Eid Mubarak!!

byeyombo

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2015
Posts
3,912
Reaction score
5,166
Asalaam aleykum wanabodi,
Napenda kuchukua nafasi adhimu kuwatakia waislamu wote iddi njema popote walipo.
Tutumie sikukuu hii katika kufurahi na kuwatembelea ndugu na jamaa na pia tusisahau kuwakaribisha Majirani zetu hata kama sio waislamu wapate kusherekea nasi kwani uislamu unafundisha kwamba jirani yako ni ndugu yako.
Tujiepushe na maasi kwenye sikukuu hii ya idd.
Mwenyezi mungu atufanyie wepesi
Amiiin!!!
 

Attachments

  • 6d49a175591bb4af4bc2ca60fbb87ae5.jpg
    38.8 KB · Views: 37
Huku kwetu kiumbe mmoja tu anaamua kujitwika mamlaka ya kuamua mambo ya Mungu. Kila kitu kilikuwa wazi kuwa Eid ni Jumanne lakini Zuberi Simba kwa matakwa yake kaamua kuipeleka jumatano. Halafu mwenye yupo Hija sasa sijui anahiji nini huko kama si unafiki.
Hii nchi laana yake ni ya kiwango cha mwisho maana Jiwe linatesa na dini nazo zimepata wapigaji, sijui tukimbilie wapi.
 
Kwahiyo Kesho wanafunga sio..dah!!
 
Tunaotambua unafiki Wa hao bakwata tushawapuuza kitambo

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Byeyombo umeongea maneno ya busara. Huo ndio uungwana. Sote tunamwabudu Mungu mmoja tu. Mtu anayeigeuza sikukuu ya dini kuwa siku ya kufanya maasi hafai kuitwa binadamu. Heri angezaliwa mbuzi!! Idd njema
 
Byeyombo umeongea maneno ya busara. Huo ndio uungwana. Sote tunamwabudu Mungu mmoja tu. Mtu anayeigeuza sikukuu ya dini kuwa siku ya kufanya maasi hafai kuitwa binadamu. Heri angezaliwa mbuzi!! Idd njema
Pamoja mkuu...Respect!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…