Eti Watanzania hatuelewi ni kwanini Uingereza wanampa fedha Rais?

Sam Naipenda

Member
Mar 1, 2018
97
720
Sikilizeni watanzania, huu sio wakati wa kutegemea kutetewa na Uingereza.

Leo mchana wengi wetu tumeshangazwa na tulichokiona kutokea Ikulu. Tumemwona waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza Bi Penny Mordaunt alipomtembelea Mh Rais Magufulu na yeye akielezea kwamba amepewe kiasi cha shilingi 307.5B za kitanzania kama msaada wa kuendeleza kazi za serikali yake katika elimu, afya na mapambano dhidi ya rushwa. Hatujachukia kusaidiwa maana tunataka misaada.

Kilichoshangaza wengi ni kuona katika mazingira ya kisiasa tuliyonayo ambayo Mh Rais JIWE na baadhi watendaji wake aliowateua wameamua kuendesha nchi kikatili, wakivunja au kutokufuata sharia, wakikandamiza haki za binadamu, kuminya uhuru wa kujieleza na vyombo vya habari, na wakiharibu misingi mingi tu ya mfumo wa demokrasia, bado taifa kama Uingereza linampa misaada anayojigamba nayo hadharani. Wengi wetu tulitegemea nchi kama Uingereza ambayo ni moja ya nchi zinazoamini katika misingi ya demokraisa duniani kuwa mstari wa mbele katika kukemea, kukaripia, na hata kumwadhibu Mh Rais JIWE kwa yanayoendelea nchini.

Uingereza na mwenzake Marekani wamekua viranja wa demokraisia duniani miaka yote na mara zote ndio wamekua mstari wa mbele kuadhibu viongozi wanaokiuka misingi hiyo. Cha ajabu inaonekana sasa sio tu kwamba wanaachana na ukiranja huo, bali wako tayari kuwapa kiburi viongozi madikteta kama Mh Rais JIWE watawale vizuri. Nini kinaendelea? Ina maana Uingereza haioni kwamba kumpa misaada Mh Rais JIWE ambaye ameonesha wazi kwamba ana kiu, hamu, njaa, na kila aina ya uhitaji wa MISIFA YA KIJINGA ni kumuongezea ujasiri na misifa ya kijinga katika mkakati wake wa kukandamiza wananchi kwa kigezo cha maendeleo? Wanajua vizuri sana wanachokifanya.

Sikiliza mtanzania, kama unafuatili mambo yanavyokwenda duniani utaelewa kwamba nchi zilizokua mstari wa mbele kupigania demokrasia kwa ujasiri kama Uingereza na Marekani, wana matatizo lukuki ndani ya nchi ya nchi zao ambayo ni vipaumbele Zaidi na haviwapi muda wa kujisumbua na nchi wasizo na maslahi mapana nazo. Kivipi?
  • Kule Uingereza wna wakati mgumu sana kutokana na kinachoendelea baada ya kura ya Brexit. Wananchi wake wana hofu kubwa na viongozi wa serikali pamoja na bunge wako bize na maslahi ya nchi yao baada ya kujitoa Jumuiya ya Ulaya na jinsi ambavyo wanaweza kuendelea kufaidika nayo. HAWANA MUDA NA DEMOKRASIA NA HAKI ZA BINADAMU TANZANIA.
  • Uingereza wako bize kutazama "malisho mapya" baada ya kujitoa EU. Wanapambana kujenga mahusiano na mazingira mazuri ya kiuchumi na nchi za Jumuiya ya Madola ambazo nasi ni wanachama. Wanajenga mahusiano na nchi yoyote ile watakayoweza kufaidika kiuchumi na kupanua himaya yao ya utawama mamboleo. HAWANA MUDA NA DEMOKRASIA NA HAKI ZA BINADAMU TANZANIA.
  • Waziri mkuu Theresa May hajawahi kukanyaga Afrika tangu achaguliwe. Sina hakika hata kama kuna waziri wake wa mambo ya nje ambaye ndio anamfuata kwa uzito kafanya hivyo. Presha aliyonayo May kwenye nchi yake ni kubwa kupita kiasi na amekua akiongoza baraza la mawaziri lililogawanyika kuhusu kujitoa EU. Kule Bungeni anabanwa na kina Corbyn kupita maelezo. HANA MUDA WA KUFUATILIA NA KUJICHOSHA NA DEKOMRASIA YA TANZANIA.
  • Hali ya uchumi wa Uingereza sio nzuri sana. Ukifuatilia habari zao utaona maisha yanakua magumu, kazi ni tabu, wanakata bajeti kwenye maeneo mengi ya muhim kama afya, elimu, nk. Haya ndio vipaumbele vyao na HAWAWEZI KUTUMIA RASILIMALI ZAO HABA KUFUATILIA DEMOKRASIA NA HAKI ZA BINADAMU TANZANIA.
  • Kwa kuwa wanataka kujenga mahusiano mapya kama mkakati mbadala baada ya kujitoa EU wanaogopa kukosana na mataifa wanayoyawinda hivyo hawawezi kuonesha misimamo migumu kuhusu mambo yao ya ndani. HAWANA MUDA WA KUINGILIA MAMBO YA NDANI YA TANZANIA.
  • Kwa upande wa Marekani, ina janga la uongozi wa Trump ambaye karibu kila asubuhi kuna jipya la kukabiliana nalo. Huyu kama sio mifumo imara wa nchi yake naye angekua na mtindo wa utawala usiotofautiana na Rais JIWE. Hana mpango na demokrasia na anaonesha viashiria vingi vya kuikanyaga hata ndani ya nchi yake. Naye ni mbabe na asiyeogopa kukanyaga haki za binadamu. Kwa tabia zake, kawafanya hata maseneta na wabunge wa bunge la wawakilishi kua na mambo mengi ya nchi yao kuliko kujishughulisha demokrasia. Majuzi tumesoma kwamba tangu Trump aingine madarakani hajateua balozi wa kuja Tanzania na aliyepo anakaimu tu. Hii inatosha kuonesha kwamba hana mpango na maslahi yetu na huenda hata hajui jina la Rais JIWE
Sikiliza watanzania, Ukiwatoa hawa wawili nani mwingine kabaki wa kuitisha Tanzania?
  • Nchi za Jumuiya ya Ulaya? Sidhani. Ufaransa na Ujerumani haina maslahi makubwa na Tanzania na ni mara chache wanaongelea maslahi yetu. Kule Afrika Magharibi Ufaransa inaleo madikteka kadhaa hivyo sio tabu kwao.
  • Nchi za EU zilizobaki ni ndogondogo zina matatizo mengi, na zisizo na historia ya kuhangaika na mambo ya nchi zingine "to that extent".
  • Binamu yetu China yeye haamini katika Demokrasia na ndio baba wa MAJIWE Afrika. Anawapenda, anawakumbatia na anawasaidia kufanikisha ujiwe wao. Si umeona anamjengea JIWE na chama chake chuo pale Kibaha?
  • Japan yeye hana shida na maisha ya watu na utawala wao. Mradi munanunua magari yake na bidhaa zao zingine yuko tayari kuwafadhili kwa chochote. Kwani umejiuliza kwa nini Rais JIWE katika mikakati yake ya kubana matumizi hajawahi kugusa eneo la magari ambalo limelalamikiwa tangu Enzi za Mkapa kwamba ni linatupotezea fedha sana? Hujaona wanavyotumia magari ya Japan ovyo hata kumlinda Mwita Mwikabe? Hagusi magari maana hataki kuigusa Japan.
  • Waarabu wao wala hawajui demokrasia nini ili mradi kuna halua mezani. Maisha yao yote wanatawaliwa na familia za kifalme na jambo lolote lisilogusa dini yao hawana habari nao.
  • Nchi jirani? Tunajua sote kwamba zinaongozwa na MAJIWE pia.
Sikiliza watanznaia, Mange Kimambi alitumia muda mwingi sana kutuelewesha na kutushawishi kwamba hakuna wa kupigania haki na demokrasia yetu kutoa sisi wenyewe. Baadhi yetu serikali tulimwelewa sana na tulitegemea watanzania waitikie nasi tusaidie "kutokea jikoni". Pamoja na kasoro zake, yule dada alikua na hoja za msingi sana katika hili. Ni kweli hatuna wa kupigania demokrasia yetu isipokua sisi wenyewe. Hakuna kiongozi mstaafu wa CCM atatusemea na wanamuogopa Rais JIWE kuliko maelezo. Si tuuliwaona akina Mwinyi, Msekwa na Warioba walivyokua wanaongea kwa kutetemeka JIWE alipowaita wamshauri? JK yeye anakula bata duniani na mambo yake na familia yake ni safi. Hata watanzania wakichwapwa viboko wote anajua yeye na familia yake wako salama, wanalindwa, wanakula posho na mke kahongwa ubunge. Hutamsikia.

Sikiliza watanzani, Rais JIWE sio mjinga. Anajua kabisa kwa sasa hakuna mtu atamtisha maana viranja wako kimya. Anajua Kiranja Uingereza anamhitaji yeye kuliko yeye anavyowahitaji. Kwani hatujaona wasemaji wake kama kina Kabuni na yeye wenyewe wakijisifu kwamba nchi za nje wanatambua kazi anayofanya na kumsifu kuliko sisi watanzania? Au hatuelewi hiyo kauli inamaanisha nini? Rais JIWE anajua itachukua muda mrefu sana hadi atishiwe na mtu yoyote musishangae muda sio mrefu ataitoa Tanzania katika mahakama ya The Hague.

Sikilizeni watanzania, Tusishangae Uingereza kumsaidia Rais JIWE. Tena tusishangae tukiona wanamsifia hadharani. Wanafanya hivyo kutetea maslahi yao na unafuuu wa watu wao kiuchumi. Wana mengi ya kuvuna hapa kwetu na hivi vibilioni walivyotoa ni chenchi tu. Kupiga kelele kwetu hakuwagusi na haiwahusu. Sisi ndio tunayaelewa machungu yetu. Tunaelewa shida zetu. Tunaelewa maumivu tuliyonayo. NA SISI NDIO WA KUJITAFUTIA TIBA WENYEWE.

Mtumishi wa Umma
 
Ukitaka kumuchinja nyani usimwangalie usoni maana utamuonea huruma,Wapiga madeal siku zenu zimekwisha,mlizoea Raid Jpm yupo sawa, Ili tuendelee tuna hitaji vitu vinne,1watu,2siasa safi,3ardhi,4Uongozi bora ! Vyote vipo Aliselema Alija Selena selema na hatudanganyiki wacha muisome namba Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Africa amen !
 
Mkuu UK kazi za kumwaga, karibuni walizuiya watu 2000, ambao wanatoka nje ya ulaya kuja ki kazi, waziri wa mambo ya Ndani amesema lazima wachukue wa fanya kazi wa ndani na ku recruit.

Ebwana nchi hii ina kazi za kumwaga sasa hivi, mi kwa siku napata call moja tofauti kwa kazi.

Na nilipo ajiriwa wanahitaji watu wa kazi, full training provide, hakuna wenye skills inabidi atakae patikana unachukuliwa.

Ukija hoja kuwa wako busy na brexit sawa, nakubaliana na wewe, hata mimi nilishangaa sana kuona kupewa hicho kipipa cha fedha.
 
Sasa unapendekeza kipi? Zirudishwe? Azikatae? Nadhani zitasaidia maeneo lengwa. Anaheshimika.
 
Uingereza wametoa ela ziwasaidie watanzania.Wewe unapinga uingereza kutoa ela kwa ajili ya kusaidia watanzania,wakati huo huo mnataka watanzania hao hao mnaotamani wasisaidiwe na muingereza mnataka wawapigie kura ili ikibidi baadae muweze kuongoza nchi hii nyie ndo maana mliitwa NYUMBU.Mpo hapa huru mnabwabwaja pumba zenu ila mnadai hakuna demokrasia?,mnamezeshwa upumbavu na wanasiasa badala ya kushinikiza maendeleo mnabaki kushinikiza demokrasia??.. Ipi?,ya kutukana kumuita raisi Jiwe?,Hamna akili kabisa.
 
Uingereza wametoa ela ziwasaidie watanzania.Wewe unapinga uingereza kutoa ela kwa ajili ya kusaidia watanzania,wakati huo huo mnataka watanzania hao hao mnaotamani wasisaidiwe na muingereza mnataka wawapigie kura ili ikibidi baadae muweze kuongoza nchi hii nyie ndo maana mliitwa NYUMBU.Mpo hapa huru mnabwabwaja pumba zenu ila mnadai hakuna demokrasia?,mnamezeshwa upumbavu na wanasiasa badala ya kushinikiza maendeleo mnabaki kushinikiza demokrasia??.. Ipi?,ya kutukana kumuita raisi Jiwe?,Hamna akili kabisa.
2.5 T ziko wapi kwanza, nyie vibaka unafikiri zitafika kwa walengwa, si mtazitumia kuhongana.
 
Hivi Uingereza ilitoa fedha kuijenga shule inayomilikiwa na CCM na kuacha kuwasaidia wananchi wahusika waliohitaji msaada baada ya nyumba zao kubomoka?
 
CHADEMA mtapata Tabu sanaa..!! So nyie CDM ndio mnajua demokrasia kuliko UK & US? Ambao wameamua kumuunga mkono Rais wetu kwa vitendo, bado mnapinga hata hilo? CDM mmechoka sana aiseee..!! Ur in the worst political shape..!!
 
Mwalimu aliwahi kusema; “TATIZO LA PANYA LINGEISHA KWA PAKA KUFUNGWA KENGELE, lakini hakuna panya wa kujitolea kumfunga paka kengele. Na PANYA watakua WAPUMPAVU sana kwa kufikiri panya WATAJIFUNGA AU KUFUNGANA KENGELE”
 
Sikilizeni watanzania, huu sio wakati wa kutegemea kutetewa na Uingereza.

Leo mchana wengi wetu tumeshangazwa na tulichokiona kutokea Ikulu. Tumemwona waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza Bi Penny Mordaunt alipomtembelea Mh Rais Magufulu na yeye akielezea kwamba amepewe kiasi cha shilingi 307.5B za kitanzania kama msaada wa kuendeleza kazi za serikali yake katika elimu, afya na mapambano dhidi ya rushwa. Hatujachukia kusaidiwa maana tunataka misaada.

Kilichoshangaza wengi ni kuona katika mazingira ya kisiasa tuliyonayo ambayo Mh Rais JIWE na baadhi watendaji wake aliowateua wameamua kuendesha nchi kikatili, wakivunja au kutokufuata sharia, wakikandamiza haki za binadamu, kuminya uhuru wa kujieleza na vyombo vya habari, na wakiharibu misingi mingi tu ya mfumo wa demokrasia, bado taifa kama Uingereza linampa misaada anayojigamba nayo hadharani. Wengi wetu tulitegemea nchi kama Uingereza ambayo ni moja ya nchi zinazoamini katika misingi ya demokraisa duniani kuwa mstari wa mbele katika kukemea, kukaripia, na hata kumwadhibu Mh Rais JIWE kwa yanayoendelea nchini.

Uingereza na mwenzake Marekani wamekua viranja wa demokraisia duniani miaka yote na mara zote ndio wamekua mstari wa mbele kuadhibu viongozi wanaokiuka misingi hiyo. Cha ajabu inaonekana sasa sio tu kwamba wanaachana na ukiranja huo, bali wako tayari kuwapa kiburi viongozi madikteta kama Mh Rais JIWE watawale vizuri. Nini kinaendelea? Ina maana Uingereza haioni kwamba kumpa misaada Mh Rais JIWE ambaye ameonesha wazi kwamba ana kiu, hamu, njaa, na kila aina ya uhitaji wa MISIFA YA KIJINGA ni kumuongezea ujasiri na misifa ya kijinga katika mkakati wake wa kukandamiza wananchi kwa kigezo cha maendeleo? Wanajua vizuri sana wanachokifanya.

Sikiliza mtanzania, kama unafuatili mambo yanavyokwenda duniani utaelewa kwamba nchi zilizokua mstari wa mbele kupigania demokrasia kwa ujasiri kama Uingereza na Marekani, wana matatizo lukuki ndani ya nchi ya nchi zao ambayo ni vipaumbele Zaidi na haviwapi muda wa kujisumbua na nchi wasizo na maslahi mapana nazo. Kivipi?
  • Kule Uingereza wna wakati mgumu sana kutokana na kinachoendelea baada ya kura ya Brexit. Wananchi wake wana hofu kubwa na viongozi wa serikali pamoja na bunge wako bize na maslahi ya nchi yao baada ya kujitoa Jumuiya ya Ulaya na jinsi ambavyo wanaweza kuendelea kufaidika nayo. HAWANA MUDA NA DEMOKRASIA NA HAKI ZA BINADAMU TANZANIA.
  • Uingereza wako bize kutazama "malisho mapya" baada ya kujitoa EU. Wanapambana kujenga mahusiano na mazingira mazuri ya kiuchumi na nchi za Jumuiya ya Madola ambazo nasi ni wanachama. Wanajenga mahusiano na nchi yoyote ile watakayoweza kufaidika kiuchumi na kupanua himaya yao ya utawama mamboleo. HAWANA MUDA NA DEMOKRASIA NA HAKI ZA BINADAMU TANZANIA.
  • Waziri mkuu Theresa May hajawahi kukanyaga Afrika tangu achaguliwe. Sina hakika hata kama kuna waziri wake wa mambo ya nje ambaye ndio anamfuata kwa uzito kafanya hivyo. Presha aliyonayo May kwenye nchi yake ni kubwa kupita kiasi na amekua akiongoza baraza la mawaziri lililogawanyika kuhusu kujitoa EU. Kule Bungeni anabanwa na kina Corbyn kupita maelezo. HANA MUDA WA KUFUATILIA NA KUJICHOSHA NA DEKOMRASIA YA TANZANIA.
  • Hali ya uchumi wa Uingereza sio nzuri sana. Ukifuatilia habari zao utaona maisha yanakua magumu, kazi ni tabu, wanakata bajeti kwenye maeneo mengi ya muhim kama afya, elimu, nk. Haya ndio vipaumbele vyao na HAWAWEZI KUTUMIA RASILIMALI ZAO HABA KUFUATILIA DEMOKRASIA NA HAKI ZA BINADAMU TANZANIA.
  • Kwa kuwa wanataka kujenga mahusiano mapya kama mkakati mbadala baada ya kujitoa EU wanaogopa kukosana na mataifa wanayoyawinda hivyo hawawezi kuonesha misimamo migumu kuhusu mambo yao ya ndani. HAWANA MUDA WA KUINGILIA MAMBO YA NDANI YA TANZANIA.
  • Kwa upande wa Marekani, ina janga la uongozi wa Trump ambaye karibu kila asubuhi kuna jipya la kukabiliana nalo. Huyu kama sio mifumo imara wa nchi yake naye angekua na mtindo wa utawala usiotofautiana na Rais JIWE. Hana mpango na demokrasia na anaonesha viashiria vingi vya kuikanyaga hata ndani ya nchi yake. Naye ni mbabe na asiyeogopa kukanyaga haki za binadamu. Kwa tabia zake, kawafanya hata maseneta na wabunge wa bunge la wawakilishi kua na mambo mengi ya nchi yao kuliko kujishughulisha demokrasia. Majuzi tumesoma kwamba tangu Trump aingine madarakani hajateua balozi wa kuja Tanzania na aliyepo anakaimu tu. Hii inatosha kuonesha kwamba hana mpango na maslahi yetu na huenda hata hajui jina la Rais JIWE
Sikiliza watanzania, Ukiwatoa hawa wawili nani mwingine kabaki wa kuitisha Tanzania?
  • Nchi za Jumuiya ya Ulaya? Sidhani. Ufaransa na Ujerumani haina maslahi makubwa na Tanzania na ni mara chache wanaongelea maslahi yetu. Kule Afrika Magharibi Ufaransa inaleo madikteka kadhaa hivyo sio tabu kwao.
  • Nchi za EU zilizobaki ni ndogondogo zina matatizo mengi, na zisizo na historia ya kuhangaika na mambo ya nchi zingine "to that extent".
  • Binamu yetu China yeye haamini katika Demokrasia na ndio baba wa MAJIWE Afrika. Anawapenda, anawakumbatia na anawasaidia kufanikisha ujiwe wao. Si umeona anamjengea JIWE na chama chake chuo pale Kibaha?
  • Japan yeye hana shida na maisha ya watu na utawala wao. Mradi munanunua magari yake na bidhaa zao zingine yuko tayari kuwafadhili kwa chochote. Kwani umejiuliza kwa nini Rais JIWE katika mikakati yake ya kubana matumizi hajawahi kugusa eneo la magari ambalo limelalamikiwa tangu Enzi za Mkapa kwamba ni linatupotezea fedha sana? Hujaona wanavyotumia magari ya Japan ovyo hata kumlinda Mwita Mwikabe? Hagusi magari maana hataki kuigusa Japan.
  • Waarabu wao wala hawajui demokrasia nini ili mradi kuna halua mezani. Maisha yao yote wanatawaliwa na familia za kifalme na jambo lolote lisilogusa dini yao hawana habari nao.
  • Nchi jirani? Tunajua sote kwamba zinaongozwa na MAJIWE pia.
Sikiliza watanznaia, Mange Kimambi alitumia muda mwingi sana kutuelewesha na kutushawishi kwamba hakuna wa kupigania haki na demokrasia yetu kutoa sisi wenyewe. Baadhi yetu serikali tulimwelewa sana na tulitegemea watanzania waitikie nasi tusaidie "kutokea jikoni". Pamoja na kasoro zake, yule dada alikua na hoja za msingi sana katika hili. Ni kweli hatuna wa kupigania demokrasia yetu isipokua sisi wenyewe. Hakuna kiongozi mstaafu wa CCM atatusemea na wanamuogopa Rais JIWE kuliko maelezo. Si tuuliwaona akina Mwinyi, Msekwa na Warioba walivyokua wanaongea kwa kutetemeka JIWE alipowaita wamshauri? JK yeye anakula bata duniani na mambo yake na familia yake ni safi. Hata watanzania wakichwapwa viboko wote anajua yeye na familia yake wako salama, wanalindwa, wanakula posho na mke kahongwa ubunge. Hutamsikia.

Sikiliza watanzani, Rais JIWE sio mjinga. Anajua kabisa kwa sasa hakuna mtu atamtisha maana viranja wako kimya. Anajua Kiranja Uingereza anamhitaji yeye kuliko yeye anavyowahitaji. Kwani hatujaona wasemaji wake kama kina Kabuni na yeye wenyewe wakijisifu kwamba nchi za nje wanatambua kazi anayofanya na kumsifu kuliko sisi watanzania? Au hatuelewi hiyo kauli inamaanisha nini? Rais JIWE anajua itachukua muda mrefu sana hadi atishiwe na mtu yoyote musishangae muda sio mrefu ataitoa Tanzania katika mahakama ya The Hague.

Sikilizeni watanzania, Tusishangae Uingereza kumsaidia Rais JIWE. Tena tusishangae tukiona wanamsifia hadharani. Wanafanya hivyo kutetea maslahi yao na unafuuu wa watu wao kiuchumi. Wana mengi ya kuvuna hapa kwetu na hivi vibilioni walivyotoa ni chenchi tu. Kupiga kelele kwetu hakuwagusi na haiwahusu. Sisi ndio tunayaelewa machungu yetu. Tunaelewa shida zetu. Tunaelewa maumivu tuliyonayo. NA SISI NDIO WA KUJITAFUTIA TIBA WENYEWE.

Mtumishi wa Umma
Eti wewe "Mtumishi wa Umma," Umma upi hasa,wa wapumbavu?Pamoja na kuelimishwa kote lakini bado CDM mmeshindwa kuelewa maana halisi ya democrasia na kumuelewa Magu?Hivi kwa akili zenu mnaona Tanzania hakuna democrasia kweli.Mnadhani democrasia ni uhuru wa manyani.Marekani na Uingereza kwenyewe uhuru wa manyani hakuna.Wenzenu Wamarekani na Waingereza wanaona Tanzania kuna democrasia,ninyi kama mnaona hakuna bakini hapo hapo,sisi tunasonga mbele.
 
Mtajitekenya sana mwishowe mtaelewa nyie ndio wajinga. Rais Magufuli siye wa kwanza na hatakua wa mwisho katika kusimamia mipango wa kuleta maendeleo ya kiuchumi kwanza kabla ya masuala mengine. Anayempinga na kuingilia kuharibu mipango yake ni lazima akubali kuadhibiwa. Uchaguzi uliisha 2015, mwacheni atekeleze Ilani ya acha a choke. Mtaenda kwa wananchi mkamshitaki 2020 kuwa hakutekeleza vipaumbele vilivyofanya wamchague 2015.

Haiwezekani kuendesha Tanzania kama Wazungu wanavyoendesha Nchi zao. Ndiyo maana na wao hawashangai kuona mtu aliyekuwa akituhumiwa kwa rushwa zaidi katika historia ya Tanzania, ndiye aliyeteuliwa na hao wanaotaka demokrasia awe Mgombea wao 2015. Hii inamaanisha CHADEMA walimu-endorse kama aliyefaa awe Rais tangu alipokuwa CCM. Hii aibu haiwezi kutokea Nchi nyingine.

Leo hii, wanaojidai wanapigania demokrasia, hawafanyi Uchaguzi wa kitaifa wa Viongozi wao halafu hao mnataka kuwaaminisha watu kuwa wana moral authority ya kuisimamia Serikali?

Hivi kwani CHADEMA inawakilisha watu au nini? Kama ni watu, mbona hawana ofisi katika maeneo ambayo ndiko asilimia 70% ya Watanzania wanaishi?

Mnataka kukaza shingo watu wenyewe hamna nazoezi. Unajidai kuongelea sijui mambo ya Brexit, kwani ni mwaka wa ngapi, Waingereza wanasumbuka nalo?
 
Mkuu UK kazi za kumwaga, karibuni walizuiya watu 2000, ambao wanatoka nje ya ulaya kuja ki kazi, waziri wa mambo ya Ndani amesema lazima wachukue wa fanya kazi wa ndani na ku recruit.

Ebwana nchi hii ina kazi za kumwaga sasa hivi, mi kwa siku napata call moja tofauti kwa kazi.

Na nilipo ajiriwa wanahitaji watu wa kazi, full training provide, hakuna wenye skills inabidi atakae patikana unachukuliwa.

Ukija hoja kuwa wako busy na brexit sawa, nakubaliana na wewe, hata mimi nilishangaa sana kuona kupewa hicho kipipa cha fedha.
vipi urais wa maalim sefu,anakabidhiwa lini maana kila ukiota unakuja kutuambia mara mambo yameiva,hivi punde halafu unaporea
 
Back
Top Bottom