Embu tutafakari kidogo

hii inakuwa kama amnesia au unakuwa hujui hata kutembea, kama kuna dunia, kuna watu yani kila kitu
Yeah lakini je, utakua unawaza nini kichwani? Kwasababu huna kumbukumbu zozote za kale... Wanasema kati ya kitu kinachomfanya mtu asiwe bora ni makelele ya nje ndio maana ukiwa katika hali ya utulivu unaweza kuiona future, kwamfano ukiwa umelala ubongo ukiwa haurecall chochote kwenye past ndio wakati ambao unaweza umaota matukio ambayo baadae yanatokea kwa namna ile ile kama ambavyo uliota.

So ile hoja ya mtu kuwa na pande mbili ndio hapo ambapo naonaga inamake sense pia, ila shida ni kujua upande upi uuongoze upande mwingine.
 
Tunazaliwa bila kujua chochote.

Taarifa zote zinazo ingia kwenye ubongo tunazikuta hapahapa duniani kutoka kwa watangulizi wetu.

Hatuwezi kujua tusivyo vijua ila tuna endelea kupunguza tusivyo vijua kwa utafiti, udadisi na uchunguzi zaidi.
 
Tunazaliwa bila kujua chochote.

Taarifa zote zinazo ingia kwenye ubongo tunazikuta hapahapa duniani kutoka kwa watangulizi wetu.

Hatuwezi kujua tusivyo vijua ila tuna endelea kupunguza tusivyo vijua kwa utafiti, udadisi na uchunguzi zaidi.
Hatari... Watu wa kwanza waliwezaje kuanzisha hizi taratibu? Ni kwamba wao walikua bora kuliko sisi au na wao walikuta baadhi ya info tayari zipo.
 
Duh! Sijawahi kufikiria hii kitu kabisa, nawaza sijui itakuwa ni mbaya au amani kwako
 
Mazingira yenyewe yapo tu.

Wala hayalazimishi mtu kufanya uchunguzi.

Ni sisi binadamu tu, tulikuwa na kiu ya kuchunguza Mazingira.

Ndio maana watu walifanya tafiti na udadisi.
Hakuna utafiti uliofanyika bila sababu, so kwanza mazingira yatakupatia sababu au kukuingiza kwenye mfumo utakaopelekea ufanye utafiti.

Kama ni ugonjwa utaumwa kwanza ili ujue kumbe upo then baada ya hapo ndio utafiti unafuata.

So ni kama mazingira yanaamua ya kwamba now hili linapaswa lijulikane coz ili iwe possible yanakupa sababu za wewe kufanya utafiti.
 


Mimi pia nawakubali kinoma.
 
Kuna sehemu mkuu The coder, unasema ulimwengu hautaki tufike level flan ya maarifa, na ukatoa mifano ya sodoma, gharika, nk, kwanini usiwaze kua Kuna utawala mkuu sehemu flani ulimwenguni unaodhibiti hizo Hali, au ukubaliane na watu wa dini wanavyoamini?
 
Ukitoka nje ya solar system tuliyopo.. more far kuna jua lingine na solar sytem nyingine yenye Dunia kama hii na watu kama sisi.

Nje ya hiyo tena kuna nyingine tena na tena.. ukienda north- south, east -west..

Hivyo hii solar sytem yetu ipo ndani ya solar sytem nyingine ambayo na yenyewe ipo ndani solar sytem.. and more …and more like that.

Hivyo MAISHA TUNAYOISHI YALIKUEPO na yataendelea kuepo. Ni mawazo yangu tu.
 
Inawezekana ni sahihi wanachokisema ndio maana labda tupo limited kwenye mambo kadha wa kadha.

Au labda ni asili ya dunia yenyewe tu, kwamba inaamua jambo lipi liwepo jambo lipi lisiwepo katika wakati gani.
 
Mkuu mi nimejiuliza kwa hoja zako hizi wewe unadhani ilipaswa/ulitaka iwaje?. Kwasababu existence ya Ulimwengu ni matokeo ya utumwa wa Time+Space+Matter
 
Mkuu mi nimejiuliza kwa hoja zako hizi wewe unadhani ilipaswa/ulitaka iwaje?. Kwasababu existence ya Ulimwengu ni matokeo ya utumwa wa Time+Space+Matter
Hata huo utumwa wa Time + Space + Matter unaonekana kufanya kazi kwa msingi wa kumbukumbu tu.

Kwa maana muda wenyewe hauwezi kueleweka bila kumithirisha kilichopita na kilichopo sasa, vile vile space huwezi kuitambua bila reference ya sehemu nyingine ulizowahi kuziona na matter nayo hupata maana kutokana na patterns ambazo tayari zilishawahi kuonekana hapo kabla.

Kwahiyo hoja yangu kuu ni kwanini consciousness ya mwanadamu imefungwa ndani ya mfumo unaolazimisha kila kitu kiwe interpreted kupitia past?.

Kwa maana hata physics yenyewe haiwezi kufanya prediction bila kutumia previous observations.

Hakuna formula inayotabiri future kutoka kwenye utupu so lazima ichukue data za kale then ndio ijenge sheria fulani.

Ndio maana nikaja hapa tusaidiane kutafakari kwenye hili eneo, ila pia tujiulize kwa pamoja...

Je, sisi tunajua ukweli wa mambo,
au tunajua tu repetition ya mambo?

Kwasababu hata ukisema universe ni matokeo ya Time + Space + Matter, bado understanding yako ya hivyo vitu vitatu umetengenezewa na historical observation... Au nadanganya mkuu?

Hujawahi kushika future,
umeshika mabaki ya jana kisha ukayatumia kukisia kesho, hivi ndivyo always tunafanya.

So kutokana na Hilo ndio maana nikasema huenda hapo ndio limitation ya akili ya mwanadamu ilipo, ya kwamba haiishi nje ya mfumo wa kumbukumbu, ya kwamba asipokua na kumbukumbu yoyote ya kale kichwani mwake hawezi kuwa kama alivyo sasa.

Ila pia nikasema, sayansi yenyewe ni historia iliyokataa kufa.

Kwa sababu sheria zote za kisayansi ni matukio yaliyotokea mara nyingi sana hadi tukayapa hadhi ya ukweli wa kudumu ila in reality bado msingi wake ni past.

So andiko lote limekaa kutafakari zaidi pasipo kudemand au kutaka kubadili chochote kwenye universe especially dunia ila kwa jinsi mambo yalivyo naona tunaishi past na sasa sio sasa na future.
 
Huenda unachokisema ni kweli mkuu, maana ukiangalia kwa umakini utagundua ni almost kila mfumo upo ndani ya mfumo mwingine kisha baada ya hapo hauelewi.

Mfano, solar system ndani ya galaxy, galaxy ndani ya cluster, cluster ndani ya structure mama.

So, kwa mtazamo huo huenda hata hii tunayoiita universe ni chembe ndani ya kitu kingine kikubwa tusichoweza kukiona.

Kwahiyo, maisha tunayoyaona na kuyaishi yanaweza kuwa si tukio jipya kama tunavyodhani bali inawezekana ikawa ni pattern inayojirudia milele katika viwango tofauti vya existence.

Kwa sababu ukiiangalia dunia kwa jicho la kawaida utaona vitu na mambo mengi yanakufa, lakini ukiiangalia kwa jicho la tafakari utaona mambo mengi hayafi bali yanabadilisha tu sura.

Kwamfano, vizazi vinaondoka lakini tabia zilezile zinarudi. , falme zinaanguka lakini mifumo ileile inajengwa tena kwa majina tofauti, teknolojia zinabadilika lakini tamaa, hofu, mapenzi, vita, nguvu, udhaifu na maswali yanabaki yale yale.

Hii inamaanisha nini sasa?, hii inamaanisha kwamba...

Existence yote inaendeshwa na repetition kubwa yenye masks tofauti kila baada ya muda fulani.

Na ukiendelea kutafakari hapo kwenye hoja yako basi utaenda mbali zaidi hadi kuhisi labda sisi sio mwanzo, wala mwisho wa maisha,
bali ni mwendelezo wa pattern ambayo imekuwa ikijirudia kwenye kona tofauti za reality kwa muda usiojulikana.

So ni kama hakuna jambo jipya bali kuna muonekano mpya wa jambo la zamani.

Na kama hii hoja ya kila kitu kunajirudia ni kweli, basi hata sisi pamoja na hiki tunachokiwaza tulishawahi kuwaza hivi katika namna tofauti ila yenye maana hii hii hapo kabla.

Then utamalizia kusema future ni historia ambayo bado hatujaifikia?

Kisha hapo utagundua maisha ni infinity loop ambayo huanzia leo itakayogeuka kuwa jana na kesho itayogeuka kuwa leo katika mtindo wa kujirudia rudia ikiwa zimebebwa na matukio tofauti tofauti ila yenye maana ile ile moja 😅😅.

Anyway, wacha nikalale sasa...
 
Noted
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…