Ethiopia yatangaza hali ya hatari katika jimbo la Kaskazini la Tigaray

Sam Gidori

Senior Member
Sep 7, 2020
165
414
Serikali ya Ethiopia imetangaza hali ya hatari katika jimbo la Kaskazini la Tigaray baada ya Waziri Mkuu wa taifa hilo, Abiy Ahmed kulaumu Serikali ya majimbo inayoongozwa na upinzani kushambulia vikosi vya Jeshi vya serikali.

Taarifa ya Ofisi ya Waziri Mkuu inasema kuwa matukio ya vurugu yanayotekelezwa na Serikali ya Majimbo ya Tigaray inavunja Katiba ya nchi hiyo na kuhatarisha usalama.

Kauli hii ya Abiy inaashiria kuanza kwa shughuli za kijeshi katika eneo hilo la kaskazini, kwa mujibu wa msemaji wake, Billene Seyoum, alipozungumza na Shirika la Habari la Reuters.

Katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter, Abiy aliandika: "Majeshi yetu ya ulinzi yameagizwa kufanya operesheni ya kuliokoa taifa. Mstari wa mwisho umevukwa. Nguvu itatumika kuwalinda watu wetu na taifa letu."

Serikali ya Jimbo la Tigaray ilifanya uchaguzi wake mwezi Septemba, uchaguzi uliohesabiwa kama 'haramu' na Serikali Kuu, huku pande zote mbili zikishutumiana kupanga njama za mashambulizi ya kijeshi dhidi ya mwingine.

Chanzo: Al Jazeera
 
Serikali za majimbo ni Changamoto sana.
Kwa tafsiri nyingine ni sawa na 'kusema kuwapa watu nguvu na uhuru wa kujiendesha na kujiamulia mambo yao ni changamoto sana.

Bora kuendelea kuwateulia tu.'
 
Kwa tafsiri nyingine ni sawa na 'kusema kuwapa watu nguvu na uhuru wa kujiendesha na kujiamulia mambo yao ni changamoto sana.

Bora kuendelea kuwateulia tu.'
Sivyo unavyomaanisha.

Sera yenu imeonekana ni ya kikaburu.

Pelekeni Ethiopia
 
Kwa tafsiri nyingine ni sawa na 'kusema kuwapa watu nguvu na uhuru wa kujiendesha na kujiamulia mambo yao ni changamoto sana.

Bora kuendelea kuwateulia tu.'
Kila mfumo unachangamoto zake, huoni hapo serikali ya Jimbo inapishana msimamo na serikali kuu hadi kufikia hatua ya kupeleka jeshi kutuliza mambo.
 
Alafu mbelgiji Lisu anataka atuletee serikali za majimbo Tanzania!!!


Hivyo kabisa
Marekani ina majimbo tena yenye nguvu kubwa, mbona hawana shida? Serikali za majimbo ni moja ya ugatuzi wa mamlaka, hakuna haja ya rais kuteau mpaka wakuu wa shule wakati zoezi hilo linaweza kufanywa na watu wengine tena kwa ufanisi mzuri.
 
Back
Top Bottom