Eti hii text ina ubaya gani wakuu?

Eti hii text ina ubaya gani wakuu?

tang'ana

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2015
Posts
12,055
Reaction score
16,510
Hello wakuu!
Kuna kesi nimeletewa na couple flani niisuruhishe, nimeshndwa hata nianzie wapi,anyway issue nzima iko hipi,

Kuna jamaa angu ana mchumba ake wanaish nae tayari ingawa hawajafunga ndoa, Sasa huyo mchumba wake ni wale wanawake wenye wivu uchwara na wasiojiamini,

Yaani kila jamaa akitoka kazini lazima simu yake ipekuliwe, Sasa juzi kati jamaa alimtumia text manzi flani ambae ni workmate wake na ujumbe ulikua mfupi tu,kosa alilolifanya ni kumuita yule manzi totoo,

Sasa mchumba wake ameinasa hiyo text na umezuka ugomvi mkubwa sana, Mchumba wa jamaa anaclaim eti huyo aliyeitwa totoo lazima atakua ni mchepuko wa jamaa,

Kwahiyo binti kajinunisha toka majuzi na hatimaye faili la hiyo kesi limetua mezani kwangu, Nimemhoji mshtakiwa kuhusiana na hyo kesi amesema ni kweli alimtumia huyo binti hyo text lakini hakua na nia mbaya.

So wakuu, Nasolve vipi hii ngoma?
 
Naona hao couples wamekosa changamoto za kweli kwenye mahusiano yao,hawana vitu vya kugombania so hata remote control yaweza kuleta ugomvi mkubwa sana.
Kifupi hiyo sio issue kubwa sana ya kuleta ugomvi uamliwe na mtu wa tatu.Very minor issue.
 
Neno la kawaida tu mkuu ila hapo mwanamke anaonesha kuwa yupo makini ndio maana kanuna.

Hapo aombe msamaha tu na kumueleza kwa kina life liendelee.
 
Mpigie namshtakiwa wapili Huyo toto uchukue maelezo yake pia .unaweza kuta mlalamikaji ameshampigia mshukuiwa natayari katoa maelezo tofauti.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawajakua bado! Wakikua na wakikwepa mishale mingi ya mahusiano naamini hawatokusumbua tena!
 
Inawezekana akawa mchepuko kweli... Japo neno la kawaida wenda mshitakiwa anajua alvolitumia alimaanishaje. Who knows...mkuu tang'ana Waachie kesi yao wamalizane wenyewe.
 
Naona hao couples wamekosa changamoto za kweli kwenye mahusiano yao,hawana vitu vya kugombania so hata remote control yaweza kuleta ugomvi mkubwa sana.
Kifupi hiyo sio issue kubwa sana ya kuleta ugomvi uamliwe na mtu wa tatu.Very minor issue.

Mh
 
Huyo hajaolewa ana wivu huo halafu mtu asiyejiamini hivyo ujue ana michepuko yeye
 
Hello wakuu!
Kuna kesi nimeletewa na couple flani niisuruhishe,nimeshndwa hata nianzie wapi,anyway issue nzima iko hipi,kuna jamaa angu ana mchumba ake wanaish nae tayari ingawa hawajafunga ndoa,asa huyo mchumba ake ni wale wanawake wenye wivu uchwara na wasiojiamini,yani kila jamaa akitoka kazini lazima simu yake ipekuliwe,asa juzi kati jamaa alimtumia text manzi flani ambae ni work mate wake,na ujumbe ulikua mfupi tu,kosa alilolifanya ni kumuita yule manzi totoo,sasa mchumba ake ameinasa hyo text na umezuka ugomvi mkubwa sana,mchumba wa jamaa anaclaim eti huyo aliyeitwa totoo lazima atakua ni mchepuko wa jamaa,so binti kajinunisha toka majuzi na hatimae faili la hiyo kesi limetua mezani kwangu,nimemhoji mshtakiwa kuhusiana na hyo kesi amesema ni kweli alimtumia huyo binti hyo text lakini hakua na nia mbaya.
So wakuu,nasolve vipi hii ngoma?
hii mambo ya mwanaume kuita workmate totoo inatoka wapi
 
Huyo bibie hajawa registered bado anatuna hivyo baada ya registration rafiki yako atapangiwa mpaka watu wa kuongea nao
 
Na wewe mtumie text huyo demu wa msela,muite "totoo"....Kesi imeisha
 
Back
Top Bottom