Evarist Ndikilo, akalia kuti kavu Mwanza.

ntamaholo

JF-Expert Member
Aug 30, 2011
12,906
6,909
Wana Bodi salamuni.

Naomba kuwasilisha kuwa, Mwenyekiti wa Ulinzi na Usalama mkoa wa Mwanza, Mhandisi Evarist Ndikilo, yuko katika wakati mgumu kutokana na yeye kushiriki kikao cha usuluhishi ambacho badala ya kuamua mambo kwa kuzingatia sheria za nchi, alitumia ukuu wake wa mkoa kuamua jambo lililokuwa mbele yake.

Jijini Mwanza, kumefukuta mgogoro wa kidini kati ya WAISLAM na WAKRISTO. Mggogoro huo ulianzia pande za IGOMBE-KAYENZE, ambako mchungaji mmjoa wa kanisa la kipentecoste alichinja ng'ombe kwa ajili ya kitoweo kwa watu waliofika kuhani msiba. Kwa kuwa msiba ni suala la kijamii, linawajumuisha WAKRISTO, WAISLAMU na dini nyingine, waislam walisusia chakula kile kwa kudai kuwa aliyechinja hakua muislam. Na wakapitisha maazimio kuwa, wao watakuwa wanashiriki misiba tu lakini vyakula vya msibani hawatakula kwa kuwa vinaandaliwa na makafiri.

Mchungaji yule alipata misukosuko lakini kwa kuwa hakuna sheria ya kumshitaki, aliachiwa huru huku kukiwa na bifu kati ya waumini wa dini hizi mbili.

Ndipo migogoro mingine imeibuka, na katika juhudi za kuitatua, Mkuu wa Mkoa alijikuta akisahau kutumia katiba ya nchi na sheria zake kwa kutamka mbele ya hadhara iliyokuwepo, kuwa WAISLAM ndio wenye jukum la kuchinja. Tamko hili liliwatifua na sasa wanahamasihsana waweke watu wao kule machinjioni na wafungue bucha waandike kabisa bucha ya mkristo.
 
Wana Bodi salamuni.

Naomba kuwasilisha kuwa, Mwenyekiti wa Ulinzi na Usalama mkoa wa Mwanza,
Mhandisi Evarist Ndikilo, yuko katika wakati mgumu kutokana na yeye
kushiriki kikao cha usuluhishi ambacho badala ya kuamua mambo kwa
kuzingatia sheria za nchi, alitumia ukuu wake wa mkoa kuamua jambo
lililokuwa mbele yake.

Jijini Mwanza, kumefukuta mgogoro wa kidini kati ya WAISLAM na WAKRISTO.
Mggogoro huo ulianzia pande za IGOMBE-KAYENZE, ambako mchungaji mmjoa
wa kanisa la kipentecoste alichinja ng'ombe kwa ajili ya kitoweo kwa
watu waliofika kuhani msiba. Kwa kuwa msiba ni suala la kijamii,
linawajumuisha WAKRISTO, WAISLAMU na dini nyingine, waislam walisusia
chakula kile kwa kudai kuwa aliyechinja hakua muislam. Na wakapitisha
maazimio kuwa, wao watakuwa wanashiriki misiba tu lakini vyakula vya
msibani hawatakula kwa kuwa vinaandaliwa na makafiri.

Mchungaji yule alipata misukosuko lakini kwa kuwa hakuna sheria ya
kumshitaki, aliachiwa huru huku kukiwa na bifu kati ya waumini wa dini
hizi mbili.

Ndipo migogoro mingine imeibuka, na katika juhudi za kuitatua, Mkuu wa
Mkoa alijikuta akisahau kutumia katiba ya nchi na sheria zake kwa
kutamka mbele ya hadhara iliyokuwepo, kuwa WAISLAM ndio wenye jukum la
kuchinja. Tamko hili liliwatifua na sasa wanahamasihsana waweke watu wao
kule machinjioni na wafungue bucha waandike kabisa bucha ya
mkristo.

ntamaholo, kuchamba kwingi...! mbona tangu ukoloni waislamu wamekuwa wakichinja na mkala leo mmeanzisha hili ili mjitenge na waislamu sio? mnajuwa wazi kuwa hata mkichinja hawatakula! hata nchi zenye wakristo wengi eg Kenya mbona wachinjaji na waislamu? nyie mna lenu!
 
Last edited by a moderator:
ntamaholo, kuchamba kwingi...! mbona tangu ukoloni waislamu wamekuwa wakichinja na mkala leo mmeanzisha hili ili mjitenge na waislamu sio? mnajuwa wazi kuwa hata mkichinja hawatakula! hata nchi zenye wakristo wengi eg Kenya mbona wachinjaji na waislamu? nyie mna lenu!

binafsi sioni tatizo klwa muislam kuchinja, lakini tatizo ni pale anapojiona yeye ni kila kitu kwa upande wa vitoeo. Na kwa kuwa waislam wamekuwa walalamishi kwa masuala mbalimbali huku wakristo wakivumilia, wenyewe wanasema sasa wataanza kufuatilia haki zao walizopokonywa na makundi mengine ndani ya jamii.

Waislam wamekuwa wakichinja tangu ukoloni ndio, lakini hakuna mahali popote pale kwenye sheria zetu wamepewa haki hiyo. Na nilichokifanya ni kutoa taarifa tu, na ukitaka kuyajua vema zaidi, fuatilia Kwa Neema FM, 98.2 YA JIJINI MWANZA kila siku 22hrs-23hrs.
 
Back
Top Bottom