Eritrea panatisha, Bora Tanzania

Eritrea panatisha, Bora Tanzania

Wanafanana kwa kiasi kikubwa na wakoloni wao Waethiopia. Ethiopia hairuhusuiwi kwa raia kuwa na akaunti ya $ hata kama mwajiri wake analipa kwa $. Na kwa wageni kama watu wanaofanya kazi balozini wanaruhusiwa kutoa kiasi kidogo tu (nadhani US$300 hivi) tu tena baada ya kuonyesha tiketi ya ndege kuwa una safari ya nje ya nchi. Yaani hao Waeritrea wamechukuwa sheria za Waethiopia waliowatawala kama sisi tulivyochukuwa za Waingereza hata baada ya kupata uhuru wetu. Kama maisha yalivyo magumu Eritrea, ndivyo yalivyo magumu Ethiopia. Kama kulivyo na kampuni moja ya simu Eritrea, hivyo hivyo Ethiopia. Kama Waeritrea wanavyokimbia nchi yao, hivyo hivyo Waethiopia.
Ethiopia ya kale ndo iko mawazoni mwako, waziri mkuu wao kawa mtamu kwa democracy mpaka kapata Nobel prize, chezea wenye roho nzuri wewe
 
Wewe na wenzako hamjui mnachoongea. Eritrea na Ethiopia walianza hivi hivi kama Jiwe anavyo-jimwambafai. Mara hiki kimezuiwa leo, mara kile kimezuiwa kesho. Mwisho wakafika hapo walipo leo. Kama hamna akili ni vizuri kunyamaza na kula ugali wenu kimya kimya na kuwaacha wenye akili walinde uhuru wenu wa kikatiba.
Mambo ya 'UKUTA' marufuku !
 
Mbona hata hapa jiwe anatuburuza apendavyo. Ni kama hapa tu, kinachofanyika mpaka kufikia huko vyombo vya dola hutumika na sana ni kwakupewa mishahara minono, na hawasumbiliwi wala kukaguliwa vyeti fake. Vyombo vya dola huweza kufanya lolote na hutekwa na maneno ya viongozi kwa kujifanya wazalendo, ghiliba hiyo huwaingia vyombo vya dola na hasa ukizingatia mishahara na marupurupu manono wanayopewa hugeuka vipofu wa unyama wote. Kisha huundwa kundi la watu wasiojulikana, hili hufanya ukatili wa kutisha huku vyombo vya dola vikifumbia macho mambo hayo, mfano hapa kwetu. Viongozi wa vyombo vya dola huhongwa vyeo na kuwa upande wa kiongozi kwa lolote mfano hapa kwetu. Chaguzi zote huwa kiini macho, na wanaotangazwa washindi ni wale wanaotakiwa na mtawala ili kumpitishia sheria zake za ukandamizaji, mfano huo pia uko hapa kwetu.

Bunge na mahakama nazo hujikuta katika hali hii ya kutii kila kitu kwani kundi la watu wasiojulikana hutumika kumnyamazisha yoyote anayekuwa kikwazo. Gia inayotumika kupandikiza unyama wote huu ni neno uzalendo. Yoyote asiyemtii mtawala huonwa ni msaliti. Wakati hayo yakiendelea zaidi ya nusu ya wananchi hulishwa propaganda na ghafla nchi nzima hujikita ikimsifia mtawala wa aina hiyo. Mifano ya mambo hayo iko wazi hata hapa nchini.
...mnahangaika !
 
Mkuu usiseme afadhali ya Tanzania wakati,Magufuli ndo anatamani tufike huko, wakati wa kikwete hali haikuwa Kama ilivyo leo.
Endapo Magufuli atang'ang'ania madarakani na sisi Tanzania tutakuwa kama Eritrea pia, kwanza mpango wake ni kuua sekta zote binafsi ,Tazama alivyoiua fast jet ili ATCL iinuke, amezima uhuru wa Habari hata humu JF yale mazito tunayoandika mods wanayafuta kwa hofu ya kukamatwa.
Hao fastjet na precision walikuwa wanahonga watu waiue ATCL
 
Hujiulizi wazungu wachache waliwezaje kutufunga minyororo kwenye ardhi!,...mchawi wa waafrika ni yule anaetufundisha historia ya kwamba tulitawaliwa ...hi ni historia mbaya ambayo hatupaswi kuijua...maana inatufanya tujione waovyo
Ni mindset mbona wwenzetu nao walitawaliwa Leo wako mbali wakikimbizana kiuchumi na waliowatawala.Hali Africa imerudi nyuma baada ya uhuru heri wangewaacha waendelee kutawala
 
Nchi ya kipuuzi Sana hiyo sipati picha wananchi wake wanavyoteseka
mji wao mkuu unaitwa Asmara
 
Mkuu ni warembo kweli ila mila zao za kutoa FGM sijui Kama wameacha

Nilikuwa Asmara mwezi May mwaka huu, mmoja wa mbongo tuliyekuwa naye, akamtania binti mmoja kuwa anataka kumuoa aje naye Dar, ilikuwa shida....binti alifurahi sana na alikuwa tayari kabisa.........wako desperate sana, wanaishi kijamaa. Na cha ajabu, kama umeingia Asmara, huruhusiwi kwenda mji mwingine bila kibali, hata kama walikupa viza.
 
Sijakuelewa mkuu, hata Ulaya maana yake nini? Je, Ujerumani inailalamikia Africa au wajerumani kwa Ujerumani yao?
Si Afrika tu bali hata Ulaya. Mpaka leo Ulaya na hasa Ujerumani inajiuliza swali hilo hilo. "Hivi mtu mmoja anawezaje kuwaburuza mamilioni ya watu atakavyo?"
 
Back
Top Bottom