VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Rais alishaeleza kwa kirefu na kina sakata lote la Escrow. Pointi kubwa toka kwa Rais ni kuwa pesa za Escrow hazikuwa za umma. Zilikuwa za watu binafsi ambao ni IPTL. Tukasikia na kuelewa. Wapo waliobaki na maswali na majibu. Wapo waliobaki wakishangaa dhahiri au kwa kuhadaa.
Mambo yakapoa kama kiporo cha Profesa Muhongo. Hali ikatulia. Sasa,TAKUKURU wameanza kuwaburuza Mahakamani maafisa mbalimbali wa Serikali. Wanawahusisha moja kwa moja na kashfa ya Escrow. Kwamba,walipokea mlungula toka kwa wanufaika wa Escrow.
Maswali yanamea;majibu yanapotea. Mfano,iweje hongo iwe kwenye fedha halali na binafsi? TAKUKURU mnapasha moto kiporo cha Escrow. Hatutaacha kukila katika njaa ya ufahamu na kusaka ukweli tuliyonayo.
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Mambo yakapoa kama kiporo cha Profesa Muhongo. Hali ikatulia. Sasa,TAKUKURU wameanza kuwaburuza Mahakamani maafisa mbalimbali wa Serikali. Wanawahusisha moja kwa moja na kashfa ya Escrow. Kwamba,walipokea mlungula toka kwa wanufaika wa Escrow.
Maswali yanamea;majibu yanapotea. Mfano,iweje hongo iwe kwenye fedha halali na binafsi? TAKUKURU mnapasha moto kiporo cha Escrow. Hatutaacha kukila katika njaa ya ufahamu na kusaka ukweli tuliyonayo.
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam