Ex wangu alivyonitesa leo ananililia

Ex wangu alivyonitesa leo ananililia

Billie

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2011
Posts
13,709
Reaction score
23,119
Miaka ya nyuma nilikuwa na msichana wangu mweupe(ugonjwa wangu aisee) Ni msichana ambae nilimpenda sana kwa sababu wenge la mapenzi ndo alinitoa yeye.In short nae alikuwa mzuri sana(according to my eyes) mpaka ikafika point akawa anavuma pale chuoni.

Nakumbuka ilipofika mwaka wa pili mwenzangu akawa na mambo mengi mimi nipo bize na masomo.Ilifika point akawa anafuata na gari kila ijumaa pale chuoni na jamaa fulani wa makamo.

Nikimuuliza mwenzangu anajibu kuwa yule ni uncle wake huwa anampenda sana na pia anafanya kazi pale mlimani city mall hivyo kila ijumaa anamchukua ili aende kwake na mke na watoto.Kwa uzoba wangu ilinibidi nikubali tu japokuwa kuna kitu kilikuwa kinanistua moyoni nikawa nakikemea.

Yule dada kwa kweli aliuwin moyo wangu kwa sababu kila sababu aliyokuwa akiniambia nilikuwa naiubali hata kwa kujilazimisha.

Uncle nilianza kumsuspect kwa sababu alikuwa anamnunulia zawadi nyingi sana including laptop,
na mazaga mazaga akawa ananitenga nikiuliza anakuwa mkali,Niwe tu muwazi mwaka wa pili nilijikuta matokeo yangu ya UE yamekaa vibaya(graph la matokeo likawa limeshuka),marafiki zangu wakawa wanaona ninavyonyanyasika kimapenzi.Ki ukweli alinipenda ila kosa langu kubwa ni kuwa nilikuwa sina hela(mwanafunzi mwenzie).

Lile li uncle likawa lipo bize nae mpaka usiku likawa linampigia simu.Kuna rafiki yangu mmoja ambae tulisoma nae shule ya msingi tumekutana pale chuo akanikalisha chini na kunipa ushauri nikubali kuwa huyu msichana kashatekwa na wajanja coz hata huyo uncle wake kuja kufuatilia kupitia kwa mdogo wake mchumba wangu akaniambia hawana mjomba mwenye jina kama hilo na pia hawana mjomba anaefanya kazi mlimani city.

Nilianza kujifunza kukubali kuwa nimeshatemwa taratibu kwa msaada na usimamizi wa rafiki yangu akaanza kunikeep bize na masomo na mazoezi mpaka ikafika point nikakubali kuwa huyu sio wangu japokuwa kuna wakati alikuwa ananimiss na kujirudi kiuongo uongo ila upendo nikaanza kuuvua taratibu nikajiapiza sitaki mbwa yeyote wa kike aharibu furaha,masomo,moyo na hata afya yangu.

Niliweza kumove on ila niliapa kutafuta pesa kwa juhudi ili nilipize kisasi(japokuwa niliona upuuzi kulipa kisasi).Nilidelete kila kitu kwenye ubongo wangu kinachomhusu yeye nikawekeza nguvu kwenye kutafuta maisha

SABABU YA KUANDIKA:Baada ya kupotezana kwa muda mrefu mwenzangu kumbe ananitafuta kwa muda mrefu sana na kubahatika kunipata kupitia namba ya simu,White ameomba kuonana na mimi bahati mbaya mi nipo mkoa nje ya Dar ikabidi kumuonesha mi mbweha nikamfanyia booking ya Go and return fast jet ili aje huku nilipo tuonane nae nikamuandalia mtu wa kumpokea airport(nina gari yangu Carina TI inafanya service ya Tax) amefikia Hotel fulani kubwa hapa Mkoa nilipo, nimeenda kuonana nae kachoka mbaya ule uzuri wote aliokuwa nao umepungua.

Mbaya zaidi nikatoka nae out mpaka kwenye kitimoto tukapiga story nyingi mi nikamuambia kuwa nimeshaoa hivyo sipo tayari kufanya chochote kibaya nae kwa sababu mi sitaki kuumiza wasio na hatia.

Alilia sana aisee anajutia mazombie aliyonifanyia anatamani movie irudiwe ili asiniumize na anatamani awe mke wangu ila ndo hivyo tena anaishia kulia lia tu hapa.mbaya zaidi nimemkatia tiketi ya go n return ili nimuumize kidogo kwa alichonifanyiaga mpaka ikapelekea mimi kudrop kiufaulu.

Ujumbe wangu:wasichana pendeni watu bila kuangalia kipato chao,kwenye life kuna ups n down tajiri wa leo anaweza akawa masikini wa kesho and vice versa usimjudge mwanaume enzi za utafutaji wake kwa sababu bado anafight hujui atapata nini?
 
Wakat mwingne mshukuru sn uyo white wako, maana alivyokupiga chini ukaanza kufeli baadae ndo ukapata Akili ya kukaza kwenye masomo na ukawa na usongo wa kuzitafuta pesa, might be asingekupiga chini nyie wote wawil akili zenu zingelala leo hii mngekua na maisha duni au ya kawaida sana.
Kikubwa tujifunze kua kwa kila Changamoto tunayokutana nao mbele ya iyo changamoto kuna Fursa kubwa sana
 
Inaonekana lile wenge la mapenzi alailokutoa kalirudisha maana ulivyoandika ni full mawenge mpaka inatia uvivu kusoma.


Ila ujumbe umefika. Hawa viumbe hawa Mungu anawaona, enzi hizo kapuku wanakudharau mbayaaaa mbovu. Ukitusua na yeye kashachezea mikuyenge mpaka kapauka ndio anakuona una maana.

Wallah bora hiyo hela nikanunua malaya kuliko nimpe hata mia yangu.

Kila kuku atakula kwa urefu wa shingo yake.
 
Kuna ka ujumbe nilikapata jana kalinifurahsha na kunichekesha sana, NANUKUU

"Kwa wale waliowapoteza ndugu na Marafiki na wanataman wapate mawasiliano nao, usihangaike we tafta tuu pesaa, watakutafta wenyewe, wapi watapata namb zako? Hilo sio jukumu lako"

Mwisho wa kunukuu

Mwenzangu na mimi kila siku ukipiga unadanganywa kwa kuulizwa
"Sijui nani Mwenzang? Nilibadilisha Simu/laini" 😝😝😝
Mkimaliza hapo hasave keshokutwa unaulizwa tena na ulivyozuzu unajibu.. Nyambafuuu, tafuta hela acha uzwazwa.
 
Ndvyo inavyokuwa. Nilipigwa chini nikiwa chuo kama ww. Akaolewa kwa mbwe mbwe mm nikarudi kitaa niakasota mbaya. Baada ya kutoka kimaisha, anarudi kunitafuta. Bwana alimpiga chini, yuko kwao tu.

usimdharau usie mjua
 
Kuna ka ujumbe nimekapata jana kalinifurahsha na kunichekesha sana, NANUKUU

"Kwa wale waliowapoteza ndugu na Marafiki na wanataman wapate mawasiliano nao, usihangaike we tafta tuu pesaa, watakutafta wenyewe, wapi watapata namb zako? Hilo sio jukumu lako"

Mwisho wa kunukuu
Upo sahihi mkuu kwa sasa pesa ndio kila kitu.
 
Fictitious thread, you just wanted a lesson
 
Akome mi ex wangu alivyogundua sina hela alianza ninyanyasa kupenda out za gharama tukaachana. Mwaka huu tulionana Dar kachoka balaa full kunuka jasho. Tako alilokuwa nalo halipo. Kujirud karudsha mapenzi kakuta nshabeba mke. Yupo zake anapigika.
 
Story hii naomba aione mtu fulani, enzi za deal alinikashfu baada ya kupata mwenye pesa wakati nilizaa nae, kilipoingia chuma madarakani kikazuia wizi wa dawa hospitalini jamaa akamtema. Alirudi kwa risala ndefu ila niliamua kuendelea kutunza mtoto tu hadi leo anaomba tuendelee kama zamani. Siwezi analia kila siku hana hata white dent.
 
Nimeamua kuupumzisha Moyo wangu
Maana siku Nyingi unateseka juu yangu
Kutwa kupelekwa puta na akili yangu
Eti kisa kuuridhisha mwili wangu
Achaaa nikajaribu na kwingine, sio fungu langu pengine
Moyo sukuma damu sio vingine
Mwili usije zusha na vingine, kuanza kuparama na mengine
Moyo sukuma damu sio vingine
Ayeee ayeee ayeee
Sukuma damu sio vingine
Ayeee ayeee ayeee
Moyo usichanganye na vingine
Ayeeee ayeee ayeee
Moyo sukuma damu sio vingine
Ayeee ayeee ayeee
Usichanganye na vingine
Kwenye mapenzi yaliyonifika sio siri yangu
Maana wengi mliiona hali yangu
Kitambaa kiliyachoka machozi yangu
Tabu niliyoipata sio stahili yangu
Aaah haaa sasa mimi ni mtu mwingine, niliyefunzwa na mengi
eeeh
Moyo sukuma damu sio vingine
Tenaa usidanganywe na mwili eeh, umeumbwa kutamani mengi eeh
Usije nikumbusha ya kuleee
Ayeee ayeee ayeee
Sukuma damu sio vingine
Ayeee ayeee ayeee
Moyo usichanganye na vingine
Ayeee ayeee ayeee
Sukuma damu sio vingine
Ayeee ayeee ayeee
Usichanganye na vingine
Usisikize ya mwili yatadanganya danganya moyo
Ayee ayee ayeee
Sukuma damu sio vingine
Ayeee ayeee ayeee
Moyo usichanganye na vingine
Ayeee ayeee ayeee
Moyo sukuma damu sio vingine
Ayeee ayeee ayeee
Usichanganye na vingine
Mo mo Moyo sukuma damu sio vingine
 
Back
Top Bottom