kwetumasoko
JF-Expert Member
- Aug 24, 2016
- 866
- 510
Wakuu, naomba tuelimishane suala hili,
Hivi ni haki kwa mke kuingia na kuleta vurugu ndani ya ofisi ambamo mme wake anafanyia kazi?
Sasa, leo nimeshangaa sana. Kuna ofisi moja nimetembelea, nilichokutana nacho ni balaa. Mke kamfuata Bwana ofisini kwake kisha kuleta vurugu kubwa sana akidai amepelekewa taarifa na watu ya kwamba kuna mfanyakazi wa kike ofisini pale ambaye ana uhusiano wa kimapenzi na mme wake.
Alichokifanya ni kumrarua makofi binti huyo ambaye ameelekezwa na kuanza kuongea maneno ya hovyo hovyo kuhusu mume wake na kusababisha kazi za kiofisi na utoaji huduma zisimame kwa muda wa kama nusu saa hivi kutokana na taharuki hiyo.
Nilivyomuona mume alikuwa mpole sana pia hakuthubutu kuongea jambo lolote, na kisha huyo mkewe akaondoka baada ya kuona taarifa imepelekwa Polisi.
Hivi ni haki kwa mke kuingia na kuleta vurugu ndani ya ofisi ambamo mme wake anafanyia kazi?
Sasa, leo nimeshangaa sana. Kuna ofisi moja nimetembelea, nilichokutana nacho ni balaa. Mke kamfuata Bwana ofisini kwake kisha kuleta vurugu kubwa sana akidai amepelekewa taarifa na watu ya kwamba kuna mfanyakazi wa kike ofisini pale ambaye ana uhusiano wa kimapenzi na mme wake.
Alichokifanya ni kumrarua makofi binti huyo ambaye ameelekezwa na kuanza kuongea maneno ya hovyo hovyo kuhusu mume wake na kusababisha kazi za kiofisi na utoaji huduma zisimame kwa muda wa kama nusu saa hivi kutokana na taharuki hiyo.
Nilivyomuona mume alikuwa mpole sana pia hakuthubutu kuongea jambo lolote, na kisha huyo mkewe akaondoka baada ya kuona taarifa imepelekwa Polisi.