kwani ni hatari, na kama jeshi halina ndege nyingine ataondoka kwenda kutafuta kazi kwingine, na ikibidi anakuwa hata whistleblower kueleza uchakavu huu wa ndege.

Tunahitaji whistleblowers zaidi, tunahitaji watu wenye integrity zaidi, tunahitaji watu ambao hawaogopi kusema ukweli kwa kufikiri kitumbua kitaingia mchanga au kibarua kitaota nyasi, tunahitaji watu wanaoweza kumwambia hata rais, rais sijui kama nikikuambia ukweli kazi yangu nitakuwa nayo kesho, au sijui kama nitakuwa huru, lakini ukweli ni huu, ndege zetu mbovu na ni hatari kwa wananchi na wanajeshi wetu, na mimi siwezi kurusha ndege hizi.

Hili ni tatizo si katika swala hili tu, hili tatizo partly ndilo linalosababisha mikataba mibovu, watu wanategeana, bosi anaamrisha rushwa kwa kutegea wa chini yake wakubali hivyo yeye asiwe na sole responsibility, wa chini wanakubali kwa kutegea kwamba ni amri ya bosi na hawana jinsi.

Guess what, ukishazaliwa binadamu tu ushakuwa na jinsi.Hata hao wanyama mwitu wengine tumeshindwa kuwa domesticate widely, itakuwa sisi binadamu?

Kusema kwamba hawana jinsi, wamepewa amri kutoka juu, nidhamu ya kijeshi hairuhusu dissent etc ni kutukana intelligence zao.Hawa watu wanarusha ndege, they can't be that stupid.

Kiranga ninakupata vizuri where you are coming from, and believe me ur not very far from where I come from.
 
Mzee Mwenzangu,

Bora wewe umenena,naona sasa hivi kila mtu yupo lwenye kampeni za kutetea kiti chake.

Mjomba sasa hvii anatafuta kura zaidi so vitu kama hivi havioni kabisa.

Nadhani hiki ni kipindi ambacho taifa linatumia pesa nyingi kuliko kipindi chochote kile toka tupate uhuru.

Wamekusikia mkuu..ujumbe mzito sana huu!
 
Raha ya JamiiForums kila kitu ni mada, na hakyanani kinajadilika. Hata nikiweka thread hapa nikasema "habari zenu", zinaweza fika posts 1000, sio za kujibu salamu, bali za kuchambua iyo salamu, wengine watasema habari zetu zinakuhusu nini, wengine wataniita mzalendo, wengine watasema nzuri, wengine watachambua asili ya salamu hii, basi ni raha tu hata kama kuna msiba

kwakuwa protokali zetu zinaruhusu kutumia majina bandia au ya kweli, unaweza kukuta Mwanakijiji ndo huyo huyo Kiranga na ndo huyohuyo Generation-Y

RIP wanajeshi wetu, aidha mliamriwa kurusha ndege ya kizamani (hata kama ni nzima), mbovu, kuukuu, au gulfstream. Muhimu nikuwa mmepoteza uhai wenu mkitumikia kiapo chenu

The code of ethics za jeshi zinasema

Rule no. 1: The general is never wrong
Rule no. 2: Whenever you think the general is wrong, consider rule no. 1

am out!
 
Mwanakijiji
nimesoma hii thread mara mbili lakini bado najaribu kujiuliza sababu zilizokusukuma kutumia neno Taifa lisilokuwa na shukrani.


Wewe unadhani ni neno lipi zuri angelitumia ili kufikisha ujumbe?

Btn the lines:Hivi wana CCM wamerogwa nini?hivi kwa akili gani mtu unaweza kumshabikia Mkwere?
 
Tanzania true heroes wanakufa hawaliliwi, na wengine wanauliwa na kusahaulishwa. Pamoja na kuwa hawa jamaa wametoa maisha yao kwa Tanzania na watanzania subiri uone wataenziwa vipi, kuna mifano mingi tu. Madaktari wangapi wamekufa kwa Ukimwi baada ya kuambukizwa wakiwa kazini, polisi wangapi wamepoteza maisha kwa kuuawa na majambazi kwa mshahara wa shilingi laki moja kwa mwezi, aren't they heroes??. Mafisadi na wengine wanaoifilisi Tanzania ndio wana respect zote na ndio hata wakifa utasikia mpaka kwenye taarifa ya habari wanatangazwa. Nakupongeza Mwanakijiji kwa kuona hilo na kuwathamaini wale wanaostahili kuthaminiwa.
 
kwa nilivyosikiliza wenyeji wakihojiwa.... ilisemekana ile ndege ilikua maeneo ya kwa zaidi ya nusu saa!!! sasa napata shida kuelewa baadhi ya kauli za mwanakijiji

what happended could only be resolved through reliable, technical details, picha na maneno ya kisiasa hayatusaidii kwani ndiyo yaliyotufikisha hapa

Mwanakijiji, kuna details zaidi unazo ambazo ni classified?

Simaanishi kwamba wale si mashujaa la hasha, i also lost a relative naye alikua instructor hapo ngerengere miaka ya themanini..... TUOMBE TU KWAMBA MAMBO YAWE YAMEBADILIKA, NA FAMILIA ZA MAREHEMU ZIFAIDI MATUNZO YA SERIKALI
 
Hiyo ndege nadhani ni Shenyang J-5 ya Kichina ambayo inafanana sana na Mig 17 ya Kirusi..Mwaka gani?... utachoka google hizo ndege kisha mnambie wenyewe ni aibu tupu..inasikitisha kuona bado tuko nyuma kiasi hiki..
 
Hiyo ndege nadhani ni Shenyang J-5 ya Kichina ambayo inafanana sana na Mig 17 ya Kirusi..Mwaka gani?... utachoka google hizo ndege kisha mnambie wenyewe ni aibu tupu..inasikitisha kuona bado tuko nyuma kiasi hiki..

unadhani kuwa tuko nyuma hivyo? la hasha.. sasa hivi tuna Mig 29 (tumenunua mapema in the 2000s); lakini haya ni mojawapo ya gharama za ufisadi... natamani nichambue hili la ulinzi wa mali zetu na kuona jinsi gani tunajaribu kulinda jumba la almasi kwa mishale na mikuki! Huku malango hayana hata komeo!
 
Mkuu, sasa kama tunazo hizo Mig 29, hii ndege ilikuwa angani ili iweje?..Kihsa unajua wazungu huwa hawafichi uwezo wa jeshi la nchi fulani kwa sababu contract za kununua ndege za kivita mara nyingi huwa wazi kwa sababu ya kisheria na malipo..Sioni kabisa mahala wanatupa nguvu ya kununua hizo Mig 29...Na sidhani kama tumezinunua kisiri hali vifaa vingine vya kivita tulokuwa navyo vinaonyeshwa wazi. Au Mig za Kichina? haaa! haaa! haaa!
 
Mkuu, sasa kama tunazo hizo Mig 29, hii ndege ilikuwa angani ili iweje?..Kihsa unajua wazungu huwa hawafichi uwezo wa jeshi la nchi fulani kwa sababu contract za kununua ndege za kivita mara nyingi huwa wazi kwa sababu ya kisheria na malipo..Sioni kabisa mahala wanatupa nguvu ya kununua hizo Mig 29...Na sidhani kama tumezinunua kisiri hali vifaa vingine vya kivita tulokuwa navyo vinaonyeshwa wazi. Au Mig za Kichina? haaa! haaa! haaa!

mzee tunazo sita!
 
Back
Top Bottom