na mimi ndo nilichokuwa nataka kukimaanisha!!He is foolSikuwa msikilizaji sana wa Clouds. Yapata kama mwaka na kidogo hivi nikashawishika kuisikiliza hasa vipindi vya asubuhi kabla sijaingia mzigoni. Kwa kiasi nilianza kupenda pale walipokuwa "Critique" kwa watumishi wa uma au watu walioshika dhamana. Ukosoaji wao ulinishawishi kuamini kuwa ni sauti au radio ya watu. Nika-extend my hearing mpaka vipindi vya jioni. Huko nikakutana na kibonde. Haikunichukua muda mrefu kuwa fade-up na radio hiyo na kuacha kabisa kuisikiliza. Ilikuwa ni Kibonde, kama ambavyo nimesoma baadhi ya maoni hapo juu, ilikuwa dhahiri huyu mtu ameingia kwenye pay roll ya Mafisadi. Bila aibu wala haya, utamsikia akisifa vilivyooza na kunuka, na kuponda vinavyong'ara. Haihitaji akili nyingi kuacha kumsikiliza. Ndio maana huo utumbo ambao ameufanya leo nimeusoma humu jamvini. Siwezi kumpa hata sekunde yangu moja kumsikiliza. Hata pale anapojipendekeza kuwa MC kwenye matukio fulanifulani. Sio tu KUMPUUZA, bali KUTOKUMSIKILIZA kabisa. HANA ANCHOWEZA kukuelimisha.
Kibonde anaongea nini na division 0 lake la form iv.
Mtangazaji wa Kituo Cha Redio cha CLOUDS FM, Bw. Efraim Kibonde ametoa ''kali ya mwaka'' pale alipojitosa mzima mzima kumsafisha Rostam Azizi kupitia kipindi chake cha Jahazi.
My Take;
1>Kibonde apuuzwe tu, kwani anafahamika ni puppet wa mafisadi akitumika kuwasafisha kupitia vipindi vyake Redioni.
Wewe nawe usiwe mgeni wa TAKUKURU,Unasahau kwamba ndio iliyomsafisha A-Ch kua hahusiki na kashfa ya Rada wakati riport ya kamati ya bunge iliyoongozwa na Bw. Ndugai unamtaja waziwazi?Vipi unasahau kua TAKUKURU ilishawahi kuchunguza sualala la RICHMOND na wakadai hakukua na dalili zozote za rushwa?Utasahau vipi kua yapo mambo makubwa tu ikiwamo EPA ambapo TAKUKURU ''walipeta'' mpaka wananchi walivyopiga kelele ndo nao wakaibuka wakati fedha zishatafunwa?SIFUTI KAULI!!..........................pili kaka shark futa kauli yako kua takukuru imebobea kwa rushwa