MAKOLE
JF-Expert Member
- Feb 5, 2012
- 618
- 280
Gazeti la Mwananchi la leo tarehe 21/11/2012 limechapisha habari kuwa Jumuiya ya Ulaya imeishauri Tanzania Kuboresha Bandari ya Dar es Salaam. Kwa wanaofuatilia habari za nchi ya kenya, BBC wametangaza taarifa ihusuyo mradi mkubwa wa Bandari kubwa kabisa katika ukanda wa Afrika inayojengwa (na tayari ujenzi umekwisha kuanza) katika eneo la Lamu nchini Kenya. Hapa naona Ushauri wa EU kwa Tanzania hautasaidia kwani wakati hiyo bandari ya Lamu haijakamilika tayari wafanyabiashara wengi huitumia bandari ya Mombasa, ikikamilika hiyo ya Lamu, ambayo itakuwa ama ni kubwa au miongoni mwa bandari kubwa hapa Afrika itakuwaje?
source, mwananchi na BBC leo tarehe 21/11/2012
source, mwananchi na BBC leo tarehe 21/11/2012