Tuna machozi ya ukweli na machozi ya uongo...Asingelia machozi...Huyo yamemfika makuubwa.
Wenye huruma hawana bahatiHabari Zenu wakubwa. Kuna kitu kimenitokea kama wiki mbili zilizopita nimekuja kwenu japo niondoe mawazo na maswali yangu.
Jambo lililonikuta ni kwamba niliachana na mpenzi ambae tulikaa kwenye mahusiano Kwa muda mrefu kidogo tulishindwa kufikia kwenye ndoa baada ya ndugu zake kuingilia mahusiano yetu na wakaamua kumshaur atafute mwanamke mwingine Kwa kua mimi nilishililia msimamo wa ndoa kabla ya Kuishi pamoja.
Sasa imepita miaka miwili bila mawasiliano na huyo mwanaume lakini cha ajabu ni kua hivi karibuni alinitafuta na alitaka tuonane akidai kuna jambo anataka tuzingumze,kibinadamu nilikubali tukapanga kuonana ilipofika siku ya Miadi nikampigia simu akaniambia nimfate maeneo ya Sinza basi nikafanya kama alivyotaka nilipofika nikakuta ameshabook room akaniomba sana niingie ndani tuzingumze nilikubali japo kishingo upande.
Baada ya kuingia room akaniomba tupeane mapenz nilikataa sana kufanya hicho kitu kwa kua sikua tayar kurudiana nae alizidi kunilazimisha hatimae nilikubali kufanya alivyotaka lakin ajabu ni kua haikupita dakika tatu maumbile yake yakasinyaa kabisa ikawa hawez kufanyae chochote nikaamua kuondoka
Baada ya kama siku tatu akanitafuta tena Ilibid niende maana kichwani nilikua namaswali mengi kuhusu hali niliyom
uona nayo.
Kweli tulikutana na hali ikawa ni ile ile maumbile yanasimama Kwa sekunde kadhaa halafu yanalala kama ya mtoto mdogo nikaamua kumuweka chin nimuulize tatizo limeanza lini hasemi analia tuu namuuliza Kwa mwanamke wake iko hivyo Hataki kusema kitu analia yupo kama kachanganyikiwa.
Sasa maswali najuiliza je huyu mwanaume Kapata ugonjwa gani.
Je ni kweli kuna wanaume hufanyiwa hivyo na wanawake Zao kama limbwata asitembee na wanawake wengine na kama kafanyiwa hivyo iweje anitafute mimi ambae hatujawasiliana Kwa muda mrefu
Akili pia inaniambia huyu jamaa amepata hili tatizo akiwa na huyo mwanamke na sasa ananitafuta Kwa kua kaona hana jipya
Naombeni ushauri nifanyaje nini na huyu mtu maana huruma ya kininadamu imenijia sasa hivi anaongea mwenyewe kama mtu aliechanganyikiwa na hana furaha na maisha
Kahangaika huko kakutana na makubwa ndio anakutafta sasa, na kajirudisha ka kuomba msamaha,na ukute kaathirika kisaikolojiaAisee sijawahi kuona maumbile yaliolala Kwa namna ile kama ya mtoto mdogo kabisaaa
Acha akome kapata alilolitakaHuyu itakua alitembea na mke wa mtu sasa yamemkuta anahangaika
Kahangaika huko kakutana na makubwa ndio anakutafta sasa, na kajirudisha ka kuomba msamaha,na ukute kaathirika kisaikolojia
Wewe dada ukaitwa room ukaingia? Huu ni udhaifu no 1.
Usirudie nasema usirudie kuwa cheap kiasi hiki tena.
Mwanamke ana option moja ya kumrudia x wake Ni pale x anapojirudi akataka muendelee kwa maisha ya kuishi wote kama wanandoa na sio kuja kukulala tu.
Inawezekana hana tatizo lolote
Ni vile tu hana mzuka na wewe
Ameshaathirika kisaikolojia analia yupo kama chizi anaongea mwenyewe
Usiweke sana chumvi nyingi hayo ni mambo ya kawaida hua yanatokea kwa wanaume labda ni wewe tu haijawahi kukutokea. Huyo jamaa mpe muda atarudi kuwa sawa tu itakua kuna mambo yamemsonga akilini. Kumbuka sasa hivi hali ya maisha ni ngumu ongezea na ma corona haya usikute jamaa mambo hayaendi ana mawazo chungu nzima kichwani we umekalia kutafuta mchawi. Kama unampenda endelea kumtia moyo badala ya kushadadia matatizo yake.
Wengi humu wanakushauri ulipize kisasi wanakupotosha.
Kuna mambo mawili hapa kumsaidia tatizo lake kibinadamu kama unavyoweza kumsaidia yeyote tofauti hapa ni kuwa huyo mliwahi kuwa na mahusiano. Pili kuamua kurudiana naye au la. Kama una uwezo wa kumsaidia hata ushauri tu akapona msaidie usiangalie mliachanaje. Jaribu kufikiri unaweza kumchukua ndugu ukamsomesha tangu primary hadi chuo kikuu na asikujue wewe wala watoto wako asiwasaidie lakini hatuachi kusaidia. Akipona sasa sio lazima urudiane naye ingawa pia unaweza kurudiana naye kama utapenda. Hivyo usichanganye issues mbili hizi ambazo ni tofauti.
Huyo jamaa inaweza kuwa alujiunga na CHAPUTA hivyo imemuathiri.
Usifuate ushauri wa kulipiza kisasi, hiyo ni kazi ya Mwenyezi Mungu.
Pa kuanzia muulize kwa upole akueleze ukweli wote tangu mlipoachana kila kitu hata kama alibobea kwenye CHAPUTA ili iwe rahisi kujua uanzie wapi kumsaidia. Ukiujua tu ukweli wote nusu ya tatizo utakuwa umelitatua. Kama hatakueleza ukweli hautaweza kumsaidia hata kama utataka utaishia kupiga ramli tu. Hivyo mueleza black and white kama anataka msaada aeleze ukweli wote.Sijawaza kulipiza kisasi ila nimetaka kujua nimsaidie vipi apone maana mpaka sasa hajajikubali hali yake