Kama unajua maana ya rushwa ni wazi hawa watu hawakupewa rushwa na kama unalijua kanisa katoliki huwezi kusema limechafuka, najua hayo ndiyo unayotamani yawe hivyo lkn sivyo yalivyo, tulieni mtaona mwisho wa haya mambo.Huyu askofu kilaini amechafua kabisa heshima ya kanisa katoliki, ni mtu mlarushwa
Akilazimishwa kuzirudisha tutamchangia tu, ni askofu wetu. Maaskofu wetu wanaishi ndani ya jamii ya waumini na wanategemezwa na waumini wao, akiwemo huyo James Rugemalila. Askofu wa kikatoliki hana familia binafsi inayoweza kufaidika na chochote anachopewa, familia yake ni sisi waumini, na nina uhakika fedha hizo alizitumia kwa manufaa ya kanisa kwani hana pengine pa kuzipeleka. Akidaiwa tutazichanga kanisani tumpe akarudishe.