Eti nimfanyaje huyu?

Eti nimfanyaje huyu?

Hahaaa..mkuu zandar kwanza pole sana.

Ungeangalia kwanza ukaribu wenu, maelewano na mapenzi kati yenu. Swala la kupeleka vitu halafu unahamia bila mipango yoyote kama Ndoa nadhani ni kutafuta mteremko wa maisha.

Halafu wewe ni mwanaume, sioni kama ni busara kwa maamuzi ulochukua ya kuhamia kwa mwanamke bila malengo madhubuti. Inaonekana wewe uliwahi kumsumbua sana na hapo anafanya malipizi tu, kwa binaadam yoyote hawezi kukurupuka na kukufanyia hivo.

Hapo kuna mawili labda ulimtelekeza na mtotot wake, sasa unaona maisha yake yamenyooka ndio unajirejesha. Cha kufanya kua mpole tu, uamuzi wowote wa kukurupuka utakutia matatizoni.

WELL SAID RAFIKI.... MKUU zandar TAFAKARI
 
Kama asingekuwa na mtoto wako hakika hata mi ningekusaidia kuvifuata vitu vyote tena hata ikibidi kwa ugomvi
 
yani ufanye unyama kisa makochi, fridge na tv au kuna mabegi yamejaa hela ulihamia nayo kayazuilia pia?
 
Na kingine ina maana kakufukuza hataki uishi nae tena na kwahiyo mlipotoka kula we ukaenda kulala wapi? na nguo zako je? nazo kazuia?
 
Mkuu haja kukata mikono chamsingi muombe mungu tu akupe uhai vyote ambavyo kajimilikisha utavipata tena kwani mikono unayo ni hayo tu!!
 
Wadau nina mpenzi wangu ambae anasoma chuo kiukweli katumia pesa zangu sana tu mpaka akafikia kunizalia mtoto, sasa pesa zimekata na nyumba niliyopanga nikarudisha nikarudi home kujipanga upya nikiwa nae, kapata pesa akanambia kapanga nyumba kwaiyo nipeleke vitu tuka ishi wote tena.

Chakushangaza ile namaliza kuingiza vitu ndani tunatoka kwenda kula ananambia pale ni kwake na vile vitu nisahau vitakuwa vya mtoto ila nikitaka kumuona mtoto niende muda wowote ila siyo kwetu tena ni kwake na mtoto wadau nimfanyaje huyu kabla sijafanya unyama.

Naomba mawazo yenu kwanza.

Sasa we unataka ufanye unyama gan wakat kakusaidia we mwachie hvo v2 ni kwel vya mtoto kasake tu maisha mengne sahau hvo na ukimwachia bila fujo hataweza kukufuata tena. Afu utakua shujaa sana brother ukiacha liende
Kuwa mjinga siku ipite, alafu kumbka siku hazigandi namaanisha hayo nayo yatapita
 
mwachie tu hivo vitu ...sio issue/ watu wanalipuliwa magorofa yao huko palestina ndo ije kua wewe vitu vya ndani tu.. just forget it..mwanao atatumia
 
ina maana kakufukuza kwamba muachane halaf abaki na vitu vyako au?
 
mi mwanaume akifanyiziwa huwa nafurah sana cjui kwanini!....

Bila shaka nawe ulishatendwa..

..jifunze kusamehe na kusahau.Kuweka kinyongo au chuki moyoni mwako ni sumu itakayokuua mwenyewe kabla ya mbaya au wabaya wako..
 
maadam ana mtoto wako mwachie tu vyombo kitu gani kaka alafu umeongea ur side of the story tu inaonekana kama kuna kitu kibaya ulimfanyia so alikua anataka ku get even na ww probably ulimtelekeza kipindi ana ujauzito wako na alipata tabu sana, usipende mteremko mtoto wa kiume kuhamia kwa mwanamke!!!
 
Umejua leo ndugu,hizo hatarii znawatokea watu kibao,hasa watu kama nyie mnaoshndwa kufkri na kuyachukilia mambo kirahisi,omba Mungu akujalie hekima kutatua tatzo hilo.
 
Utakuwa kuna mahali ulikosea na yeye analipiza. Afu mwanaume unakubalije kwenda kuanza maisha kwa demu wako?

Unajuaje kama amepangishiwa? Tena ni mwanafunzi ambaye kipato chake kinajulikana, wewe eti kapata pesa amesema nikaishi kwake!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom