Emmanuel Eboue hali mbaya, Mke amfilisi

Na kama Dunia tambara, langu lishatoboka Sina hata pa kulala,Nakesha kwa boka

Hii ni mistari iliyopo katika Wimbo wa SINA wa msanii wa Bongofleva,Harmonize.

Emmanuel Eboue Alicheza katika fainali ya Klabu Bingwa Ulaya 2006, alikusanya mamilioni ya pesa katika miaka 7 aliyocheza katika EPL, hi kwenye nyumba nzuri a kuendesha magari ya kifahari Mambo yamebadilika sasa kwa beki huyo wa zamani wa Arsenal.

Kwa sasa anaishi kwa kuwakimbia watu wa mahakama, muda mwingine analala kwenye sakafu za nyumba za rafiki zake, anasafiri kwa basi na hata pia kufua kwa mikono yakekwa sababu hana mashine ya kufulia Akihojiwa na gazeti la Daily Mirror Eboue,34, amesema kuwa hali hiyo inamfanya mpaka atamani kujiua.

Ninataka Mungu anisaidie." Anasema Eboue, Pekee yeye anaweza kuyaondoa haya mawazo kichwani mwangu Eboue amepoteza utajiri wake wote kutokana na usimamizi mbaya pamoja na kuachana na mke wake ambapo ametengwa mbali na watoto wake Watoto wake wote watatu,hajaonana nao tangu mwezi juni.

01252ce9e015ebfb65fefa5252a21492.jpg


Mtoto wake wa kiume,Mathis anacheza katika Academy ya Arsenal.

Baada ya kushindwa ka vita ya talaka, mahakama iliagiza mali zake zote ziende kwa mkewe, Aurelie ambaye ni raia wa Ubelgiji Pia anataraji kukabidhi kwa mkewe jumba lake la kifahari lililopo Enfield,London, endapo atashindwa kufanya hivyo jaji atasaini kuruhusu madalali waende kumtoa.

Eboue anasema kuwa, sasa hana pesa ya kuwalipa mawakili ili kufattilia mali zake. Nipo ndani ya nyumba lakini ninaogopa.

Kwa sababu sijui muda gani polisi watakuja, Muda mwingine ninazima taa kwa sababu sitaki wajue kama nipo ndani," Alisema Kutokana na kuwa na elimu ndogo,alikuwa anatuma karibia mshahara wote kwa mkewe. Na wakati wowote mkewe alikuwa akimtaka asaini hati (Document) yoyote alikuwa anasaini.

Mipango yake ya kurudi katika EPL iliota mbawa msimu uliopita, alisajiliwa na Sunderland lakini hakucheza hata mechi 1 kufuatia kufungiwa na Fl FA kutokana na kushindwa kumlipa wakala wake wa Zamani

Cc ws14
Ufala wa kushobokea kuoa wazungu umeanza kujionesha.
 
Wachezaji wengi waliofanikiwa huko ulaya ambao wanatokea africa huoa wafrica wenzao wakutoka nchini mwao kima kanu, okocha, eto nk walioa wanawake wa nchini mwao wakijua hata ikitokea mzozo hawezi kukuacha mikono mitupu kama huyu eboue
 
Kutumia public transport sio umaskini nchi za Ulaya hata mawaziri wanapanda subway, basi au wanaenda kazini kwa bike, ni bongo tu ndo umaskini.
 
Hakuna cha mental illness jiulize kwanini hachezi Mpira na haja staafu na hana majeruhi ?

Alisajiliwa na klabu yake mpya uturuki kwenye vipimo alifeli na taarifa za madaktari zinasema wame spot virus na wakaishia hapo hawakutaka kuendelea mbele ila vyombo vya habari za uturuki zikasema Ebou alifeli vipimo sababu alikutwa na HIV mbona hii habari ilikuwa hot news sana September,

Na saizi kwenye hii taarifa ya Ebou kufilisika wanasema hachezi mpira sababu yupo ill na wala sio majeruhi

Yaani Ebou wa miaka 30 na kitu apate mental illness kisa babu kafa acha masihara ww

HIV inamsumbua na anajuta saizi
mbona inaonesha kafungiwa kucheza mpira kwa mzozo na wakala wake!?
 
Si wazungu, wanawake wote hawana huruma na mwanaume yeyote labda awe mtoto wake.Ni vizuri kuishi kwa tahadhari sana na hawa wanawake
Umeandika nilichokua nakifikilia

Hata maandiko matakatifu yameandika tuishi nao kwaakili. no way
 
Wazungu wakike wanahila sana.Hawawapendi waafrika huwa wanaangalia wanakitu gani ndio waolewe nao,sio watu lakini sisi ndio tunamatatizo zaidi,kwa nini hakuoa mmatumbi mwenzake?
 
Huyo hakua Gentleman...alikua mhafidhina wa ndoa,Gentleman mwanamke kwake si kila kitu
 
Ndio uhalisia nakumbuka sijui miezi mingapi imepita ndio ilikuwa habari ya mjini ,alitaka kusajiliwa na klabu yake mpya ila alifeli vipimo sababu ya ugonjwa huo

Na stress akawa anajifungia ndani sana na alijaribu kujiua
Acha uongo eboue alifungiwa kucheza mpira baada ya kusajiliwa na Sunderland mwaka 2016,March.


Inasemekana alimtapeli agent wake... Alifungiwa na Fifa kutokucheza mpira kwa miaka kadhaa na mpaka sasa hana team... Alipewa long term Ban.



Muwe mnafuatilia habari acheni uongo na habari za kwenye kahawa.


Ingia hapa Eboue: Year-long ban like being in prison
 
Acha uongo eboue alifungiwa kucheza mpira baada ya kusajiliwa na Sunderland mwaka 2016,March.


Inasemekana alimtapeli agent wake... Alifungiwa na Fifa kutokucheza mpira kwa miaka kadhaa na mpaka sasa hana team... Alipewa long term Ban.



Muwe mnafuatilia habari acheni uongo na habari za kwenye kahawa.


Ingia hapa Eboue: Year-long ban like being in prison

7557d50734dbcb3b805ba63da7eeddf9.jpg


1212bd5922d5a2d20218d9077f5424b0.jpg


ac2471cf54ef3ec87ea28c30f167dc61.jpg


Mkuu inabidi wewe uwe unafuatilia mambo sababu haupo updated
 
Komenti yako nimecheka sana, jamaa tumuombee kwa mungu , so sad this story, mwanaume unampaje mke umiliki wa mali zote , upoyoyo huo, eti kila kitu unachonunua unaandika jina la mke, inaonekana alikufa kwa mkewe kabisa jamaa
Halafu mbona demu lenyewe baaayaaa
 
Back
Top Bottom