snowden E,
Katika Majmul Fatawa Wamaqalaati Mutanawwia, Mujallad wa 15 Swafha ya 79 Sheikh Abdulaazizi Ibn Baazi aliulizwa. Swali linasema:
Muundamo wa mwezi unatofautiana (kwa maana Ramadhani). Kuna tofauti kati ya mwezi wa Ramadhani na Arafa(Yaani Ramadhani yafaa kufuata miezi ya mbalimbali lakini Arafa tufuate mahuujjaj)?
Sheikh akajibu: Fadhwahir annahu la faraqa bayna Ramadhwana wal Adh'ha fiimaa aalam minashariaa.
Kwa maana: Ni dhahir( wazi iliyopo) hakuna tofauti iliyopo baina ya Ramdhani na Adh' ha.( Yaani Ramadhani inafuata mwandamo wa mwezi na Al Adh' ha inafuata mwandamo wa mwezi) kwa kile ninachokijua mimi katika SHARIA.
Majmul Fatawa: Mujallad wa 20, Sheikh Muhammad Bin Swaleh Al Uthaimiin aliulizwa, swali linasema:
Ikitofautiana siku ya Arafa kwa kutofautiana sehemu mbalimbali katika miandamo ya mwezi. Je, tufunge kwa kufuata mji ambao tupo ndani yake? Ama tufuate mwandamo wa Makkah?
Sheikh Al Uthaimiin akajibu:
Hili linajengwa kwa ikhtilafu ya Ahlul ilm( walipozungumzia Je, mwezi ni mmoja popote utakapoonekana ufuatwe ama una tofautiana kwa kutofautiana miandamo yake). Sheikh akatoa mfano katika jawabu lake akasema:
Ikiwa mwezi umeonekana katika mji wa Makkah na ikiwa ni siku ya 9 unavyoonekana mwezi katika mji mwengine (kabla ya Makkah, kwa maana mji mwengine umeutangulia Makkah kwa siku na huo mji ni siku ya 9) kwa siku. Na ikawa siku ya Arafa kwao Makkah na ni siku ya 10 kwa mji huo uliyoutangula Makkah. Sheikh anasema "Fa' annahu la yajuuzu lahum an'ya suumu hadhal yaum, Liannahu yaumul iid"
Sheikh anasema haitojuzu wao kufunga ikiwa Makkah ni siku ya 9 na kwa mji mwengine ni siku ya 10. Kwa sababu hao wa siku ya 10 kwao ni siku ya EID. Na sheikh akasema vilevile:
Wakadhalika lau itakadiriwa kule mji mwengine wameuona mwezi kabla ya Makkah( Maana Makkah wametangulia kuuona) na Ikiwa Makkah ni siku ya 9 na mji mwengine ni siku ya 8. Sheikh akasema:
" Fa' anna ya suumuna yawma ttisii in'dahum" kwa maana hao wa mji mwengine watafunga siku ya kwao ya 9 itapoingia ambayo kwa Makkah itakuwa ni siku ya 10. Sheikh akasema: Hadhal huwal Qauli rrajii, kwa maana hii ndiyo kauli yenye nguvu.
Vile Sheikh Al Uthaimiin akairudia hii kauli katika Mujallad wa 19, Swafuha ya 41.
Na mwandamo wa mwezi wa Dhul hijja ni kama wa Ramadani kama Sheikh Ibn Baaz alivyosema kwamba watu wafuate miandamo ya maeneo yao. Na si yeye bali hata kwa madhehebu ya:
Imam Abuu Hanifah, tizama Maimamu wakubwa wa hayo madhehebu, mfano: Sheikh Zaada katika Majmul Anhar, Al Imam Kassaani katika Baadaril Uswani, Imam Zay Lai katika Tabiinul Haqaiq.
Madhehebu ya Imam Malik nao wana wa Zuoni wengi kauli ni ufuate mwezi wa kwako. Mfano Maimam Kama: Qurtubii, Ibn Barr, Ibn Rashid n.k
Madhehebu ya Imam Hambali, Imam Hambali anasema mwezi ni mmoja. Sheikh Al Islam Ibn Taymia anasema katika majmul Fatawa kuwa Kauli ya Imam Hambal inamaanisha kwa miji ya karibu si miji ya mabli.
Kwa Imam Shafii karibu wote. Haya niambie upotofu wangu upo wapi?