Elimu bure ni ndoto za abunuasi

Elimu bure ni ndoto za abunuasi

Pj nani kakwambia mzunguko wa pesa ni mdogo hali Mafisadi wanaibuka kama mzunguko ungekuwa mdogo hilo lisingekuwepo tatizo ni ubinafsi wa wachache kujilimbikizia mali na kuacha wengine wakiteseka

alichojaribu kusema huyo victoire ni kuua ndege wawili kwa jiwe moja, ni hivi serikali inazuia pesa kwa wingi at the same time wana ongeza matumizi (contractionary monetary policy and expansionary fiscal policy) ndo leo tunaona maswala ya kuimport BVR tools, ambapo kwa upande mwengine imeonekana kuwa imekaa kimasilahi zaidi kwa wanasiaisa wetu kwa kuwa ni project iliyotengenezwa ili kupiga hela...ndo hilo tatizo la ubinafsi na ufisadi unaozungumzia ambapo mwisho wa siku kunasababisha yote haya ya kuporomoka kwa uchumi na maswala mengine yanayohusiana nayo.
 
Tanzania hakuna mafuta,hata kama yapo hayatafikia ya Angola,Congo brazaville,Gabon na Nigeria.

hayatafikia ya Angola,nk;umepima?
unatunisha maziwa ujasiri unatoa wap;ccm wamechukua mpk uwezo wako wa kufikiri
unaandika pumba tupu hap
 
Pj nani kakwambia mzunguko wa pesa ni mdogo hali Mafisadi wanaibuka kama mzunguko ungekuwa mdogo hilo lisingekuwepo tatizo ni ubinafsi wa wachache kujilimbikizia mali na kuacha wengine wakiteseka
Think out side the box
 
Binafsi nimesoma bure kuanzia darasa la kwanza hadi chuo sasa wewe unayesema ni ndoto za abunuasi umekuwa na roho ngumu ya kuamini kwanini.Muulize mgombea Urais Magufuli au huyo Lowasa alilipa kiasi gani kwenye elimu yake hakika atakueleza ni bure kwanini leo isiwezekane?.hadi mwaka 1997 elimu ilikuwa bure baada ya hapo ikawa ya kulipia tena kwa faida yako tulilipiwa hadi usafiri kwa kwenda na kurudi shule wakati huo tulitumia "warranty" JKT tulikuwa tunalipwa stipend allowance ununue sabuni ya kufulia au mahitaji yako muhimu ya kibinadamu na ilikuwa inatosha. chuo chakula unaenda mess unaagiza chakula kilichopikwa siku hiyo,malazi bure na hela ya vitabu kalamu au mahitaji yako ya muhimu unapewa cash.ukimaliza chuo unapangiwa kazi siyo kuandika barua za maombi na kuzunguka nazo hadi unakata tamaa hakuna msomi aliyekosa kazi hii ndiyo sababu watu wanataka mabadiliko hivi sasa viwanda vyote vilivyokuwa sehemu kubwa ya ajra vimekufa migodi imebinafsishwa mashamba ya mifugo na mazao yote yameuzwa vimeanzishwa viwanda vya kiushkaji vya kichina na kihindi wanaleta watu wao kufanya kazi zinazoweza kufanywa na wa TZ tena vinatumia teknologia ya karne ya 19 wakati tuko karne ya 21 inasikitisha sana.
 
Mleta mada,

Elimu bure Tanzania inawezekana. Kwanza uelewe kitu kimoja, elimu hii itatolewa kwa shule na kwa vyuo vya serikali tu. Hivyo basi, hii inafanya wale wanafunzi waliopata fursa na nafasi ya kusoma katika shule na vyuo hivyo vya serikali wafaidike na sera hiyo na sio kila mwanafunzi wa Tanzania kama ambavyo inatafsiriwa na baadhi ya watu.

Kingine cha muhimu katika hii sera ni kuhakikisha mazingira bora yanakuwepo ili watoto wetu waweze kupata elimu bora na sio bora elimu.


Muulize CCM wanapoahidi milion 50 kila kijiji na kuna jumla ya vijiji zaidi ya 18,000 akipeleka kwa elimu haitatosha?
 
Back
Top Bottom