SIMU YA TOCHI
JF-Expert Member
- Dec 12, 2014
- 1,385
- 894
Jinga kabisa hilo li mkorea kama lingekuwa ni kaka yangu ningeenda kulibadili kwa debe la mahindi mnadani
Taarifa hii ni yauongo, nimezungumza na viongozi wa Wilaya wamekanusha kupokea pesa hiyo, Mwekahazina wa Wilaya amesema wazi kuwa utaratibu wa upokeaji wa michango ya wadau na wanachama hufanywa kwakufuata misingi yote ya utawala wa fedha,
Amemtaka huyo binadamu aende kwenye vyombo vya kisheria kama anaamini yupo sahihi kwa madai yake.
Mtangazania Jimbo la Musoma mjini kwa tiketi ya Chadema, Eliud Tongora (a.k.a. Mkorea) anajiandaa kuipeleka Chadema mahakamani ili alipwe pesa zake sh. 6,000,000/- (milioni sita) alizowapa viongozi wa Chadema wilaya ya Musoma mjini kwa madai kuwa angepitishwa bila kupingwa kugombea Ubunge Jimbo la Musoma mjini.
Jimbo la Musoma mjini ni Jimbo linaloongozwa na Mhe. Vincent Nyerere ambae hakupatikana mara moja kujibu madai haya. Habari za ndani zinaeleza kuwa Tongora kama anavyosema, aliahidiwa pia na viongozi waandamizi wa Chadema akiwemo Rebecca Mngodo, John Shibuda na Said Arfi kuwa angepitishwa kugombea Ubunge huo wa Musoma mjini kwenye vikao vya juu vya Chadema.
Mtangaza nia Tongora baada ya kutoona dalili zozote za ahadi yake kutekelezwa hasa baada ya Mbunge Vincent kuwa na mkutano wa hadhara wenye mafanikio, juzi Jumatatu tarehe 6/7/2015 ametishia kukipeleka Chama cha CHADEMA mahakamani au arudishiwe pesa zake. Viongozi wa wilaya wao wanadai walipokea pesa za Mtangazania huyo na si kwa kiasi anachodai kama mchango wake kwa Chama na si kama anavyodai hivi sasa.
Mleta mada unaharufu ya unafiki afri shibuda wote wanajulikana ni kina nani hivi huyo jamaa mpaka anataka kugombea,ubunge cdm akijiu chama mpaka awape ela hao watu huu ni uongo na unafiki tena wewe unastahili kuwa kule wasaliti walipo
Yawezekana ni staili aliyotokanayo huko alikokuwa ndiyo maaana katoa Rushwa na bila aibu anatamka katoa Rushwa ili apitishwe peke yake bila kupingwa, alafu aende mjengoni kuwatetea watanganyika na nyika yao. Cha kujiuliza hizo pesa katoa wapi? Na atarudishaje ikiwa atapata nafasi. Je? Siyo sisiemu ndani ya Chadema huyo? Na ikiwa Shibuda aliongea naye pamoja na Arf kwanini asiwafuate ili wamurudishie pesa zake badala ya kusema Chadema.
Aende kule Said Arfi na Rebecca Mgondo walipokuwa wamemuahidi cheo
Musoma imekuwa kama kijiji tangu Vi-cent awe mbunge. Rudisha hela au kortini. cdm bana kudadadeki na Ukawa kimenuka
alifikiri viongozi wa chadema musoma hawana uzoefu na mazuzu, wacha ile kwake kdg
Mbuzi anaenda kufia Kwa muuza supu