Uwezo Tunao
JF-Expert Member
- Nov 14, 2010
- 6,942
- 1,190
Dr Mohamed El Baradei ajichanganya na waandamanaji mitaani kuwahutubia na kuwatia wazimu mkali kwa kitendo cha kuonekana tu hata kabla ya tamka neno.
Yule kiongozi mstaafu wa Tume ya Umoja wa Mataifa kuthibiti mabaya Nguvu za Nuklia Duniani, Dr Mohamed El Baradei, aongoza njia katikati ya umati mkubwa ajabu kwenda kuwahutubia Wa-Misri wanaoandamana wenye hasira nyingi kutaka serikali ya Hosni Mubarak ijiuzulu.
Kulikua na mlipuko mkubwa sana wa kelele za furaha zikisikika kila mahali tangu habari kuenea kwamba El Baradei yuko njiani anakuja kuwahutubia.
Hiyo hali iliendelea muda mrefu hata kabla kiongozi huyo hajawasili mahali hapo huku akisaidiwa na walinzi vijana wadogo wa kujitolea wakimzingira kila upande.
Haikuwa kazi rahisi hata kidogo hata kusema sentensi akamaliza mara baada ya waandamanaji kumtia machoni pale uwanja wa Tahriri Square.
El Baradei, kwa kufungua tu kinywa chake kwa sentensi ya kwanza tu huku akiwapungia waandamanaji kila upande, alitoa maneno machache kwa lugha ya Kiarabu na karibu kila mwandamanaji mahali hapo kuonekana wazi kulewa na furaha, shangwe na nderemo kwa takriban muda wa dakika 15 na yakatafsiriwa na Al Jazera kwa Kiingereza kama vile:
"Wameiba uhuru wetu, tumelitambua hilo na tayari tupo kwenye safari ya kujikomboa. Hakuna wa kuturudisha nyuma - Mubarak na serikali yake zima wajiuzulu mara moja," El Baradei adondosha huo 'mzinga' dhili ya Mubarak dakika chache zilizopita.