Unachosema Mkuu Mr Rocky ni kweli kabisa, lakini pamoja na kuwa watoto wao ambao ni asilimia ndogo sana ya Watoto wa Tanzania hawasomi katika shule hizo lakini hakuna sababu yoyote ya kuiacha Elimu nchini ianguke kiasi hiki. Wanabwabwaja kwa dakika chache mjengoni kisha hakuna lolote la maana linalofanyika na huku elimu ikiendelea kuporomoka.
Mkuu BAK nani anayewaza hayo kwamba kuna mtoto wa mlala hoi kule chunya au kasulu ambaye anakalia jiwe au hana kitabu cha kiada au hana mwalimu wa kumfundisha au shule yake haina maabara
Wewe ndio unaona uchungu na elimu yetu ila waliokalia viti vya kunesa na kupigwa na kiyoyozi watoto wao wako shule za St nanihii na International School au wako Malaysia au South Africa au Uk wanasoma au wakiwa hapa bongo wako Feza au Tusiime na sio shule ya kijijini kwako ambako mwalimu akifuata mshahara shule inafungwa mpaka arudi
Bungeni mimi naitaga comedy maana hakuna wanachojadili wanapiga makofi na kugonga meza hata kwa upuuzi au kwa porojo za mchakato sijui tuko kwenye mpango ambako hizo comedy tumezisikia toka tunajua kuwa kuna bunge
And then viongozi wako kwenye ziara wanafuatilia utekelezaji wa ahadi na ilani za chama na kuangalia namna wanafunzi wanavyokaa chini kwenye vumbi wakati makampuni yao yanashindana kusafirisha mbao na magogo nje ya nchi kupata fedha za kigeni
Halafu BAK unajua ni aibu mbao zinatoka mikoani huko ila huko ndio kunaongoza kwa watoto kukaa kwenye mawe na sakafuni
Last edited by a moderator: