Tuna safari ndefu ya kwenda ili kufikia lengo la elimu bora kwa kila mtoto.
Hao tunaowaona hawapati elimu bora, wapo kwenye mazoezi ya kupiga desa kwa ajili ya mitihani ya nekta
Hilo darasa mbona limeendelea sana na linaweza kuwa la mfano,kama ukitembelea kijijini kwetu Nusa ndipo utaweza kuona darasa halisi la mpiga kura wa CCM.Nikipata picha zake nitakuwekea.
Mnamlipa Downs bilioni 185, IPTL kila siku milioni 55, madini wazungu wanajichukulia kama vile mali yao wanawapa commission watu wa serikalini, halafu SERIKALI inaenda UN kujisifia kuhusu elimu, aibu kubwa hii sababu hela tunayo ya kuondokana na haya mateso kwa watoto.
Lakini ccm haiwezi kutuletea mabadiliko, lazima tuongoe kabla hata hayo madarasa hayajaezuliwa mabati na kupelekwa kwenye mabanda ya kukunua vyuma chakavu
:redfaces: kweli tanzania hakuna usawa wenzenu afya tu wanachekiwa ulaya, spika anajengewa jumba la mamilioni tena lenye swimming pool, dowans wanalipwa alote of shillings but luk at wat they did to our children with our own money, may God help us. poor us ...............
Kweli elimu bora kwa kila mtoto wa kitanzania inawezekana. Wenzetu wanafikiria kufanya tafiti za kisayansi kwenye sayari mbalimbali watoto wetu wanasoma wakikaa chini.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.