EWURA Fanyeni Utafiti kwenye Vituo vya Mafuta, Wananchi tuaibiwa

Faana

JF-Expert Member
Dec 12, 2011
31,281
32,325
Nipo mjini Morogoro, siku kadhaa zilizopita nilikwenda kununua petroli kwenye kituo cha mafuta kilichopo opp na stand ya Dodoma, ambapo bei zao kwa lita ni shilingi 2348, mafuta hayo yalikwisha baada ya mizunguko yangu ya kilomita kadhaa na nikapata hofu, jana nikahamia kituo kingine kilichopo na eneo hilohilo, mafuta niliyopata yalinifikisha umbali uleule wa juzi na yakabaki, nikapata wasiwasi kwamba kituo kimoja kinafanya ujanja.

Leo nimekutana na vijana wawili wanaouza mafuta ya kupima kwenye chupa, vijana hao hununua mafuta kwenye vituo hivyo viwili tofauti, leo walipokutana wakawa wanapeana uzoefu kuwa wakinunua mafuta ya shilingi 56000 kwenye kituo kinachouza mafuta kwa bei ya juu wanapata lita 22.29 lakini kwenye kituo kinachouza mafuta kwa bei ya chini wanapata mafuta pungufu zaidi, kitu kinachoashiria kuwa kuna wizi unafanyika.

Kwa scenario hizo mbili, mkasa wa kwangu na wale vijana wawili ninajifunza kuwa EWURA mnatakiwa kufanya ukaguzi wa kushitukiza kubaini ujanja unaofanywa na vituo vya mafuta, nimejifunza pia kuwa wengi wa wahanga wa wizi huu ni wanunuzi wanaoweka mafuta kwenye matanki ya magari moja kwa moja, wenzetu wanaonunua kwenye madumu wanaweza kubaini mchezo huo mchafu kwa urahisi zaidi.
 
Mkuu ili suala ni kubwa mi nshamuachaga Mungu maana unajaza mafuta lakini unatembea kwa hofu


Tunapigwa vibaya Mkuu, ingekuwa inawezekana pump zote zingeagizwa na mamlaka moja na zifungwe seal kudhibiti ujanjaujanja, wanajifanya wanauza mafuta kwa bei ndogo kumbe wezi wakubwa
 
Nipo mjini Morogoro, siku kadhaa zilizopita nilikwenda kununua petroli kwenye kituo cha mafuta kilichopo opp na stand ya Dodoma, ambapo bei zao kwa lita ni shilingi 2348 kwa lita, mafuta hayo yalikwisha baada ya mizunguko yangu ya kilomita kadhaa na nikapata hofu, jana nikahamia kituo kingine kilichopo na eneo hilohilo, mafuta niliyopata yalinifikisha umbali uleule wa juzi na yakabaki, nikapata wasiwasi kwamba kituo kimoja kinafanya ujanja.

Leo nimekutana na mdau vijana wawili wanaouza mafuta ya kupima kwenye chupa, vijana hao hununua mafuta kwenye vituo hivyo viwili tofauti, leo walipokutana wakawa wanapeana uzoefu kuwa wakinunua mafuta ya shilingi 56000 kwenye kituo kinachouza mafuta kea bei ya juu wanapata lita 22.29 lakini kwenye kituo kinachouza mafuta kwa bei ya chini wanapata mafuta pungufu zaidi, kitu kinachoashiria kuwa kuna wizi unafanyika.

Kwa scenario hizo mbili, mkasa wa kwangu na wale vijana wawili ninajifunza kuwa EWURA mnatakiwa kufanya ukaguzi wa kushitukiza kubaini ujanja unaofanywa na vituo vya mafuta, nimejifunza pia kuwa wengi wa wahanga wa wizi huu ni wanunuzi wanaoweka mafuta kwenye matanki ya magari moja kwa moja, wenzetu wanaonunua kwenye madumu wanaweza kubaini mchezo huo mchafu kwa urahisi zaidi.
EWURA hawawezi kamata huo uwizi kwasababu anaeibiwa ni mteja na mwizi ni muuza mafuta na sio sheli. Wenye magari huibiwa kilaini sana kwasababu hashuki kwenye gari kuangalia kilichoandikwa kwenye pamp. Mfano km umeomba mafuta sh50000, bas muuzaji anakusoma kwanza je ulivyo akiona haushuki kusoma pamp ataandika 30000 shap na kuweka mafuta alafu anafuta tarakimu ili usione. Na atakuambia sogeza gari mbele. Na kwa vile kuna jam utalipa fasta 50000 yake na kuondoka.
 
Swala la uaminifu ni sifuri kwa jamii zetu, hata Dar kuna "sheli" ukithubutu kujaza mafuta imekula kwako. Tunawaza kuiba mda wote...
 
EWURA hawawezi kamata huo uwizi kwasababu anaeibiwa ni mteja na mwizi ni muuza mafuta na sio sheli. Wenye magari huibiwa kilaini sana kwasababu hashuki kwenye gari kuangalia kilichoandikwa kwenye pamp. Mfano km umeomba mafuta sh50000, bas muuzaji anakusoma kwanza je ulivyo akiona haushuki kusoma pamp ataandika 30000 shap na kuweka mafuta alafu anafuta tarakimu ili usione. Na atakuambia sogeza gari mbele. Na kwa vile kuna jam utalipa fasta 50000 yake na kuondoka.


Mkuu, hii kitu bila kufika kwenye eneo husika na kijaribu utaona kama ni uzembe wa mnunuzi lakini kiukweli kuna mbinu zaidi ya ufahamu wa kawaida
 
Kuna wakala wa vipimo. Taasisi hii ipo na inafanya kazi. Kama wanafika hadi mitaani na wanakagua mizani ya akina mangi basi unaweza wapata. Nenda wilayani au Manispaa eneo ulilopo
Binafsi nilidhani EWURA, kwakuwa sijawahi kusikia kitu inaitwa wakala wa vipimo maana hasikiki kabisa na wala hajitangazi ili afikishiwe malalamiko kama haya
 
Kuna wakala wa vipimo. Taasisi hii ipo na inafanya kazi. Kama wanafika hadi mitaani na wanakagua mizani ya akina mangi basi unaweza wapata. Nenda wilayani au Manispaa eneo ulilopo


Nashukuru Mkuu
 
Pole sana mkuu.

Hayo yapo sana. Mi huwa nahisi wauza nafuta wanazichezea pump kiasi kwamba hata wakaguzi wa vipimo huwa hawang'amui ama wanakula nao maana utakuta ukaguzi wameufanya jana na kuweka stika zao/ wakala wa vipimo lakini bado hakuna mabadiliko.

Ina kera sana hii hali.
 
Mbinu mojawapo ni pale unapouziwa mafuta kwa kuynganisha. Utaratibu ni lazima arudishe mkono wa pump mahali pake mpaka receipt ya mteja aliyetangulia itoke. Vinginevyo anakuunganisha na bili iliyopita.
Pole sana mkuu.

Hayo yapo sana. Mi huwa nahisi wauza nafuta wanazichezea pump kiasi kwamba hata wakaguzi wa vipimo huwa hawang'amui ama wanakula nao maana utakuta ukaguzi wameufanya jana na kuweka stika zao/ wakala wa vipimo lakini bado hakuna mabadiliko.

Ina kera sana hii hali.
 
Zipo baadhi ya vituo vya njia kuu kama korogwe ni shida. Kila leo nalazimika kuhama kituo.


Mkuu upo sahihi hata Moshi na njia nzima mpaka kufika Same nako ni taabu, inatakiwa wabunifu watengeneze mfumo wa kusoma umiminishaji wa mfuta kwa wateja centrally kudhibiti wizi
 
Mbinu mojawapo ni pale unapouziwa mafuta kwa kuynganisha. Utaratibu ni lazima arudishe mkono wa pump mahali pake mpaka receipt ya mteja aliyetangulia itoke. Vinginevyo anakuunganisha na bili iliyopita.


Elimu hii ni mpya hata kwangu sikuwa nalifahamu hili, na sidhani kama watu wengi wanafahamu
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom