Eliud Tongora kuipeleka CHADEMA Mahakamani

Eliud Tongora kuipeleka CHADEMA Mahakamani

madai kama haya ata Afande sele aliwahi kusema kuwa aliambiwa atoe hela ili wampitishe agombee ubunge kwa tiketi ya CHADEMA morogoro mjini alikataa wakamwambia agombee udiwani ubunge nafasi zimejaa

Wanaongea vitu kama hivyo ujue si wanaCDM na hawajui Itikadi na sera za CHADEMA sababu waraka maalumu ulishatolewa makao makuu wanaohitaji kugombea uongozi wa Ubunge na madiwani wapeleke maombi yao mapema makao makuu kwa Katibu Mkuu kwa ajili ya kuwafuatilia tabia, mienendo na uadilifu wao. Hao wanaokurupuka tu kuongea walikwishasoma alama za nyakati kwamba watu wanaokwenda kukutana nao kwenye ushindani ndani ya Chama hawawezi Mfano Afande Sele Morogoro mjini alikwishaona hana uwezo wa kumshinda Dr. Malukus ambaye ni mwanasheria na mwanaharakati mwenye jina kubwa Moro.
 
Eti aliahidiwa na Arfi na Shibuda kuwa atakuwa mgombea wa CDM Musoma mjini??!!

Oooh Gosh my ribs, With all the people Arfi and Shibuda! I'm speechless and mouth open.
 
Nayeye haponi mtoa na mpokea rushwa wote ni wahalifu, halafu watu anaowataja kuwa walipokea hiyo hela siyo wanachama wa Chadema, Arfi na Shibuda hao wote ni makada wa ccm waliokuwa wamejichimbia Chadema, hivi sasa wamesharudi kwao baada ya kushindwa kazi waliyopewa. Tongora kama ana malalamiko aende Lumumba kwa mabosi wa Shibuda na Arfi
 
Mwambieni Arfi ni tapeli, amfuate mpanda amlipe
Hata huyo Tongora ni tapeli. Mwaka 2010 alivyoshindwa kura za maoni ccm alipewa pesa na TLP Musoma ili awe mgombea wao, pesa alikula akaishia mitini.

Mimi nashauri uongozi wa juu ulifanyie uchunguzi swala hili na mengine mengi kuhusu uongozi wa CDM Musoma mjini. Kumekuwa na malalamiko mengi kuhusu uongozi wa Musoma mjini, yasiachwe hivihivi.
 
Huyo Tongora ni Mjasiriasiasa tu sidhani kama ana mkakati wowte katika kukujenga chama na kusukuma gurudumu la Chadema na UKAWA mbele. Mwaka 2010 alikuwa CCM, baada ya kupigwa chini kura ya maoni akakimbilia CUF nako alipoona hakuna chochote akakimbilia TLP napo hivyo hivyo baadaye akakimbilia kuchukua kadi ya Chadema ambayo ndiyo anawasumbulia wenye akili zao eti wampitishe na kumuacha jembe letu, Vincent Nyerere. Arudi kwa hao hao waliomtuma, Musoma Mjini ni UKAWA kwa kwenda mbele huo Ujasiriasiasa wake aurudishe huko Jamhuri ya Korea.
 
Si awafate Shibuda na huyo Arfi awsdai ela zake.
CDM inawahusu nini?
Yaani Shibuda na Arfi ambao wamejitoa kwenye chama ndio walikula hela yake? By the way, kwa nini utoe hela kwa ahadi ya kupitishwa bila kupingwa ndani ya chama wakati kuna majimbo kibao kila awamu hukosa wagombea ubunge wa upinzani?
 
Masikini wa Mungu MKorea tazama alivyo kuwa anarekodi mkutano mzima wa Chadema juzi..😁😁😁pole yako Musoma mjini ni ya Vincent Nyerere na wana Musoma✌✌
 

Attachments

  • 1436444283184.jpg
    1436444283184.jpg
    67.7 KB · Views: 198
Mtangazania Jimbo la Musoma mjini kwa tiketi ya Chadema, Eliud Tongora (a.k.a. Mkorea) anajiandaa kuipeleka Chadema mahakamani ili alipwe pesa zake sh. 6,000,000/- (milioni sita) alizowapa viongozi wa Chadema wilaya ya Musoma mjini kwa madai kuwa angepitishwa bila kupingwa kugombea Ubunge Jimbo la Musoma mjini.

Jimbo la Musoma mjini ni Jimbo linaloongozwa na Mhe. Vincent Nyerere ambae hakupatikana mara moja kujibu madai haya. Habari za ndani zinaeleza kuwa Tongora kama anavyosema, aliahidiwa pia na viongozi waandamizi wa Chadema akiwemo Rebecca Mngodo, John Shibuda na Said Arfi kuwa angepitishwa kugombea Ubunge huo wa Musoma mjini kwenye vikao vya juu vya Chadema.

Mtangaza nia Tongora baada ya kutoona dalili zozote za ahadi yake kutekelezwa hasa baada ya Mbunge Vincent kuwa na mkutano wa hadhara wenye mafanikio, juzi Jumatatu tarehe 6/7/2015 ametishia kukipeleka Chama cha CHADEMA mahakamani au arudishiwe pesa zake. Viongozi wa wilaya wao wanadai walipokea pesa za Mtangazania huyo na si kwa kiasi anachodai kama mchango wake kwa Chama na si kama anavyodai hivi sasa.

Hao waliomwahidi hapo kwenye Red MMMMMMH!!!inatia shaka hata uelewa na ufuatiliaji wa mambo ndani ya chama kwa Mtangaza nia!
 
Wajameni, ndugu moja tunajenga nyumba moja, ya nini kugombania fito? Ndugu Eliud Tongora kama nilivyoonana naye leo ofisi za Chadema akirudisha fomu ya kugombea Ubunge wa Musoma Mjini, asingeenda huko mbali eti apitishwe bila kupingwa kwa vihela akigawa-gawa kwa viongozi wetu. Miye naona amepoteza na anazidi kupoteza muda na hela zake. Tangu baada ya Uchaguzi wa 2010 hakuonekana mpaka hivi karibuni tena karibu na Uchaguzi wa Oktoba 2015. Miye kwa kumshauri, angechukua fomu agombee Udiwani, hapo ungekuwa ni mwanzo wake mzuri kwake kupitia Chama kuliko kujidanganya kwamba atapitishwa kwa nguvu za hao Viongozi wa Wilaya na wamuache 'jembe,' Mhe. Vincent Nyerere.
 
Unatapeliwa kifala halafu unatishia kwenda mahakamani, huyu ndo mjinga kabisa, hajui kushtaki Chama mahakamani ni kujifukuza Chama moja kwa moja
 
Mpuuzi tu kwani hajui taratibu za chama za kupata wagombea, mgombea gani mjinga kiasi hicho hahaha
Hata kwa kurumangia hafai kama kweli hayo ndo yalojiri.Iweje demokrasia iuzwe/kumilikishwa kwa mtu mmoja tena kwa tupesa tudogo kiasi hicho.Waliostaafu ubunge wanaruka na 230 M..amabo ni mtaji tosha yeye anaununua kwa 6M.Kama ndo ilivyo cheap mimi namrejeshea mara mbili yake nikagombee mimi...nyambaf.Mahakama ni kama sebule wote hupitia wanapoelekea vyumbani mwao.Hata CCM walishakipeleka chama hicho mahakamani mara ntingi lakini matokeo yakawa.....Hajiulizi mbona wawili hao (Arfi na Shibuda) wameshatangaza kutogombea kupitia CDM lakini hawakumpa nafasi ya yeye kwenda kugombea huko kwao?

 
Eti aliahidiwa na Arfi na Shibuda kuwa atakuwa mgombea wa CDM Musoma mjini??!!

Oooh Gosh my ribs, With all the people Arfi and Shibuda! I'm speechless and mouth open.

Ha ha ha ha nimecheka sana mkuu.!!?
 
Taarifa hii ni yauongo, nimezungumza na viongozi wa Wilaya wamekanusha kupokea pesa hiyo, Mwekahazina wa Wilaya amesema wazi kuwa utaratibu wa upokeaji wa michango ya wadau na wanachama hufanywa kwakufuata misingi yote ya utawala wa fedha,

Amemtaka huyo binadamu aende kwenye vyombo vya kisheria kama anaamini yupo sahihi kwa madai yake.
 
Wanaongea vitu kama hivyo ujue si wanaCDM na hawajui Itikadi na sera za CHADEMA sababu waraka maalumu ulishatolewa makao makuu wanaohitaji kugombea uongozi wa Ubunge na madiwani wapeleke maombi yao mapema makao makuu kwa Katibu Mkuu kwa ajili ya kuwafuatilia tabia, mienendo na uadilifu wao. Hao wanaokurupuka tu kuongea walikwishasoma alama za nyakati kwamba watu wanaokwenda kukutana nao kwenye ushindani ndani ya Chama hawawezi Mfano Afande Sele Morogoro mjini alikwishaona hana uwezo wa kumshinda Dr. Malukus ambaye ni mwanasheria na mwanaharakati mwenye jina kubwa Moro.
basi ktk hizo kanuni na taratibu za huo waraka maalum unaoelekeza mtia nia kutuma maombi makao makuu unatoa mianya kwa watu wachache kupitisha milungura. elimu/taaluma,umaarufu au nafasi pekeake haitoshi kupata mgombea bora ndio maana kunatokea mambo kama hayo.''CHAMA KINACHOPUUZA MAONI YA WATU KITALIA'' Mwalimu Nyerere
 
basi ktk hizo kanuni na taratibu za huo waraka maalum unaoelekeza mtia nia kutuma maombi makao makuu unatoa mianya kwa watu wachache kupitisha milungura. elimu/taaluma,umaarufu au nafasi pekeake haitoshi kupata mgombea bora ndio maana kunatokea mambo kama hayo.''CHAMA KINACHOPUUZA MAONI YA WATU KITALIA'' Mwalimu Nyerere

Nasikitika hujaelewa content za waraka. Maombi yanapelekwa kufuatilia tabia, mienendo na uadilifu na si kuteua WAGOMBEA MAJINA YATAPIGIWA KURA ZA WANACHAMA KWENYE KATA NA MAJIMBO YAO (KURA ZA MAONI) na lengo lake ni kuudhibiti wagombea ambao wanakuja kusaliti sera, misimamo, uadilifu kwa chama na kuepusha watu kuibuka dakika za mwisho nakuja kupata mgombea kumbe ana kasoro nyingi. kama ilivyotokea 2010 kuna watu walichaguliwa kugombea kumbe hajui hata sera za chama zinasemaje mfano Shibuda na Selasini, meya wa mwanza na wengineo. Naamini utakuwa umeelewa
 


Jimbo la Musoma mjini ni Jimbo linaloongozwa na Mhe. Vincent Nyerere ambae hakupatikana mara moja kujibu madai haya. Habari za ndani zinaeleza kuwa Tongora kama anavyosema, aliahidiwa pia na viongozi waandamizi wa Chadema akiwemo Rebecca Mngodo, John Shibuda na Said Arfi kuwa angepitishwa kugombea Ubunge huo wa Musoma mjini kwenye vikao vya juu vya Chadema.



Mkuu unauwakika ni CHADEMA ? maana hapo wote ulio wataja ni wnachama wa Chama cha wasaliti ?
 
Back
Top Bottom