MwitaOmondi
New Member
- Jul 8, 2015
- 2
- 1
Mtangazania Jimbo la Musoma mjini kwa tiketi ya Chadema, Eliud Tongora (a.k.a. Mkorea) anajiandaa kuipeleka Chadema mahakamani ili alipwe pesa zake sh. 6,000,000/- (milioni sita) alizowapa viongozi wa Chadema wilaya ya Musoma mjini kwa madai kuwa angepitishwa bila kupingwa kugombea Ubunge Jimbo la Musoma mjini.
Jimbo la Musoma mjini ni Jimbo linaloongozwa na Mhe. Vincent Nyerere ambae hakupatikana mara moja kujibu madai haya. Habari za ndani zinaeleza kuwa Tongora kama anavyosema, aliahidiwa pia na viongozi waandamizi wa Chadema akiwemo Rebecca Mngodo, John Shibuda na Said Arfi kuwa angepitishwa kugombea Ubunge huo wa Musoma mjini kwenye vikao vya juu vya Chadema.
Mtangaza nia Tongora baada ya kutoona dalili zozote za ahadi yake kutekelezwa hasa baada ya Mbunge Vincent kuwa na mkutano wa hadhara wenye mafanikio, juzi Jumatatu tarehe 6/7/2015 ametishia kukipeleka Chama cha CHADEMA mahakamani au arudishiwe pesa zake. Viongozi wa wilaya wao wanadai walipokea pesa za Mtangazania huyo na si kwa kiasi anachodai kama mchango wake kwa Chama na si kama anavyodai hivi sasa.
Jimbo la Musoma mjini ni Jimbo linaloongozwa na Mhe. Vincent Nyerere ambae hakupatikana mara moja kujibu madai haya. Habari za ndani zinaeleza kuwa Tongora kama anavyosema, aliahidiwa pia na viongozi waandamizi wa Chadema akiwemo Rebecca Mngodo, John Shibuda na Said Arfi kuwa angepitishwa kugombea Ubunge huo wa Musoma mjini kwenye vikao vya juu vya Chadema.
Mtangaza nia Tongora baada ya kutoona dalili zozote za ahadi yake kutekelezwa hasa baada ya Mbunge Vincent kuwa na mkutano wa hadhara wenye mafanikio, juzi Jumatatu tarehe 6/7/2015 ametishia kukipeleka Chama cha CHADEMA mahakamani au arudishiwe pesa zake. Viongozi wa wilaya wao wanadai walipokea pesa za Mtangazania huyo na si kwa kiasi anachodai kama mchango wake kwa Chama na si kama anavyodai hivi sasa.