EWURA Fanyeni Utafiti kwenye Vituo vya Mafuta, Wananchi tuaibiwa

Pole sana mkuu.

Hayo yapo sana. Mi huwa nahisi wauza nafuta wanazichezea pump kiasi kwamba hata wakaguzi wa vipimo huwa hawang'amui ama wanakula nao maana utakuta ukaguzi wameufanya jana na kuweka stika zao/ wakala wa vipimo lakini bado hakuna mabadiliko.

Ina kera sana hii hali.



Naafikiana 100% na wewe, kuna jambo ambalo serikali hailijui, yawezekana wanatumia mwanya wa viongozi wa mamlaka za juu kutokuwa mafundi, na hao mafundi ndiyo wanaokula na wamiliki wa vituo, haiwezekani mafuta ya shilingi 56000 yakimiminwa kwenye dumu katika kituo kinachouza mafuta kwa bei ya juu yakawa mengi kuliko mafuta ya bei hiyohiyo kwenye kituo kinachouza mafuta kwa bei ya chini, hapa ni dhahiri pump zimechezewa
 
Mimi acha nionekane mshamba tu ila natembea na dumu langu
nikilipa 20 liters naziona ...wengine unakuta inazidi mpka 5,000 then wananiambia ni offer kumbe washaona 20 lots haijafika
 
Nipo mjini Morogoro, siku kadhaa zilizopita nilikwenda kununua petroli kwenye kituo cha mafuta kilichopo opp na stand ya Dodoma, ambapo bei zao kwa lita ni shilingi 2348, mafuta hayo yalikwisha baada ya mizunguko yangu ya kilomita kadhaa na nikapata hofu, jana nikahamia kituo kingine kilichopo na eneo hilohilo, mafuta niliyopata yalinifikisha umbali uleule wa juzi na yakabaki, nikapata wasiwasi kwamba kituo kimoja kinafanya ujanja.

Leo nimekutana na vijana wawili wanaouza mafuta ya kupima kwenye chupa, vijana hao hununua mafuta kwenye vituo hivyo viwili tofauti, leo walipokutana wakawa wanapeana uzoefu kuwa wakinunua mafuta ya shilingi 56000 kwenye kituo kinachouza mafuta kwa bei ya juu wanapata lita 22.29 lakini kwenye kituo kinachouza mafuta kwa bei ya chini wanapata mafuta pungufu zaidi, kitu kinachoashiria kuwa kuna wizi unafanyika.

Kwa scenario hizo mbili, mkasa wa kwangu na wale vijana wawili ninajifunza kuwa EWURA mnatakiwa kufanya ukaguzi wa kushitukiza kubaini ujanja unaofanywa na vituo vya mafuta, nimejifunza pia kuwa wengi wa wahanga wa wizi huu ni wanunuzi wanaoweka mafuta kwenye matanki ya magari moja kwa moja, wenzetu wanaonunua kwenye madumu wanaweza kubaini mchezo huo mchafu kwa urahisi zaidi.

Bila kutaja hivyo vituo hututendei haki na sisi pia. Unaogopa nini kutaja hicho ambacho unadhani kinatuibia? Kuogopa kutaja maana yake watu waendelee kuibiwa.
 
Bila kutaja hivyo vituo hututendei haki na sisi pia. Unaogopa nini kutaja hicho ambacho unadhani kinatuibia? Kuogopa kutaja maana yake watu waendelee kuibiwa.


Mkuu mbona nimetaja vyote viwili, labda rudia kusoma uzi vizuri.
 
Mimi acha nionekane mshamba tu ila natembea na dumu langu
nikilipa 20 liters naziona ...wengine unakuta inazidi mpka 5,000 then wananiambia ni offer kumbe washaona 20 lots haijafika



Mkuu unafanya jambo la maana sana, mimi nakuunga mkono 100%
 
Huu mchezo una mnyororo mrefu kuanzia wauza mafuta pump attendants mmiliki wa kituo hadi hao sijui wewura! Pump zinachezewa na mafundi, mmiliki ana mtu wake huko wewera siku wakipanga hizo safari za kishtukiza mtu wa wewera anampigia mmiliki simu fasta fundi anaitwa wanarekebisha hata wakija kusoma zinatoka lita zilezile za kipimo. Kingine kwenye hizo filling stations kuna pump moja ambayo wanaichezea na hiyo ndo kula ya mwenye pump mwisho wa mwezi pump attendtants wanapewa bonus kama responsibility allowance elfu hamsini maisha yanasonga. Usitarajie wewera kuwakamata kwa kushtukiza ni mpango usio rasmi wameuweka.
 
Huu mchezo una mnyororo mrefu kuanzia wauza mafuta pump attendants mmiliki wa kituo hadi hao sijui wewura! Pump zinachezewa na mafundi, mmiliki ana mtu wake huko wewera siku wakipanga hizo safari za kishtukiza mtu wa wewera anampigia mmiliki simu fasta fundi anaitwa wanarekebisha hata wakija kusoma zinatoka lita zilezile za kipimo. Kingine kwenye hizo filling stations kuna pump moja ambayo wanaichezea na hiyo ndo kula ya mwenye pump mwisho wa mwezi pump attendtants wanapewa bonus kama responsibility allowance elfu hamsini maisha yanasonga. Usitarajie wewera kuwakamata kwa kushtukiza ni mpango usio rasmi wameuweka.


Kwa mantiki hii hakuna haja ya kuwa na mamlaka inayolipa wafanyakazi wakati hakuna kinachofanyika, ni kama kufuga paka ukamfurahia kwa rangi zake wakati hakamati panya au anashirikiana na panya kuharibu nafaka
 
Labda kila kituo kifungwe CCTV camera kwa ajili ya monitoring, na readings zake ziwe makao makuu ya mamlaka husika, na wasomaji wawe tume maalumu ya watu waadilifu waliokula kiapo cha Rais badala ya kuwategemea watumishi wala rushwa
 
Wanabana mita hao
Kituo cha uhakika ni PUMA pekee hapo zamani ilikua BP
Hawanaga uchakachuaji wala kuiba kwenye Pump
 
Pole sana mkuu.

Hayo yapo sana. Mi huwa nahisi wauza nafuta wanazichezea pump kiasi kwamba hata wakaguzi wa vipimo huwa hawang'amui ama wanakula nao maana utakuta ukaguzi wameufanya jana na kuweka stika zao/ wakala wa vipimo lakini bado hakuna mabadiliko.

Ina kera sana hii hali.

wakaguzi wanacheza na wenye vituo. pale kwenye pump kuna ajasti ya kipimo kwa hiyo wakaguzi wanapiga pesa na wahusika hupunguza lita kwenye ajasti pale na kupiga sildi sasa wewe ukija kuweka lita 5 itasoma lita 5 kwenye pump utaridhika lakini mafuta yaliyotoka sio ya lita 5 yanatoka ya lita 4 kwa hiyo utowaji na usomaji unakuwa tofauti mfano chukua gallon ya plastic zile za oil lita 5 ambayo huwa zina alama pembeni zinaonyesha lita 1 2 3 4 mpaka 5. mwambie akupimie lita 5 mafuta baadae utaona iliposimamia. ya pili unaibiwa vipi ? unafika kituo cha mafuta huangalii kwenye unit unamwambia akuwekee mafuta ya elfu 50 na pale kwenye pump unit inasoma sh 15000 sasa kama huangaliii yeye anaanzia na hiyo uliyoikuta elf 15000 anakuwekea uliyosema elf50 hapo utakuwa umeweka mafuta ya elf 35 badala ya elf5. nini kifanyike. unapofika kituo cha mafuta mwambie aiandike pale kwenye pump kiasi unachotaka na ijaze yenyewe ikifika kiwango chako itajikata na hapo hapo risiti inatoa. mimi huwa naweka kituo cha puma ni uhakika na mafuta mazuri nikikosa puma kama nasafiri mikoani basi nitatafuta total hizi kampuni uhakika ila kwanza puma
 
Opposite na sta
Mkuu mbona nimetaja vyote viwili, labda rudia kusoma uzi vizuri.

Opposite na stand ya Dodoma- Ndo jina la sheli?
na hiyo nyingine umesema "kingine kilichopo na eneo hilo hilo"- May be ulitaka kusema jirani na eneo hilo hilo...
Acha woga wewe
 
Opposite na sta


Opposite na stand ya Dodoma- Ndo jina la sheli?
na hiyo nyingine umesema "kingine kilichopo na eneo hilo hilo"- May be ulitaka kusema jirani na eneo hilo hilo...
Acha woga wewe


Opp na stand ya Dodoma ni Lake
 
Back
Top Bottom