Epuka Mtego huu Jakaya

yaani hao makuwadi wa serikali hata mkiwaambiwa mambo ya maana wao wanaongea kishabiki tu! Biblia inawaita vipofu wenye macho na viziwi wenye masikio!
 
mkuu samahano, sekta ya afya hapa nchini ilikuwa imara lini na ilianza kudorora lini?
kwa hiyo kama mwenzako hakufanya vizuri wewe ndio unatakiwa uje kuharibu kabisa? Mseven wenzake walifanya vibaya yeye akarekebisha, kagame kutoka nchi yenye mizoga hadi maendeleo, kenya narc wanasonga mbele na uchumi wa kenya haukamatiki. Sisi hadi leo tunasingizia vita vya idi amin. Shida sio mtangulizi wewe uliyepo ungeweza kufanya zaidi.
 
Mkuu samahano, sekta ya afya hapa nchini ilikuwa imara lini na ilianza kudorora lini?
ilianza kudorora muda mrefu sana,since nimejiunga kwenye hii fani, thats why nakwambia tumechoka kuona watu wakifa mikononi mwetu kwa sababu ya ukosefu wa vifaa na dawa, its enough, come what may.
 
acha vitisho kwa mkuu wa nchi, wewe nani bwana!
lak
kuwa baba sio kulala kitanda kimoja na mama kuwa baba ni kutekeleza majukumu ya kifamilia! Kuwa mkuu wa nchi ni kuact kutokana na uhitaji wa nchi lakini kama huyo mkuu wako wa nchi hatimizi majukumu acha ameze vidonge! Kama kila wakati anamuingiza mkenge pinda halafu pinda na yeye haone! Posho mkenge, madactari mkenge, jairo mkenge oooowi! juzijuzi tb joshua (yule mchungaji maarufu wa nigeria) alitabiri kwamba kuna rais mmoja wa afrika ata-rest in peace! Watanzania tunatamani huo utabiri utimie kwetu!
 
Rais hawezi kuwaondoa watendaji wake only kwa sababu madokta wanataka, akishamuondoa Nkya na Mponda watataka amuache na mama Salma Kikwete.

Wakati unaandika haya naamini ulikuwa umelewa, bandika mawazo ukiwa sober.
Salma Kikwete ni Waziri wa wizara gani? Familia; mke na watoto wanahusika vipi na mgomo wa madaktari?
 
Hivi ni nini hasa kinachomfanya Kikwete ashindwe kuwaondoa Nkya na Mponda? Kama ni wazuri sana kwenye utendaji si awahamishie wizara nyingine?

Una hakika sababu za uteuzi utendaji mzuri wa kazi? Yawezekana siyo ndiyo maana anashindwa kuwachukulia hatua stahili nadhani pengine hata kuwahoji hathubutu.
 
Madactari majibu yenu mtayapata kutoka kwa Rais atakapo shuka toka kileleni mwamlima Kilimanjaro.
huyo ndio JK bwana Rais ambae waTanzania wengi mwaka 2005 walimuamini kuliko marais wote, lakini imekuwa kinyume amekuwa Rais mbovu kuliko marais waliotangulia
 
Mtu mwenye akili na ufahamu hawezi kutetea tumbo lake huku akiwa amezungukwa na ndugu jamaa na marafiki wenye shida na wasiojua kesho yao.Tanzania ni yetu wote, maamuzi ya hovyo na dhulma zenu zinaiathiri jamii yote. Wezi wakubwa!!
Damu nzito kuliko maji,wana macho lkn hawaoni ,wanamasikio lkn hawasikii ,ujumbe umeufikisha ndg licha ya vikwazo vingi vya wapita njia
 

wewe acha unazi uliopitiliza, madai ya madaktari yanafanyiwa kazi siku ngapi? Posho za wabunge mbona hazikupitia mchakato wote huo? Au za wabunge zipo na za madaktari hazipo?
 
Jamaa sidhani kama atasikia..ni moja kati ya wabishi.
 

Serikali isiyojali wananchi wake itazembea utekelezaji wa maazimio yake na madaktari na kupelekea kufumuka upya kwa mgomo. tafakari
 
Rais hawezi kuwaondoa watendaji wake only kwa sababu madokta wanataka, akishamuondoa Nkya na Mponda watataka amuache na mama Salma Kikwete.
Mbona unajitia kiherehere!!! Wewe ndio msemaji wa Ikulu?

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…