Enzi hizo je wewe umesha wahi kupitia mchezo huu?

Dah. Kweli dunia imebadilika. Siwaoni watoto wa siku hizi wakihanga ika na vitu kama hivi zao ni tv, game na ngumi.
 
Umenikumbusha mbali kukata maganda ya nyanya na chenga za mchele upo busy kupika
 
Dah! Kitambo sana, hasa kwa sisi tuliokuwa na madada wakubwa kutuzidi,
tulikuwa hatuchezi mbali na ubwabwa wa kwenye vifuu...
 
Umenikumbusha mbali sana. Wavulana wanawinda ndege wasichana tunapika na vikopo vya nyanya au beef tunaenda kwa mangi kudokoa mchele.

Watoto wa siku hizi hawapiki wao ni computer games na facebook
 
Heee hao wanaopuliza wasipoangalia sufuria pindu lol

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
yaani tumekumbuka mbali sana! hawa dot.com ndo maana wengine wakiolewa tunarudishiwa tena kama miezi mitatu hivi ili wajifunze kupika! majanga!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…