Wakati mwingine najisikia hasira lakini na gundua ni ujinga.
Fanya utafiti wa awali kabla ya kupost kitu.
Engine za magari zina bei zake na zinajulikana.
Hivi ukisema unataka engine ya 1 HZ kwa 2.5m uko sawa kweli?
Jiulize ya Rav 4 itauzwa bei gani?
Hata ya wizi huwezi pata.
Mkuu Maringeni!!!..
Huna haja ya kupata hasira Kaka, hili dogo moja tu linakutia hasira Mkuu?!! Mbona kuna mengi ambayo ukitaka kukabiliana nayo kwa namna hii utabaki kitandani unaugulia maumivu ya hasira wala usitoke nje!!!..
Taratibu tu Mkuu, bahati mbaya sana (kama utapenda kuiita hivyo) Mwenyezi Mungu kaijaza dunia hii na viumbe wa kila aina; wafupi, warefu, wanene, wembamba, weupe, weusi n.k, pia uwezo wetu wa kuona, kufikiri, kusikia, kupanga, kuamua n.k hutofautiana pia, hilo linakwenda mbali zaidi hata kufikia namna tunavyoweza pata taarifa (kwa maana ya uwepo wa taarifa husika, teknolojia ya usambazaji, gharama za kuifikia taarifa husika n.k).
Utofauti wetu ndio tunu yetu (na hii inakwenda mbali kabisa mpaka kwenye utofauti wetu wa rangi za ngozi, jinsia, mahali mtu alipotoka, imani zetu, mitizamo na itikadi za kisiasa, tamaduni n.k) na ndio hutufanya tuione dunia hii katika mwanga tofauti kila mmoja wetu, tuna mengi mno yanayotutofautisha kama binadamu tukiyaangalia kwa upande mmoja tu itatuwia vigumu sana kuielewa hii dunia. Hebu tutambue na tushukuru mizania na kani ya uwiano wa uwepo wetu na yote yatokanayo na hilo.
Hongera kwa kuwa na taarifa (kwa kiwango ulichonacho) kuhusu magari na vifaa vyake, kwa bahati mbaya sana Binadamu hatukuwahi wala hatutaweza kuwa sawa kila wakati au wakati wote, ningeshukuru sana kama ungeweza kuweka bandiko la bei za magari yote, kwa miundo yake yote, matoleo yake yote, vifaa vyake vyote kwa hali zake zote ili kukwepa kughafirishwa na mbumbumbu watarajiwa kama mimi.
Kwa sasa ninachojua tu ni kuwa ninahitaji engine ya Landcruiser 1Hz, na pesa niliyonayo kwa minajili ya engine hio ni millioni mbili na nusu (2,500,000/=) pesa za Ki-Tanzania na nina imani kuna mtu mmoja, sehemu flani atakuwa na uhitaji wa pesa hiyo dhidi ya engine hio ninayoitafuta.
Mkuu Maringeni, sitaki kufikiria uwepo wetu na ushiriki wetu enzi za "BARTER TRADE" ya wahenga, Daaaah ingebidi nivae "BODY SHIELD" Kabisa, Daaaaaaah...LOL !!!..
Kuna kabandiko haka kanaweza kushusha hasira zetu pia..
Kwa sasa nikutakie jioni njema sana, na mafanikio katika kuufunga mwaka 2018 na kuelekea 2019.
Jioni njema Mkuu..
¬Mawio !!!...
Kwa hili jibu la kistaarabu jamaa alikuja na hasira zake za umaskini atakuwa msata anakimbilia morogoro
Nimewahi ninua 1HZ kwa ajili ya coaster kwa 1.5M.