Enzi Hizo S02

Balantanda

JF-Expert Member
Jul 13, 2008
12,476
4,752
Habari za siku nyingi wakuu wangu...Heri ya mwaka mpya....
Baada ya kipindi kirefu cha kutokuwa hewani leo nimeona tuanze awamu nyingine ya 'Enzi Hizo' ambapo tunapata fursa ya kuzikumbuka nyimbo zilizotamba kipindi cha nyuma,kupitia mashairi ya nyimbo hizo pamoja na kuangalia maisha ya wanamuziki wa Dansi waliotamba enzi hizo hapa nchini kwetu Tanzania,DRC(Zaire),Congo Brazaville na kwingineko barani Afrika,zaidi tunaujadili muziki wa nyumbani Tanzania...Katika bandiko hili pia utajadili matukio/mambo mbalimbali yaliyokuwa yakifanyika kipindi cha nyuma(kuanzia mia ya 90 kurudi nyuma) ambayo kumbukumbu yake ni burudani iliyopitiliza....

Ni matumaini yangu wakuu wangu akina Mzee Mwanakijiji,Baba Desi,Sanda Matuta,Gang Chomba,FMES na wengineo tutashirikiana katika kukumbuka muziki na matukio ya zamani ambayo kwa hakika ni hazina isiyochuja....Kwa kuanzia ninaomba tuanze kumjadili Daktari wa Muziki Tanzania Ramadhani Mtoro Ongala 'Dk.Remmy Ongala' aliyetutoka tarehe 13 Desemba na kuleta kilio kikuu miongoni mwa wapenda muziki wa Tanzania.....
 
Remmy Ongala

Personal Information
Born Ramadhani Mtoro Ongala, 1947, in the Kivu region of Belgian Congo (now Zaire); married, with three children.

Politics: Populist.


Career
Itinerant guitarist and singer, touring throughout Eastern Zaire and Uganda, 1964-78; member of Orchestra Makassy, 1978-81; leader of Orchestre Super Matimila, 1981--; participated in World of Music, Arts, and Dance (WOMAD) tours, 1988-89; released albums on England's Real World label, 1989-90. Has made frequent tours of Africa and Europe, 1988--.
Life's Work
American children dream of becoming pop musicians because of the glamorous lifestyle that accompanies pop stardom in the United States. For Remmy Ongala, who grew up in Zaire and lives in Tanzania, music was a constant, completely woven into his everyday life. Becoming a musician was as natural for him as a career in agriculture would be to somebody who grew up in a remote farming village. In his song "Lolango," Ongala articulated his reasons for being a musician: "What is my work? My work is to sing! I live so I can sing, I eat because I sing. Everything in life is because I sing."
Performing mainly in a country where recording facilities are scarce, copyright laws are nonexistent, and music is played in small clubs rather than gigantic sports arenas, Ongala has managed to gain an international following. Many of his songs deal directly with the subjects of urban poverty, unemployment, and death. Nevertheless, his message of hope for the underdog in the face of oppression seems to strike a chord with listeners of diverse backgrounds. Although he sings primarily in Swahili, the passion with which Ongala presents his case transcends barriers of language.
Ongala was born in 1947, in the Kivu region of eastern Zaire, which at that time was known as Belgian Congo. His family lived at Kindu, not far from the Tanzanian border. Shortly after Remmy was born, they relocated to Kisangani, about 250 miles to the north. In these areas, as in much of Africa, music permeated just about every facet of life, and Ongala was immersed in it from birth. His father was a talented musician, regionally well-known as a hand drum and mbira player. The mbira, a hollowed piece of wood or gourd bearing wooden or metal strips that vibrate when plucked, is one of the variety of instruments Ongala began learning from his father at a very early age.
Gary Stewart, in his book Breakout, retold Ongala's own account of the uncommon circumstances surrounding the musician's birth. According to Stewart, Ongala's mother had been pregnant twice before, and both times the child had died. As a last hope, she turned to one of the local traditional doctors for advice. He told her not to go to the hospital next time she was pregnant; instead, the baby was born in the forest with the help of the healer. He then warned her never to cut the child's hair, a vow that she kept for the remainder of her life.
As a youth, Ongala was ashamed of his shaggy hair. But later, when reggae star Bob Marley's image became visible in Zaire, the locks became a source of pride. Remmy was also born with two front teeth intact, thought to be a sign that he himself could become a healer. Although he elected not to pursue that career path, "The Doctor" did eventually become Ongala's nickname among fans in Zaire and Tanzania.
When Ongala was only six years old, his father died. Since his mother could not pay for school, Ongala was forced to quit. By the early 1960s, Ongala was teaching himself to play guitar. When his mother died in 1964, he became the head of the family, responsible for the care of his younger siblings. With no other job options available, Ongala began eking out a living playing music. His guitar playing improved quickly, and soon he was able to get frequent jobs playing at area hotels. For the next dozen years, he toured throughout eastern Zaire and Uganda, playing guitar and drums with a number of bands from the region, including Succ s Muachana and Grand Mickey Jazz.
While he was teaching himself to play guitar, and as he developed his own style during the early part of his career, Ongala was greatly influenced by the new urban Congo style of music that was becoming popular in the early 1960s. Cuban music was also being played widely in eastern Africa at that time. Ongala cites as his major influences from that period the singing of Joseph Kabasele and the laid-back rumba guitar stylings of an artist known simply as Franco.
In 1978 Ongala was summoned by an uncle to Dar-es-Salaam, the capital of Tanzania, to join Orchestra Makassy, a popular band led by Mzee Makassy, who was also originally from Zaire. While a member of that group, Ongala wrote his first hit song, "Sika Ya Kufa (The Day I Die)," honoring a friend who had passed away. Ongala's tenure with Orchestra Makassy lasted about three years. He then left to join Orchestre Super Matimila, another up-and-coming Tanzanian group.
Matimila, whose name came from that of a small village nearby, became a fixture on the bustling Dar-es-Salaam club music scene, and Ongala quickly emerged as the group's leader. The band had as many as 18 members, although usually only six or eight would appear on stage at any given moment of performance because club gigs in Tanzania can last as long as six hours. The casual atmosphere allowed the musicians to rotate in and out freely, usually including two guitars, a bass, a standard drum kit, other African percussion instruments, and a saxophone. Just about everybody sang.
Over the next decade, Ongala became one of Tanzania's most prolific songwriters. He generally left the love songs to others, concentrating instead on writing lyrics that addressed social concerns. Even after achieving a reasonably comfortable standard of living for himself, Ongala continued to champion the poor in his songs. He dubbed the style of his material ubongo, which roughly means "brain music" in Swahili.
Essentially no recording industry exists in Tanzania, and therefore, no mechanism is in place for the collection of royalties; likewise, musicians' unions and copyright laws are not available. Local musicians are almost completely reliant on live performances for their income, and while the music scene in and around Dar-es-Salaam is certainly vibrant, the competition among bands is fierce. As Matimila gained attention, the group started recording some of its songs for Radio Tanzania, but this did not translate into big money as airplay in the West generally does.
The introduction of Ongala's music to a European audience began in simple fashion. In the late 1980s, Ongala gave a tape of his band to a British friend who was about to return to England. The tape was eventually passed along to members of World of Music, Arts, and Dance (WOMAD), an organization that promotes Third World performers. The people at WOMAD were so impressed by the material that Ongala and company were invited to take part in the 1988 WOMAD tour.
Western audiences appreciated Ongala's danceable music immediately. Back in Tanzania, however, his European debut was not universally praised. One member of the press, Omar Bawazir, was especially harsh. Writing in Uhuru, he criticized the band for performing with "naked and rounded stomachs" rather than in normal Western garb, fueling the Western press's biased ideas about Third World underdevelopment.
Matimila's warm European reception led WOMAD to release a collection of Ongala's best Tanzanian radio recordings from the early 1980s. The resulting album, entitled Nalilia Mwana, featured an array of songs dealing with the politics of poverty. Included were such titles as "Ndumila Kuwila (Don't Speak With Two Mouths)," and "Mnyonge Hana Haki (The Poor Have No Rights)."
Reviews for Ongala's European debuts, both live and recorded, were almost unanimously stellar, leading WOMAD to invite the group along on its 1989 tour as well. Matimila was also invited to record in a well-equipped Western studio for the first time. The resulting product, Songs for the Poor Man, was recorded at British rock star Peter Gabriel's Real World Studios, and released on the WOMAD-affiliated Real World label. Again, the album was packed with songs written from the perspective of the downtrodden.
Songs for the Poor Man included "Kipenda Roho," an anti-racism anthem that proclaims the universality of love. This was a theme especially close to Ongala's heart, since he had married and had had three children with a white Englishwoman by this time. Although most of the songs on the album had somber topics, the music itself was uplifting. With his newfound access to sophisticated recording equipment, Ongala was able to produce a cleaner sound without sacrificing the authenticity of his musical roots.
In 1990, Ongala and Super Matimila released a second British recording on Real World. Again drawing on the traditional soukous and rumba traditions of his homeland, Ongala produced Mambo, another collection of songs about social and political injustice. Mambo translates loosely from Swahili as "things," in the sense of comments or concerns. In an effort to involve his growing international audience with the meanings of his songs rather than just their infectious pulsations, Ongala sang several songs in English on Mambo. Once again, the most prevalent theme found on the album is poverty. Among the song titles on Mambo are "No Money, No Life," and "One World."
Meanwhile, Ongala's popularity at home in Tanzania continued to soar as well, although the element of protest in much of his material did not always endear him to government officials. Ongala created a controversy in 1990 by releasing a song called "Mambo Kwa Socks (Things With Socks)," a reference to Tanzanian slang for condoms. The song was a plea to young African men to help slow the spread of AIDS by practicing safe sex.
In general, musicians are not held in high esteem in Tanzania. Often they are portrayed in the press as vagabonds and drug addicts. Among the common people, however, whose cause his entire body of work celebrates, Remmy Ongala is well on his way to attaining folk-hero status. A bus stop in the Sinza district of Dar-es-Salaam, for example, has been renamed Sinza kwa Remmy. Even as his audience grows to include many who are neither poor nor oppressed, Ongala's message speaks loudest to people who are more accustomed to crowded buses than to comfortable sedans.
Works
Selective Discography

  • Nalilia Mwana, WOMAD, 1988.
  • On Stage with Remmy Ongala, AHADI, 1988.
  • Songs for the Poor Man, Real World, 1989.
  • Mambo, Real World, 1990.
Further Reading
Books

  • Stewart, Gary, Breakout, University of Chicago Press, 1992.
Periodicals
  • Ear, May 1990, p. 49.
  • Folk Roots, June 1990, p. 51.
  • New York Times, April 26, 1992, p. H30.
  • Popular Music, 1989, p. 243.

Maelezo haya ni kwa mujibu wa Anwers.Com na yalitolewa kabla Dk. Remmy hajaaga dunia(hajafa)




 
Kwa upande wa Wikipedia wao wanamzungumzia Dk. Remmy ifuatavyo:

Remmy Ongala (1947 - Desemba 13 2010) alikuwa mwanamuziki nchini Tanzania mwenye asili ya Zaire. Alizaliwa na jina la kiraia la Ramadhani Mtoro Ongala katika jimbo la Kivu la Kongo ya Kibelgiji.

Wasifu

Remmy Ongala pamoja na bendi yake ya Super Matimila, ni mashuhuri sana nchini Tanzania, na wamepiga muziki mara nyingi katika nchi za Ulaya na Marekani. Remmy Ongala kwa asili anatoka Zaire. Akiwa na umri wa miaka tisa mama yake alifariki, hivyo ikimbidi achukue jukumu la kutunza wadogo zake.
Akiwa na umri wa miaka 17, alikuwa muimbaji na mpiga ngoma katika bendi ya vijana ya Bantu Success. Hii haikuwa na maana kwa familia yake, hivyo Remmy ilimbidi atoke katika bendi. Miaka miwili baadaye, alijishughulisha tena na muziki. Alijiunga na vikundi mbalimbali vya bendi za muziki akiwa mpiga gitaa na baadhi yake zilikuwa Micky Jazz ya Zaire na Grand Mike Jazz ya huko Uganda. Mwaka 1978 alihamia Tanzania na kujiunga na bendi ya mjomba wake Ochestre Makassy ya jijini Dar es Salaam.
Mwaka 1981 alijiunga na bendi ya Matimila, ikiwa na wanamuziki 18 na ikimilikiwa na mfanya biashara mmoja. Baadaye alianzisha bendi yake ya Super Matimila na kuendeleza mtindo wa kutumia magitaa 3, besi, ngoma na tarumbeta aina ya saksafoni. Remmy Ongala alipiga muziki wake kwa mtindo wa Soukous, katika maumbile mapya kabisa kwa kutumia asili na jadi ya kitanzania. Akiimba kwa kiswahili, ushairi wake mzuri una tunzi zinazohusu siasa na pia maisha ya mtu wa kawaida. Kwa ajili ya uimbaji na utunzi wake wa kuliwaza, Remmy anaitwa "Dokta" na ni mtu anayejulikana sana katika sehemu za Sinza ambazo ni jirani na anakoishi yeye na mkewe Mwingereza na watoto wao 5 na kasuku mmoja, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.


Albamu Alizotoa


  • 1. Songs for the Poor Man (1989)
  • 2. Mambo (1992)
  • 3. Sema (1995)
  • 4. The Kershaw Sessions (1995)
 
Wakati tukiendelea kujiandaa kuanza kuyapitia mashairi ya baadhi ya nyimbo za Dk.Remmy Ongala hebu tujiburudishe na kitu MESENJA.

Wimbo huu uliimbwa na Maxmillan Bushoke akiwa na Bima Lee Orchestra wana Magnet Tingisha,ni wimbo mzuri sana maana ulikuwa kama jamaa anawahadithia watu stori flani hivi.....

Wee Mesenjaa,hallow Sekretari(naam bosi) Mesenja yuko wapi(sijui bosi)
Mara Mesenja anaitika naaam bosi nilikuwa uani tumbo linaniletea matatizo mimi
Nae bosi anasema nenda Post office kachuke barua za ofisini na za nyumbani,za ofisini leta ofisini na za nyumbani peleka nyumbani

Kama inavyoeleweka kazi ya Mesenja ni kutumwa Posta au ofisi za nje na shughuli nyingine zinazohusu kutumwana kiofisi(rudia tena)

Mesenja kaleta balaa nyumbni kwa Meneja bila kufahamu(Mesenja kaleta balaa nyumbani kwa Meneja bila kufahamu)

Wakati anakwenda Post office anawaza moyoni mzee mie darasa la 3 la mkoloni nyumbani mke wangu na watoto wangu wamelalia ugali wa muhogo na sunga la kuchemsha jana,kutoka Post office kapitia Kariakoo,kaingia mitaaani anaikimbiza mia wakati siku hizi mia imeota matairi Mesenja hajatahamaki ni saa 7 na nusu wakati osisi zinafungwa saa 6 na nusu mchana

Mesenja kaleta balaa nyumbni kwa Meneja bila kufahamu(Mesenja kaleta balaa nyumbani kwa Meneja bila kufahamu)

Kakimbilia ofisini kakuta ofisi imefungwa na mlangoni yupo mlinzi kajaribu kumbembeleza zile barua akakataa akaamua kuzipeleka nyumbani kwa bosi wake alimkuta mkewe bosi na kumpa zile barua za ofisini na za nyumbani,mkewe bosi kapokea zile barua akaamua azitazame zile za ofisini kwa kuwa si desturi barua za ofisini kufika nyumbani katazama kaweka kando,katazama barua nyingine anuani maandishi yamelalia kushoto,hati kama ya kike akaamua aifungue na akakumbana na neno Darling kama kichwa cha habari na baada ya kuisoma akazimia nusu saa maskini

Siri imefichuka siri imefichuka kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu(Siri imefichuka siri imefichuka kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu)

Alipozinduka akamkuta mwanae mdogo amamuegemea analia mama nasikia njaa,alimjibu subiri baba ako aje apike,mimi leo sipiki sipakui,analia akisema mimi Baba Kulwa nimemtendea nini mie jamani eee,haya kamjengea nyumba ya ghorofa na gari kamnunulia huyu Darling jamani

Siri imefichuka siri imefichuka kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu(Siri imefichuka siri imefichuka kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu)

Bosi siku hiyo karudi saa 6 na nusu za usiku kichwani ana moja moto moja baridi,kubisha hodi aanza kushambuliwa na maneno,kalale huko huko kwa hao unaowajengea majumba na kuwanunulia magari,ilibidi bosi abembeleze alipoingia ndani kataka tu kumgusa mkewe kidogo,alipigwa kibao na zogo kubwa likaanza,mara maneno,mara kavutwa koti,mara kachaniwa shati...Mesenja kaleta aibu jama

Siri imefichuka siri imefichuka(imefichukaaa) kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu(Siri imefichuka siri imefichuka kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu) kaleta aibuuuu
 
Sasa turudi kwa Dk. Remmy....kwa kuanzia leo naanza na nyimbo mbili ambazi si za siku nyingi sana,nyimbo hizi ni Nasikitika na Muziki Asili yake wapi
 
Nasikitika


Nasikitika yeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee..............Maisha yamenijia magumu,nashindwa la kusema....mmmmmmmmmmm
Nasikitika eeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee..............Maisha yamenijia magumu,nashindwa la kusema
Nasikitika eeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee..............Maisha yamenijia magumu,nashindwa la kusema

Ningeelewa walimwengu ni wachina,mimi nisingekubali kuzaliwa,nsingekubali kuzaliwa ee,lakini nimedanganyika,wakati nalikuwa mdogo,nalikuwa nabebwa,nalikuwa nabembelezwa,nalikuwa nalishwa ee,sikutegemea kama leo nitakuwa hivi,eeeeeeee...

Ulimwengu uwanja wa mapambano,kila mtu kujitafutia,kula kwa tabu,kuvaa kwa tabu,kila kitu kwa shida....

Ilimwengu umejaa maovu,walimwengu tumezingirwa,magonjwa chungu nzima,hata ukijifanya wewe mlevi wa Gongo jirani yako anawagombanisha mke wako na watoto wako anawapika bila sababu kwa tabu,hata ukijifanya wewe mpenda mabibi mabwana hamsini lakini ujihadhari na Ukimwi utapata ukavu kwa tabu......

Ulimwengu imani imekwisha,imani imekwisha,imani imekwisha,watu wameota mapembe,hata watoto zetu heshima hawana tena,imani imekwisha,imani imekwisha,imani imekwisha....

Ulimwengu hakuna raha,hata ukiwa na mapesa ulimwenguni,porini hawakujui,mnyama hakujui,nyoka hakunujui,hasa mbu hakujui,hata ukiwa mheshimiwa ulimwenguni,majani haikujui,porini haikujui...

Ulimwengu uwanja wa mapambano,kila mtu kujitafutia,kula kwa tabu,kuvaa kwa tabu,kila kitu kwa shida....

Nasikitika eeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee.....


Nasikitika yeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee..............Maisha yamenijia magumu,nashindwa la kusema
Nasikitika eeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee..............Maisha yamenijia magumu,nashindwa la kusema
Nasikitika eeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee..............Maisha yamenijia magumu,nashindwa la kusema........mmmmm........eeeeeeee

Nasikitika eeeee....kula kwa tabu,kuvaa kwa tabu,kila kitu kwa shida.......eeeeeeeeeeeeeeeeeeeee,mmmmmmmmmmmmmmm
 
Muziki Asili yake wapi

Muziki asili yake wapi eeeeee,Muziki ni wa nani eeeeeeeeeeeee,
Muziki hakuna mwenyewe,Muziki ni mwito,
Muziki ni fundisho,Muzi maombolezo kilio
Usinione nikiimba,ukadhani ninayo furaha,kumbe ninayo huzuni moyoni.

Muziki alivyo na nguvu ulimwenguni kote,
Hata makanisani wanaimba kwaya kwa kumuomba Mungu,kumuabudu Mungu,kwa kumsifu Mungu,
Hata kukiwa sherehe za serikali,mbele ya Mwenyekiti kuhutubia,ni Muziki unaanza kuwakusanya watu;
Kumbuka Paulo na Sila waliimba gerezani Mungu amewasikia,
Kumbuka Mussa aliimba Muziki wa aina yake,kuwakomboa wana wa Israel waliopo utumwani katika nchi ya Misri..

Kukiwa na sherehe utaimba nyimbo za furaha,kukiwa na tabu utaimba nyimbo za masikitiko;
Ukifa leo utapelekwa kaburini na nyimbo za maombolezo;
Ni mzuiki pekee ulio na nguvu,utawakusanya wabaya na wazurimsiku ya mwisho Mungu akitoa hukumu.

Muziki sio uhuni,kama muziki ni uhuni kwa nini unanunua kaseti;
Kama muziki ni uhuni kwa nini unaomba nyimbo redioni;
Kama muziki ni uhuni kwa nini kwa nini unanunua rekodi;
Kama muziki ni uhuni kwa nini unacheza muziki weeee;
Kama muziki ni uhuni kwa nini unafanya top ten show...

Kumbuka siku ya mwisho ikifika,kutakuwa mlio mmoja wa parapanda utawakusanya wateule wote,
walioteuliwa katika pembe nne za dunia siku ya mwisho mungu akitoa hukumu,hukumu,hukumu.
Hata kwa Mungu malaika wanaimba oooooooooooooooooooo

Muziki asili yake wapi eeeeee,Muziki ni wa nani eeeeeeeeeeeee,
Muziki hakuna mwenyewe,Muziki ni mwito,
Muziki ni fundisho,Muzi maombolezo kilio
Usinione nikiimba,ukadhani ninayo furaha,kumbe ninayo huzuni moyoni.
 
Nalilia mtoto

Nakulilia Mola wangu weee,
Nakuwaza Mola wangu wee,
Yalonipata makubwa naona balaa,
Wala hamu sina x2

Wenzangu wana watoto,
Mimi sina hata wa dawa eeeh,
Niwatumapo wana wa wenzangu,
Mama zao hunisimanga x2

Nalia nasikitika bahati sina,
Kwa waganga wa kila namna nimefika ni bure tuuuu,
Hospitali za kila namna nimekenda ni bure tuuuu,
Mola nimemuomba na sadaka nimetoa ni bure tuuuu,

Mola, Mola, Molaaa eeeh,
Mola eeeh nataka mtoto,

Mola Mola, Molaa eeh,
Mola eeh, nalilia mtoto

Mtoto angelikuwa ni nguo ningenunua,
Mtoto ni mtoto kwa mama hakui,
Hata angelikuwa kilema au mbaya kama Remmy ni mtoto tu!

Mola Mola, Mola eeeh....
 
Mariamu


ataka yote akosa yote
apita ahangaika asijue la kufanya ... asijue la kufanya
mshika mawili yote yamponyoka
apita akebakeba asijiue la kujitetea
mmmhhh mapenzi yawaka moto
naitika nilikukosea sasa nihurumie
si ninafikiri zaidi kuliko wewe
nakonda kama mnazi kwa mapenzi nilionayo
nilalapo nakuota mchana kutwa sili
moyo wanichechemea mwili damu hukauka
penzii eh ..... mmmh penzi eh x 2

nasumbuka kwako unionavyo moyo wangu
wewe ndio dawa yangu
Maraimu wangu
Tanga mbali
waja leo wondoka leoo
waja leo warudi leo

Mariamu bibi
mwenzenu sina pumuzi kujizuwia siwezi ohhh
mwanaume barabara kazi ya mume kwa mke
neno ya mke chumvi kwa mumewe
neno ya muke kachumbari kwa mumewe
penzi oh penzi likamung'uma he heh heh

likamung'uma hen heh heh .... mmhhhh
mdundiko, mdundiko ........ waaaaaa
mdundiko ...... waaaa
 

Mwanaidi

Nimetokea kumpenda binti Mwanaidi

nimeridhishwa na tabia yake
nikaamua tufunge nae pingu za maisha
urithi ulioacha baba niliutumia
ili kuneemesha ukoo wake
nilianza kuuza mifugo
hatimaye shamba
ili kumtosholeza mahitaji yake ehhh

baada ya miezi michache nikapata barua kutoka kwa Mwanaidi
..... .. kuwa yeye hanitaki tena
tena hawezi kuolewa na mimi

(wote)
mimi najuta eh najuta mama
gharama nilizogharamia
ameona bure
sijui la kufanya .. nasikitika oh
sababu yako ....... Mwanaidi x 3
 
Hamisa

Hamisa eeeeeeee,Hamisa eeeeeeeeeeee
Nimetokea kumpenda mtoto Hamisa,Hamisa mtoto wa kigogo Hmisa,Hamisa umezaliwa Mpwapwa,pia waishi Dodoma,
Kila nikifikiria nikulete Daresalama Hmisa.......lakini naogopa,Dareslama kuna vituko.....Watu tunaoishi nyumba za kupanga Daresalama...

(Remmy) Hodi hodi jamani humu ndani hodiii,
(Binti) kariibu,
(Remmy) Wewe ni mke wa nani kwenye nyumba hii,
(Binti) mimi mke wa fundi koroboi pale muembeni,
(Remmy) yule mwenye anakaa banda la uani huku,
(Binti) mmmmmm!
(Remmy) Mume wako ameenda wapi?
(Binti) Mume wangu ameenda gerezani kutafuta makopo,

(Remmy) Hivi we mtoto unajua mi ni nani?
(Binti) hivi we ndio nani?
(Remmy) Mi ndio baba mwenye nyumba hii!
(Binti) mmmmmm, Shikamooo!
(Remmy) Marahaba marahaba,mpaka nikuambie mi ndio mwenye nyumba ndio unaniamkia? haya mama marahaba!


(Remmy) Hivi we mtoto umetoka wapi
(Binti) mimi nimetoka Dodoma
(Remmy) umetoka Dodoma? we Mgogo?
(Binti)Aka! Mi sio Mgogo mi Mkaguru


(Remmy) Sasa we mtoto!
(Binti) mmmm?
(Remmy) Unajua ukifika Darisalamu ni lazima utuone watu kama sisi utapata kila kitu bure! Au Vipi?
(Binti) basi nitasubiri mume wangu akija nimuambie tumepata chumba cha bure!
(Remmy) Utasubiri mume wako akija umumbie ya kwamba Mzee Chumaulete ametupa chumba cha bure? basi akija fungasheni na ondokeni, Ondokeeni!
(Binti) Baaasiii!
 
Mwanza

Mwanza oooh Mwanza eeeh,
Mwanza mji mzuri eeh,
Mwanza nitarudi Mwanza,
Mwanza nitakuja tena! x2

Mji wa Mwanza umezungukwa na milima ya mawe,
Milima ya alimasi,
Milima ya dhahabu,


Mji wa Mwanza umezungukwa na Lake Victoria,
Lenye maji bariiiidi,
Na samaki watamu wazuri,
Mwanza ooh,

Nalia Mwanza,
Wakazi wa Mwanza ni Wasukuma ooh,
Kabila Wasukuma,
Sukuma waaa!
Sukuma waaa!


Kutoka Mwanza tulielekea Bukoba,
Bukoba tulipokewa vizuri eeh,
Matoke kwa wingi,

Wakazi wa Bukoba wanasema Kihaya,
Mwabonaki waitu,
Mmmmh waitu eeeh


Mwanza oooh Mwanza eeeh

 
Kidogo kidogo

Kidogo kidogo bwana wewe eeeeee
Kidogo kidogo baba
Kidogo kidogo
Pole pole
Pole pole mume wangu wee

Saa nane za usiku bwana wewe watoka wapi?
Saa nane za usiku mume wangu nambieeeee

Kama ni marumba, mbona peke yako?
Kama ni maraha, ulikuwa na nani bwana

Pole pole
Pole pole mume wangu wee

Nikikuulliza ulikuwa wapi Bazo
Nikikuuuliza unatoka wapi mume wangu baba watoto?
Wanijia juu kwa mateke na mangumi(x2)
Haina ujanja hiyo
Haina dawa
Haina Kinga
Haina sindano.....WAFWA
 

Dunia

Yote utakayofanya ukimtendea mwenziox2
ubaya ee utalipwa hapa ulimenguni,
Kwa mungu hatuonani,
Kwa Mungu hatupajui,
Kwa Mungu kuna Giza,
aee dunia, jamani dunia, inasikitisha dunia, wandugu dunia,

Ukinipiga leo kesho utapigwa na wengine,
ukinitukana nawe utatukanwa,
ukilangua jua utakamatwa,
kuna wengine watu hudhulumu wenzio wao,
kwa uongo wao, kwa maneno yao, kwa rushwa zao, kwa vyeo vyao kazini, kwa ujanja wao oo dunia,
jamani dunia, inasikitisha dunia, wandugu dunia,

Anakukopa pesa na anakuahidi nitakulipa siku fulani,
siku ikifika humuoni,
na siku ukimuona anakueleza matatizo ya uongo, matatizo ya uongo, ya uongo,matatizo ya uongo,
kukopa harusi kulipa matanga,
kukopa asali kulipa shubiri

jamani dunia, wandugu dunia,
dunia kwa nini waleta vifoo, dunia kwa nini haupendi walimwengu,
Kwa nini nife x2 dunia,
niache mke wangu,
niache mali yangu,
niache nyumba yangu,
aeee dunia oo ooooooooo,
 
Tembea Ujionee

Natembea popote unapokwenda,
iwe usiku ama mchana mbele yetu kuna mwanga wa maisha,
Natembea popote lakini wajua pa kula pa kulala,
maisha ya mtu tumefautiana na tumezaliwa mahali mbali mbali,

Mtu anaweza kufanana na nduguye sio shangazi wala mjomba,
labda pengine rafiki yake,
mkifanana kwa sura mwendo tofauti,
mkifanana kwa mwendo sura tofauti,
mawazo mbali mbali,
tabia mbali mbali,
mavalio mbali mbali,

Tumefikiria kuimba hivi kutokana na kutembea sehemu mbali mbali,
kutofautisha tabia na vitendo vya huyu vipi na kile vipi,
huyu bwana vipi na yule bibi vipi,
Hii shati vipi na suruwali vipi,
hii soksi vipi na kiatu vipi,

Kila mtu na kila sehemu vinatofautiana,
hauwezi kufananisha Morogoro na Darisalama,
tembea ujionee usingoje kuambiwa,

(chorus ya akina Skassy kasambaula na wenzake)
Tembea ujionee usingoje kuambiwa,
Duniani kuna mengi yote yanakusubiri x2

(Dr Remmy)
Tembea mama tembea bibi ii,
Tembea uone mambo,
tembea ushangae,
tembea upande mabasi,
tembea tembea tembea mama tembea bibi oo x2
oo tembea oo mama,

tembea oo mama
(oo tembea bibi oo)
tembea oo bibi oo
(oo tembea uone mambo)
tembea uone mambo


embea oo mama
 
Kwa hakika Ramadhani Mtoro Ongala alisitahili kuitwa Daktari wa muziki Tanzania.......Shukrani kwa wakuu Ngongo na BabaDesi
 
Wakuu Ngongo,Gang Chomba,Baba Desi ,Mzuzu na wengine naomba kama kuna mwenye mashairi ya nyimbo zifuatazo za Dk.Remmy aniwekee...Kilio cha samaki,Niseme nini,Shida na Carola....Mbarikiwe sana wakuu wangu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom